Tanzania Mpya Hiyooo Inakaribia !

Tanzania Mpya Hiyooo Inakaribia !

Mfikirishi

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2012
Posts
10,405
Reaction score
12,096
Wakuu!

Nimekuwa nikifuatilia kwa karibu matukio yanayotokea nchini na nimebaini kuwa ni jambo la muda tu ili tuifikie Tanzania yenye maendeleo; nchi yenye uchumi wa kati barani Afrika. Imetuchukua muda mrefu kufika huko kwa sababu ya uelewa duni wa wananchi na fikra potofu za watawala kuwa maendeleo yetu yataletwa na misaada toka kwa wajomba!

Kwa muda mrefu sasa tulikuwa tumesinzia tukitegenea IMF, WB na wahisani watuamshe! Rasilimali tunazo za kutosha angani, juu ya ardhi, ndani ya maji na chini ya ardhi! Napata faraja ninapowaona wananchi wengi wanakuza uelewa wao kuhusu utajiri wa nchi yao! Pamoja na watawala kufanya kila aina ya hila ili tu wananchi wasijue utajiri wa nchi yao lakini wengi wanazidi kufunguka macho na masikio! Ukisikia watu wanavyojenga hoja kuanzia kwenye vijiwe vya kahawa kwa haraka unagundua kuwa Tanzania ya sasa si ile ya 1987!

Nadiriki kukiri kuwa ipo siku na haipo mbali sana...ipo siku ambayo watanzania kwa umoja wao bila kujali tofauti zao, bila kujali wanakotoka, bila kujali hali ya hewa, bila kujali gharama wanayoingia kwa sasa na bila kujali muda wala nguvu zao... kwa wingi wao wataungana na kufanya maamuzi Hiyo siku imezuiliwa sana kwa mabavu, hoja muflisi, hadaa za hapa na pale! Lakini kwa sasa hiyo siku imekaribia na hakuna wa kuizuia!

Lakini kufika huko tunahitaji kuunganisha nguvu zetu na kuwaelimisha wananchi hasa wa vijijini! Napongeza juhudi za Kinana na timu yao wanaozunguka kuwaelimisha wananchi kuhusu udhaifu wa Serikali yao na utajiri wa nchi yao! Napongeza harakati za UKAWA kuimarisha juhudi zao za kuwafikia wananchi wakiwa wanaongea lugha moja! Upinzani umefanya mengi kutufikisha hapa tulipo!

Tunategemea muungano wa UKAWA utakuwa chachu ya kutufikisha kwenye Tanzania Mpya! Ili tufike huko tunahitaji kusema HAPANA KWA KATIBA PENDEKEZWA! Mchakato wa Katiba mpaka sasa umewasaidia wananchi kujua maadui zao! Kwa sasa ni rahisi sana kufikisha ujumbe na ukaeleweka vema!
 
Viongozi wa TZ ni walewale tu fikra mbovu cdhani kama hao ukawa ndio watakaoleta chachu ya maendeleo.
 
Hii ni mara ya pili naona post yako...naomba kusema unajitahidi sana kuleta mada zenye mantiki na maana naamini tutakua pamoja
 
IMF na WB ndio zilitukomboa tulipokuwa tunakaa foleni hata ya mkate. Usisahau hilo.

Mpango wa Kikwete kututoa kwenye umasikini umefanikiwa kwa kiwango kikubwa kuliko Rais yeyote wa kabla yake. Katutoa Tanzania katika chini ya dollar moja kwa siku na sasa tunapaa. Malengo na mkakati wake wa 2025 tuwe tumeshafikia middle income status yako pale pale na yanakwenda vizuri sana.

Yeyote atakaekuja baada ya Kikwete anakuta ubwabwa umeshapikwa yeye ni kupakuwa na kula tu.
 
Tatizo kuna watu hawataki mabadiliko, tuwape nafasi tuone ndio tukosoe.
 
Mungu Awalaani Vibaya Wanaotuongoza Cc Kama Vipofu..N Wakae Wakijua Ipo Cku Kipofu Ataona Mwanga Wa Jua Hapo Ndo Baraa Litapoa Anza Maana Jua Litakuwa Limepoteza Nuru Yake Kwa Kuranguliwa Na Viongozi Wasio Waadilifu. Hakuna Kipofu Atakae Kubari Kuzibiwa Hata Huu Mwanga Wa Jua
 
Watu huwa mara nyingi hatujui tunachotaka unless somebody atuonyeshe. Ndio maana hatuna budi kuwapa nafasi Hawa watu watuonyeshe Kama wanayoyasema ni kweli ama lah.
 
IMF na WB ndio zilitukomboa tulipokuwa tunakaa foleni hata ya mkate. Usisahau hilo.

Mpango wa Kikwete kututoa kwenye umasikini umefanikiwa kwa kiwango kikubwa kuliko Rais yeyote wa kabla yake. Katutoa Tanzania katika chini ya dollar moaja kwa siku na sasa tunapaa. Malengo na mkakati wake wa 2025 tuwe tumeshafikia middle income stattus yako pale pale na yanakwenda vizuri sana.

Yeyote atakaekuja baada ya Kikwete anakuta ubwabwa umeshapikwa yeye ni kupakuwa na kula tu.

unawajua IMF na WB ni akina nani?? hakuna nchi yeyote duniani iliyoendelea kwa kufuata masharti ya IMF or WB kwani mashirika hayo katika biashara ya kukomboa watu bali to make money for their investors the key is rob the poor for the rich.

unadai kafanikiwa kututoa kwy umaskini wapi source inayosema umaskini umepungua Tanzania ??

maendeleo duniani yanaletwa na vitu viwili tu Labour na Equity na siyo huyo Prof. wa kichina sina haja ya kutoa somo la uchumi sidhani hata kama utaelewa anyway.
 
IMF na WB ndio zilitukomboa tulipokuwa tunakaa foleni hata ya mkate. Usisahau hilo.

Mpango wa Kikwete kututoa kwenye umasikini umefanikiwa kwa kiwango kikubwa kuliko Rais yeyote wa kabla yake. Katutoa Tanzania katika chini ya dollar moja kwa siku na sasa tunapaa. Malengo na mkakati wake wa 2025 tuwe tumeshafikia middle income status yako pale pale na yanakwenda vizuri sana.

Yeyote atakaekuja baada ya Kikwete anakuta ubwabwa umeshapikwa yeye ni kupakuwa na kula tu.


Kwenda shule kuzuri, tutafika lakini kwa elimu yetu hi hii ndogo tuliyonayo
 
Fikra kama hizi nafasi yake ni ndogo sana kwenye ujenzi wa jamii mpya ziliwahi kushindwa kwenye mataifa mengi zitashindwa hata tanzania pia.
 
Watu huwa mara nyingi hatujui tunachotaka unless somebody atuonyeshe. Ndio maana hatuna budi kuwapa nafasi Hawa watu watuonyeshe Kama wanayoyasema ni kweli ama lah.
Sidhani kama ni sahihi kuonja sumu,hawa watu wanaojiita ukawa siyo watu wa kupewa nchi hata kidogo wao malengo yao ni kugawana vyeo wala siyo kuleta maendeleo ya taifa hili ni vema kuwapima kwa kina kabla ya kufanya chochote.
 
Back
Top Bottom