Tanzania na uwekezaji

Ngamanya Kitangalala

JF-Expert Member
Sep 24, 2012
501
1,214
Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na wawekezaji inatarajiwa kuanza kutekeleza miradi miwili mikubwa kabisa ya kimkakati( Strategic projects) katika ukuaji wa uchumi wetu

Kwanza, ni mradi wa kuchakata gas asilia, Liquefied Natural Gas( LNG) plant katika mkoa wa Lindi, mradi huu unatekelezwa kwa pamoja kati ya TPDC kwa upande wa serikali ya Tanzania, kwa kushirikiana na makampuni makubwa ya mafuta na gas hapa duniani, yakiongozwa na Equinor ya Norway, Royal Dutch Shell, Exxon Mobil na Ophir Energy, Tanzania inakadiriwa kuwa na hifadhi ya gas( Gas reserve) yenye ujazo wa cubic feet 57.54 milioni

Mradi huu mkubwa kabisa kuwahi kutokea katika nchi za Afrika mashariki, wenye thamani ya $30 billion unatarajiwa kuanza kutekelezwa mwaka 2022 na kukamilika mwaka 2028, kukamilika kwa mradi huu, inatarajiwa itaongeza ukuaji wa uchumi wetu kutoka 7% ya sasa mpaka 9% kwa mwaka

Mradi mwingine, ni mradi wa ujenzi wa kiwanda kikubwa cha kutengeneza mbolea katika mkoa wa Pwani, mradi huo wenye thamani ya $1.9 billion, utatekelezwa kwa pamoja kati ya TPDC kwa upande wa Tanzania na makampuni ya Ferrostaal ya Ujerumani, Haldor Topsoee ya Denmark na Fauji Fertilizer Company kutoka Pakistan, mradi unatarajiwa kuanza kutekelezwa mwaka 2021 na kukamilika mwaka 2024

Kiwanda hicho ndio kitakuwa kiwanda kikubwa kabisa cha kutengeneza mbolea katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na kati

Kukamilika kwa kiwanda hiki, kutasababisha hupatikanaji wa uhakika wa mbolea, na kitasaidia kushusha bei ya mbolea na kuongeza tija kwa wakulima wetu, hasa ukizingatia kilimo kimeajiri zaidi ya 75% ya watanzania na ndio sekta inayoongoza katika kuchangia kwenye pato ghafi la taifa( GDP) 29%

Binafsi napenda kuchukua fursa hii, kuipongeza sana serikali ya awamu ya tano, chini ya uongozi wa mheshimiwa Rais wetu Dr John Pombe Joseph Magufuli,kwa jitihada kubwa wanazochukua katika kukuza uchumi wetu na maisha ya watanzania wote kwa ujumla 👏🏿👏🏿👏🏿👏🏿👏🏿👏🏿👏🏿

Mungu ibaraki Tanzania
 
Unapenda kuota mchana.

Makampuni hayo uliyoyataja yalitaka kujenga kiwanda hicho. Uwekezaji wake ni U$30 billion. Serikali Kutokana na kuweka masharti magumu yasiyo ya kibiashara, makampuni hayo yaliacha huo mpango, na sasa wanajenga kiwanda hicho mjini Pemba-Mozambique kwa gharama ya u$28 billion. Juhudi za kuwarudisha kwa siku za karibuni zimegonga mwamba.

Nimeenda Pemba mara 3 kwa kazi maalum katika kipindi cha miezi 6. The place is really busy. We lost a rare opportunity kwa kujifanya wajuaji lakini ni ujuaji wa kijinga!

Ukijifanya mjuaji wakati hujui chochote, lazima uangukie pua.

Gas haipo Tanzania tu. Ukiweka masharti ya kipuuzi, itaendelea kubakia chini kama mapambo. Huko Mozambique, kiwanda kinajengwa, na uvumbuzi mpya unafanyika kila wakati.

Tunaweka masharti ya kijinga ambayo hayapo mahali popote Duniani. Uchimbaji gas, madini na biashara nzima ya madini na gas ni ya kimataif. Terms zako zikiwa za kijinga, utadharaulika na kuonekana hayawani. Wawekezaji wataenda mahali pengine, na Dunia hauwezi kusimama wala kuathirika kwa chochote kwa vile tu hawajachimba nchini mwako. Utabakia kama ulivyo. Huna uwezo wa kugundua hata ujazo wa cubic 1 ya gas wala kuchimba.

Unatakiwa uijue biashara, jenga mazingira competitive, wawekezaji wavutike kuja kwako, wananchi wako wanufaike na makampuni yaliyowekeza yanufaike pia. Ukiyafanya mazingira ya nchi yako kuwa hovyo, wataebda mahali pengine, kwenye nchi ambazo watu wanaelewa undani wa hiyo biashara.

Miaka 5 inaisha, hakuna mradi mkubwa wa uwekezaji mpya hata mmoja. Hayo ndiyo mafanikio ya awamu hii.
 
Unapenda kuota mchana.

Makampuni hayo uliyoyataja yalitaka kujenga kiwanda hicho. Uwekezaji wake ni U$30 billion. Serikali Kutokana na kuweka masharti magumu yasiyo ya kibiashara, makampuni hayo yaliacha huo mpango, na sasa wanajenga kiwanda hicho mjini Pemba-Mozambique. Juhudi za kuwarudisha kwa siku za karibuni zimegonga mwamba.

Ukijifanya mjuaji wakati hujui chochote, lazima uangukie pua.

Gas haipo Tanzania tu. Ukiweka masharti ya kipuuzi, itaendelea kubakia chini kama mapambo. Huko Mozambique, kiwanda kinajengwa, na uvumbuzi mpya unafanyika kila wakati.
Haya mambo ya gas, Magufuri angekubali tu hajui ampigie magoti profesa muhongo arudi kazini
 
Back
Top Bottom