Tanzania Heart Institute imeishia wapi?

Tanzania Heart Institute imeishia wapi?

SSH2025_2030

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2012
Posts
9,661
Reaction score
9,753
Wadau
Hii taasisi ya THI (Tanzania Heart Institute - About THI) bado inafanya kazi? maana pamoja na moyo wa Dr. Masalu (Mwanzilishi) wa kusaidia Watanzania kupata tiba ya moyo hapa hapa TZ wanasiasa wakaona dili lao la kupeleka wagonjwa wa moyo India litavurugwa wakaanza kumpikia majungu/mizengwe.

leo nimeangalia website yao naona information nyingi ni za 2008 na 2009. Yoyote mwenye info kuhusu hili, na je Wabunge hawawezi kuulizia hususani wakati wa bajeti ya wizara ya afya kuhusu mustakabali wa kuwasaidia wataalamu wazawa kama kina Dr. Masalu wenye nia ya ku-invest home?
 
Hivi hii ki2 haina uhusiano na ile Hosptal ya Moyo aliyokua anaijenga Mengi MOSHI magamba wakaifanyia hujuma?
 
Kamanda correction kwenye jina anaitwa Dr. Mansau sio Masalu
 
Wadau
Hii taasisi ya THI (Tanzania Heart Institute - About THI) bado inafanya kazi? maana pamoja na moyo wa Dr. Masalu (Mwanzilishi) wa kusaidia Watanzania kupata tiba ya moyo hapa hapa TZ wanasiasa wakaona dili lao la kupeleka wagonjwa wa moyo India litavurugwa wakaanza kumpikia majungu/mizengwe. leo nimeangalia website yao naona information nyingi ni za 2008 na 2009. yoyote mwenye info. kuhusu hili. na je Wabunge hawawezi kuulizia hususani wakati wa bajet ya wizara ya afya kuhusu mustakabali wa kuwasaidia wataalamu wazawa kama kina Dr. Masalu wenye nia ya ku-invest hom?

Nilikuwa na shangazi wa baba pale ilifungwa kimazingara flan wangonjwa wote wakapelekwa muhimbili nusu yao hawakulast wengi sana walitutoka,serikali inapenda unyonyaji ile hospital iliwazaidia sana watu sema wakuu flani walikuwa wanakosa ulaji kwa kusafirisha pipo nje wakaifunga.hata ile ya,mengi bado sanaa labda chadema iingie madarakani.
 
ile ya mengi ilikuaje?haijakamilika tu?mwenye info atujuze
 
Baada ya vuta nivute ya muda na serikali, walipiga mnada vifaa vyote vya hospital kwa kushindwa kulipa kodi ya pango kwa NSSF......hivyo jamaa alioata wafadhili, wanajenga hospital maeneo ya Boko, kuna wakati wafadhiri wake toka USA walikuja kukagua maendelo ya ujenzi wa mradi....kwa maana hiyo huduma kwa sasa zimesimama

Wadau
Hii taasisi ya THI (Tanzania Heart Institute - About THI) bado inafanya kazi? maana pamoja na moyo wa Dr. Masalu (Mwanzilishi) wa kusaidia Watanzania kupata tiba ya moyo hapa hapa TZ wanasiasa wakaona dili lao la kupeleka wagonjwa wa moyo India litavurugwa wakaanza kumpikia majungu/mizengwe. leo nimeangalia website yao naona information nyingi ni za 2008 na 2009. yoyote mwenye info. kuhusu hili. na je Wabunge hawawezi kuulizia hususani wakati wa bajet ya wizara ya afya kuhusu mustakabali wa kuwasaidia wataalamu wazawa kama kina Dr. Masalu wenye nia ya ku-invest hom?
 
Issue ya watu kupelekwa india ni deal la wakubwa ukihatarisha biashara yao wanakumaliza!

Wahindi wako corrupted sana ndio maana madaktari walipogoma "wakubwa" walitaka kuwakomoa kwa kuletewa madaktari kutoka kwa hao wanaofaidi kodi zetu hadi za wagonjwa wa malaria wanaopelekwa india!!
 
Ni kweli THI ilikuwa isaidia. Lakini hicho si kigezo cha kumfanya asilipe kodi ya pango. Pamoja na kusaidia huko si kwamba wagonjwa walikuwa wanatibiwa bure, walikuwa wanalipa na katika malipo hayo bila shaka mmiliki wa hospitali aliweka na asilimia fulani ya pango. Sasa inapotokea pango halipi unategemea mwenye nyumba afanyaje? Tumeshuhudia hata baadhi ya idara za serikali zikitolewa kwa nguvu kwenye nyumba za NHC baada ya kushindwa kulipa kodi. Mmiliki wa THI alijua anachokifanya na alijua hata asipolipa kodi atapata huruma ya kutoondolewa kutokana na huduma anayotoa huku akiendelea kuwalipisha wagonjwa gharama zenye mjumuisho wa kodi ya pango. Tusipende kuacha umaskini wetu ukatumika na wenye hela kama kigezo cha kujiongezea kipato pasipo kupitia njia halali.
 
Back
Top Bottom