Tanzania inaendeshwa kibepari au kijamaa?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
21,441
40,534
Pamoja na mikanganyiko miingi iliyoko kwenye Jamii yetu kuhusu mambo ya kisiasa na kijamii, kuna jambo nataka kulijua. Ili nchi isonge mbele kiuchumi na kijami ni lazima kuwepo na sera zinazoongoza masuala hayo ya Kiuchumi na kijamii. Na sera hizo ni lazima zijengwe juu ya msingi wa mfumo wa uendeshaji mambo unaofuatwa na nchi husika.

Kwa mfano Misingi ya Chama cha "Democratic" na "Republican" vya Marekani kuhusu binadamu inatofautiana kabisa. Demokratik chenyewe kinaamini kuwa Binadamu ni mtu huru na anatakiwa kulindwa ili autumie uhuru wake huo kwa ukamilifu.

Ndiyo maana huwa Demokratik ikishika uongozi wa nchi ya Marekani basi na sera za nchi hiyo kuhusu mambo yafuatayo hubadilika. Kwanza ushoga huruhusiwa na mashirika yanayopiganiA haki za ushoga na usagaji husaidiwa fedha na taasisi za Kiserikali kama vile USAID na zinginezo. Utoaji mimba huwa ni jambo linaloruhusiwa na utaona wanaotaka utoaji mimba liwe jambo la kisheria wanapata nguvu sana kwa kuwa serikali ya shirikisho huwa inawaunga mkono.

Hoja kubwa ya Demokratik ni kwamba kama mtu anataka kutoa mimba wewe ambaye si sehemu ya mimba hiyo unaathirika kivipi. Au mtu anapenda kuwa shoga wewe ambaye jirani yake utapatwa na nini kwa yeye kuwa shoga au Msagaji? Demokratiki ni waungaji mkono wakubwa sana wa hoja ya kuwasaidia wagonjwa mahututi kujitoa uhai kwa usaidizi wa "wataalam" ili waondokane na mateso yanayowakabili.

Kwa hiyo utaona kwa sasa kwa miaka kama 8 ambayo Marekani inaongozwa na Demokratik na sera za nchi hiyo kuhusu ushoga zimebadilika. Kwa sasa majimbo yanayoruhusu watu kujitoa uhai yameongezeka, yanayokubali ndoa za jinsia moja yapo ya kutosha na watu wanaotoa mimba "Kisheria" wamekuwa wengi zaidi kuliko wakati nchi hiyo inaendeshwa na chama cha Republikan.

Ingawa Demokratik nao wana sifa nyingine nzuri ambayo mara nyingi huchaguliwa wakati uchumi wa nchi hiyo unapokuwa umedorora na wao hufanikiwa kuufufua, lakini pia wao huwa hawapendi kuingilia sana mambo ya mataifa mengine kutokana na misingi ya chama hicho kuamini kuwa kila mtu anao uhuru wa kujiamulia mambo yake mwenyewe bila ya kuingiliwa ingiliwa.

Republikan wao ni wahafidhina (Conservatives) wanaamini mtu ni mali ya jamii! Ndiyo maana wao huzuia utoaji wa mimba, huzuia ushoga na usagaji, hawaungi mkono kujiua kwa hiyari, wanapenda kuingilia mambo ya nchi nyingine kwa sababu hiyo wao ndiyo mara nyingi huanzisha vita na nchi nyingine na kutumia hela nyingi kwa ajili ya vita hizo na kuleta mdororo wa kiuchumi katika nchi yao.

Nimetoa mifano hiyo ili kuonesha misingi ya vyama au nchi jinsi inavyoathiri utungaji sera wa nchi husika. Kwa misingi hiyo ndiyo maana nataka kujua kwa sasa misingi ya uendeshaji wa mambo katika nchi yetu kisiasa ni ya Kijamaa au ni ya kibepai? Yaani sera za nchi yetu zinatungwa juu ya msingi wa Kijamaa au Juu ya Msingi wa Kibepari?
 
Last edited:
tunatumia msingi ulioko katikati ya misingi hiyo uliyoitaja! inaitwa Idd Amin style!
 
Tunatunga sera za kiuchumi na kijamii ktk misingi ya confusionist ideology, to put your argument into perspective.
 
Mkuu usipate shida, TZ kwa sasa tunafuata mfumo wa matamko tu! Huu ni mfumo tuliojitengenezea wenyewe!

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Mwalimu Nyerere aliamini katika ujamaa, vita ya kagera ikatutandika kweli kiuchumi, madhara yake ikabidi ageuke jiwe na kuanza kutekeleza masharti ya wazungu, ule ujamaa aliokuwa nao kichwani ukapoteza nguvu. Mzee Mwinyi akaamua kulegeza masharti ya uchumi, kila kitu rukhsa, tukaingia kwenye ubepari wa IMF. Mzee Mkapa akaingia madarakani akausimamia ubepari lakini kwa kukusanya kodi, baadae akaingia kwenye mtego wa ubepari wa hali ya juu wa kubinafsisha viwanda. Mzee Kikwete akaingia madarakani na kuuendeleza ubepari ule ule, kwa utafutaji wa wawekezaji. JPM anakusanya kodi, yeye ni muumini wa Tanzania kwanza, hahubiri utandawazi kama Mkapa, hayanyenyekei makampuni makubwa ya Magharibi (kwa mtazamo wangu). Kilicho muhimu ili nchi iweze kujiendesha na ikajitegemea kwa asilimia kubwa ni kuzipa kipaumbele kila aina ya rasilimali ilizojaliwa na Mungu. Kinyume na ukweli huo tutakuwa ni bendera hufuata upepo, fedha wakitoa wachina tunageukia upande wao, fedha wakitoa wamarekani tunawaheshimu. Kila kinachoweza kukusanywa kikikusanywa tutakuwa na nguvu ya kuamua tuishi kwa kutegemea mfumo wa maisha tutakaoupenda wenyewe. Kinyume cha hapo mfumo wowote tunaoletewa na wafadhili kwetu ni mzuri tu. Mwalimu Nyerere alisema "mjitegemee kwa kila hali", yale maneno hayawezi kupoteza maana hata siku moja.
 
JPM anakusanya kodi, yeye ni muumini wa Tanzania kwanza, hahubiri utandawazi kama Mkapa, hayanyenyekei makampuni makubwa ya Magharibi (kwa mtazamo wangu). Kilicho muhimu ili nchi iweze kujiendesha na ikajitegemea kwa asilimia kubwa ni kuzipa kipaumbele kila aina ya rasilimali ilizojaliwa na Mungu. Kinyume na ukweli huo tutakuwa ni bendera hufuata upepo, fedha wakitoa wachina tunageukia upande wao, fedha wakitoa wamarekani tunawaheshimu.

Kila kinachoweza kukusanywa kikikusanywa tutakuwa na nguvu ya kuamua tuishi kwa kutegemea mfumo wa maisha tutakaoupenda wenyewe. Kinyume cha hapo mfumo wowote tunaoletewa na wafadhili kwetu ni mzuri tu. Mwalimu Nyerere alisema "mjitegemee kwa kila hali", yale maneno hayawezi kupoteza maana hata siku moja.
Hata kama kodi inakusanywa na lengo likiwa ni kujitegemea, lakini kwa kutumia msingi wa Kijamaa au Kibepari? Magufuli kavunja mkataba na Kampuni gani ya kibepari iliyowekeza hapa Tanzania?
 
Hata kama kodi inakusanywa na lengo likiwa ni kujitegemea, lakini kwa kutumia msingi wa Kijamaa au Kibepari? Magufuli kavunja mkataba na Kampuni gani ya kibepari iliyowekeza hapa Tanzania?
Iwe ni ubepari au Ujamaa sio kitu muhimu sana, wapo mabilionea marekani ambao hawaoni taabu kujitangaza kama wao ni wajamaa, japo wamezungukwa na mabepari. Wapo matajiri Ulaya ya mashariki ambao hawaoni taabu kujitangaza kama wao ni mabepari japokuwa wamezungukwa na wajamaa. Wale mabilionea wa kirusi ambao leo hii wanamiliki vilabu vikubwa vya soka kama Chelsea wamelelewa katika misingi ya kijamaa, lakini ulipovunjika mfumo wa kijamaa wakawa na akili za kuutafuta ubepari na fursa za kifisadi zza kuiibia Russia zilipojitokeza, hawakuzifanyia makosa hata kidogo. Mfumo wa ujamaa na ubepari sio kama misahafu, inaweza kubadilika wakati wowote ule. Tunao mabepari Tanzania, tunao wajamaa pia. Nchi kama Norway na Sweden zinajiendesha kwa misingi ya kijamaa lakini makampuni yao yanapokuja kutafuta fursa Afrika, wanageuka kuwa mabepari. Tanzania itakayoweza kujitegemea itakuwa na uhuru wa kujiamulia mfumo wa kufuata kati ya ubepari na ujamaa.
 
Iwe ni ubepari au Ujamaa sio kitu muhimu sana, wapo mabilionea marekani ambao hawaoni taabu kujitangaza kama wao ni wajamaa, japo wamezungukwa na mabepari. Wapo matajiri Ulaya ya mashariki ambao hawaoni taabu kujitangaza kama wao ni mabepari japokuwa wamezungukwa na wajamaa. Wale mabilionea wa kirusi ambao leo hii wanamiliki vilabu vikubwa vya soka kama Chelsea wamelelewa katika misingi ya kijamaa, lakini ulipovunjika mfumo wa kijamaa wakawa na akili za kuutafuta ubepari na fursa za kifisadi zza kuiibia Russia zilipojitokeza, hawakuzifanyia makosa hata kidogo. Mfumo wa ujamaa na ubepari sio kama misahafu, inaweza kubadilika wakati wowote ule. Tunao mabepari Tanzania, tunao wajamaa pia. Nchi kama Norway na Sweden zinajiendesha kwa misingi ya kijamaa lakini makampuni yao yanapokuja kutafuta fursa Afrika, wanageuka kuwa mabepari. Tanzania itakayoweza kujitegemea itakuwa na uhuru wa kujiamulia mfumo wa kufuata kati ya ubepari na ujamaa.
Hilo la magufuli kuvunja mkataba na kampuni ya wazungu lipo juu ya ufahamu wangu, lakini ninachokueleza ni kuwa ujamaa na ubepari zinabakia kuwa ni dhana tu ikiwa lengo la uongozi wa nchi ni kuyagusa moja kwa moja maisha ya walio wengi. Hizo ni theories tu, ambazo hata hao waliozitunga hawana uwezo wa kuziishi. Haushangai rais wa marekani baada ya kuwa ameshashinda uchaguzi huwa anapewa miezi zaidi ya miwili kwa ajili ya kufundishwa miiko na maadili ya marekani?. Wanachokijali ni maslahi yao yatafikiwa vipi. Sisi wa dunia ya tatu ndio tumebaki kukariri hii mifumo ya kimaisha.
 
Iwe ni ubepari au Ujamaa sio kitu muhimu sana,
Najiuliza kama si muhimu kiasi hicho kuwa na falsafa ya kundeshea nchi. Ni kama mtu unataka kujenga nyumba halafu Fundi mwashi anakwambia kuwa si muhimu kuwa na Ramani la muhimu ni matofali na simenti, nondo na kokoto. Lakini Ramani si ndiyo inaweka msingi jinsi gani jengo litajengwa na litakuwaje?

wapo mabilionea marekani ambao hawaoni taabu kujitangaza kama wao ni wajamaa, japo wamezungukwa na mabepari. Wapo matajiri Ulaya ya mashariki ambao hawaoni taabu kujitangaza kama wao ni mabepari japokuwa wamezungukwa na wajamaa.
Hapa unazungumzia mtu mmoja mmoja. Ni kama kusema kuwa hata saudia kuna wakristo wakati unajua kwamba nchi hiyo inaendeshwa kiislam! Kama taifa Marekani ni ya Kibepari ingawa kuna watu wanatamani iendeshwe kiijamaa. Sisi ni wajamaa au ni Mabepari?

Wale mabilionea wa kirusi ambao leo hii wanamiliki vilabu vikubwa vya soka kama Chelsea wamelelewa katika misingi ya kijamaa, lakini ulipovunjika mfumo wa kijamaa wakawa na akili za kuutafuta ubepari na fursa za kifisadi zza kuiibia Russia zilipojitokeza, hawakuzifanyia makosa hata kidogo.
Hizi fikra za kusifia wizi kama ni kuona fursa zimo pia miongoni mwa hawa tuliowachagua?

Mfumo wa ujamaa na ubepari sio kama misahafu, inaweza kubadilika wakati wowote ule. Tunao mabepari Tanzania, tunao wajamaa pia.
Sawa hapa hatuzungumzii mtu mmoja mmoja bali tunazungumzia ngazi ya taifa!

Nchi kama Norway na Sweden zinajiendesha kwa misingi ya kijamaa lakini makampuni yao yanapokuja kutafuta fursa Afrika, wanageuka kuwa mabepari. Tanzania itakayoweza kujitegemea itakuwa na uhuru wa kujiamulia mfumo wa kufuata kati ya ubepari na ujamaa.
Kwa ivo mpaka sasa hatujaamua tutumie sera gani kuelekea huko kwenye kujitegemea?
 
Najiuliza kama si muhimu kiasi hicho kuwa na falsafa ya kundeshea nchi. Ni kama mtu unataka kujenga nchi halafu Fundi mwashi anakwambia kuwa si muhimu kuwa na Ramani la muhimu ni matofali na simenti, nondo na kokoto. Lakini Ramani si ndiyo inaweka msingi jinsi gani jengo litajengwa na litakuwaje?

Hapa unazungumzia mtu mmoja mmoja. Ni kama kusema kuwa hata saudia kuna wakristo wakati unajua kwamba nchi hiyo inaendeshwa kiislam! Kama taifa Marekani ni ya Kibepari ingawa kuna watu wanatamani iendeshwe kiijamaa. Sisi ni wajamaa au ni Mabepari?

Hizi fikra za kusifia wizi kama ni kuona fursa zimo pia miongoni mwa hawa tuliowachagua?

Sawa hapa hatuzungumzii mtu mmoja mmoja bali tunazungumzia ngazi ya taifa!

Kwa ivo mpaka sasa hatujaamua tutumie sera gani kuelekea huko kwenye kujitegemea?
Sisi tulitaka kuwa wajamaa safari yetu ikaishia njiani, tunapenda kuwa mabepari lakini misingi yetu bado ni mibovu. Tunaelea katikati, na yapo mengi tunayoyakosa ambayo kama tungekuwa nayo tungeweza kuwa na itikadi maalum tunayoifuatia. Na sio serikali kuu peke yake hata vyama vya upinzani havina itikadi maalum, zaidi ya kujipachika itikadi zitakazowapendeza wafadhili wetu.
 
Ki-Bepaja! Kwa kweli hatuna itikadi, sera wala mfumo wa maendeleo. Twataraji tu tutatokea kweupe!
 
Pamoja na mikanganyiko miingi iliyoko kwenye Jamii yetu kuhusu mambo ya kisiasa na kijamii, kuna jambo nataka kulijua. Ili nchi isonge mbele kiuchumi na kijami ni lazima kuwepo na sera zinazoongoza masuala hayo ya Kiuchumi na kijamii. Na sera hizo ni lazima zijengwe juu ya msingi wa mfumo wa uendeshaji mambo unaofuatwa na nchi husika.

Kwa mfano Misingi ya Chama cha "Democratic" na "Republican" vya Marekani kuhusu binadamu inatofautiana kabisa. Demokratik chenyewe kinaamini kuwa Binadamu ni mtu huru na anatakiwa kulindwa ili autumie uhuru wake huo kwa ukamilifu.

Ndiyo maana huwa Demokratik ikishika uongozi wa nchi ya Marekani basi na sera za nchi hiyo kuhusu mambo yafuatayo hubadilika. Kwanza ushoga huruhusiwa na mashirika yanayopiganiA haki za ushoga na usagaji husaidiwa fedha na taasisi za Kiserikali kama vile USAID na zinginezo. Utoaji mimba huwa ni jambo linaloruhusiwa na utaona wanaotaka utoaji mimba liwe jambo la kisheria wanapata nguvu sana kwa kuwa serikali ya shirikisho huwa inawaunga mkono.

Hoja kubwa ya Demokratik ni kwamba kama mtu anataka kutoa mimba wewe ambaye si sehemu ya mimba hiyo unaathirika kivipi. Au mtu anapenda kuwa shoga wewe ambaye jirani yake utapatwa na nini kwa yeye kuwa shoga au Msagaji? Demokratiki ni waungaji mkono wakubwa sana wa hoja ya kuwasaidia wagonjwa mahututi kujitoa uhai kwa usaidizi wa "wataalam" ili waondokane na mateso yanayowakabili.

Kwa hiyo utaona kwa sasa kwa miaka kama 8 ambayo Marekani inaongozwa na Demokratik na sera za nchi hiyo kuhusu ushoga zimebadilika. Kwa sasa majimbo yanayoruhusu watu kujitoa uhai yameongezeka, yanayokubali ndoa za jinsia moja yapo ya kutosha na watu wanaotoa mimba "Kisheria" wamekuwa wengi zaidi kuliko wakati nchi hiyo inaendeshwa na chama cha Republikan.

Ingawa Demokratik nao wana sifa nyingine nzuri ambayo mara nyingi huchaguliwa wakati uchumi wa nchi hiyo unapokuwa umedorora na wao hufanikiwa kuufufua, lakini pia wao huwa hawapendi kuingilia sana mambo ya mataifa mengine kutokana na misingi ya chama hicho kuamini kuwa kila mtu anao uhuru wa kujiamulia mambo yake mwenyewe bila ya kuingiliwa ingiliwa.

Republikan wao ni wahafidhina (Conservatives) wanaamini mtu ni mali ya jamii! Ndiyo maana wao huzuia utoaji wa mimba, huzuia ushoga na usagaji, hawaungi mkono kujiua kwa hiyari, wanapenda kuingilia mambo ya nchi nyingine kwa sababu hiyo wao ndiyo mara nyingi huanzisha vita na nchi nyingine na kutumia hela nyingi kwa ajili ya vita hizo na kuleta mdororo wa kiuchumi katika nchi yao.

Nimetoa mifano hiyo ili kuonesha misingi ya vyama au nchi jinsi inavyoathiri utungaji sera wa nchi husika. Kwa misingi hiyo ndiyo maana nataka kujua kwa sasa misingi ya uendeshaji wa mambo katika nchi yetu kisiasa ni ya Kijamaa au ni ya kibepai? Yaani sera za nchi yetu zinatungwa juu ya msingi wa Kijamaa au Juu ya Msingi wa Kibepari?


Acha kujidangnaya wewe, hakuna tofauti kati ya Democrats na Republican Marekani na kama ipo ni ndogo sana, kwanza Marekani ni de facto one party State kwa maana inaongozwa na vyama viwili tu ambavyo vyote vina sera sawa na tofauti ipo kwenye mambo madogo sana ambayo wala siyo muhimu, hivyo ni sawa kusema Marekani ina chama kimoja cha siasa!
 
Acha kujidangnaya wewe, hakuna tofauti kati ya Democrats na Republican Marekani na kama ipo ni ndogo sana, kwanza Marekani ni de facto one party State kwa maana inaongozwa na vyama viwili tu ambavyo vyote vina sera sawa na tofauti ipo kwenye mambo madogo sana ambayo wala siyo muhimu, hivyo ni sawa kusema Marekani ina chama kimoja cha siasa!
kwa hivyo unataka kutuambia kwamba Demokratik nao wanaiunga mkono Taasisi ya "Prolife" au Republikan wanaiunga mkono taasisi ya "Marie Stopes" ? Kama kuna utofauti unadhani unatokana na nini. Kwa mfano John Maccain Msimamo wake kuhusu wanajeshi wa Marekani Afghanistan unafanana na ule alio nao Obama. Hivi Bi Hilary Clinton sera yake kuhusu wahamiaji wa kutoka Mexico na nchi nyingine zinazozungumza kilatino inafanana na ile ya Donald Trump na kama haifanani ni kwa sababu imetokea tu?
 
A very good question , hata mimi nasubiri jibu na ningependa sana mkuu @Tandale One ajitokeze kusaidia hapa , maana inatuchanganya mara kasi zaidi nguvu zaidi , mara sijui tumbua jipu , ni vema tukaeleweshwa .
 
kwa hivyo unataka kutuambia kwamba Demokratik nao wanaiunga mkono Taasisi ya "Prolife" au Republikan wanaiunga mkono taasisi ya "Marie Stopes" ? Kama kuna utofauti unadhani unatokana na nini. Kwa mfano John Maccain Msimamo wake kuhusu wanajeshi wa Marekani Afghanistan unafanana na ule alio nao Obama. Hivi Bi Hilary Clinton sera yake kuhusu wahamiaji wa inafanana na ile ya Donald Trump inafanana na kama haifanani ni kwa sababu imetokea tu?



Kama kuna tofauti ni ndogo sana na ipo kwenye mambo ambayo siyo muhimu kama hayo ya kutoa mimba au kutotoa n.k lkn linapokuja kwenye maswala muhimu kabisa ya nchi vyama vyote viko sawa kwa mfano mambo ya kunusuru mabenki kwa kutumia fedha za walipa kodi (banks bail out) vyama vyote viko sawa, mambo ya vita kuna tofauti gani kati ya Obama na Bush?
Obama alikampeni akasema akiingia ataifunga Guantanamo mpaka leo hii miaka minane baadaye Guantanamo bado ipo, Obama alikampeni akawadanganya Wamarekani kwamba Bush ni mtu wa vita na yeye akiingia jambo la kwanza ni kurudisha majeshi ya Marekani kwao miaka minane baadaye Obama amevamia nchi nyingi klk Bush, ni nani kamuua Gadafi?
Bush alitengeneza Al kaida Obama kaja na Isis ukiangalia hakuna tofauti kati ya Al kaida na Isis isipokuwa jina tu lkn mbinu ni zile zile!
Kwenye mambo ya kuzuia Global warming Marekani ya Bush na ya Obama haina tofauti, hivyo utaona kwamba hivi vyama ni kiini macho tu na ndiyo maana hata Wamarekani wenyewe wengi huwa hawapigi kura kwa sababu hiyo wanaona kila chama kinachoingia hakuna lolote kubwa wanalofanya vita bado iko pale pale tu, financial crisis inayosababishwa na mabenki iko pale pale tu na Serikali bado inalipa mabenki yaliyosababisha financial crisis na haijalishi Chama gani kipo madarakani!
 
Ni kweli hakuna tofauti kati ya utawala wa Bush na Obama. Au ni kweli kwamba Demokratik na Republikan tofauti yao ni ndogo sana!? Katika hili Barbarosa hujitendei haki!!
 
Back
Top Bottom