Ulongupanjala
JF-Expert Member
- Apr 9, 2013
- 8,259
- 13,549
Habari zenu wote,
Naomba niliseme hili tatizo la kufutika kwa alama ya pundamilia (Zebra) kwenye barabara nyingi hapa Arusha mjini,imechukua miezi mingi kama sio miaka bila wahusika kulifanyia kazi,nakumbuka miaka michache nyuma niliona Rotary/Lions International wakipaka rangi hiyo mistari kwenye barabara ya jirani na TANESCO na TFA,lakini naona hawakumaliza kwa barabara zote.(Labda fungu liliisha)
Nimejiuliza ina maana TANROADS na halmashauri ya jiji,hawaoni kama hili ni tatizo,au hizo alama mwanzo zilichorwa kimakosa au wanataka watu wagongwe na magari/toyo wakivuka kwenye sehemu hizo ambazo madereva wengi wahasimami maana hakuna alaza ya Zebra tena?
Leo nitataja barabara mbili tu ambazo zilikuwa na Zebra na imefutika kwa muda mrefu sasa.
1.Barabara ya Namanga/Nairobi jirani na Triple A Night club
2.Barabara ya inayopita jirani na chuo cha ufundi Arusha(ATC) jirani na ghorofa za NHC (Kambi ya fisi)
Kama wao hawajui wapi palikuwa na alama hizo na zimefutika,nipo tayari kuwatembeza ili wajue na watuondolee kero hii inayotia aibu kwa mji kama wa Arusha tunaoita wa kitalii,lakini pia askari wa usalama barabarani nao hawaoni hili tatizo au wao wapu busy kuangalia over speed na kutofunga mkanda nk?
Tuna safari ndefu sana kuiona Tz tuitakayo!
Naomba niliseme hili tatizo la kufutika kwa alama ya pundamilia (Zebra) kwenye barabara nyingi hapa Arusha mjini,imechukua miezi mingi kama sio miaka bila wahusika kulifanyia kazi,nakumbuka miaka michache nyuma niliona Rotary/Lions International wakipaka rangi hiyo mistari kwenye barabara ya jirani na TANESCO na TFA,lakini naona hawakumaliza kwa barabara zote.(Labda fungu liliisha)
Nimejiuliza ina maana TANROADS na halmashauri ya jiji,hawaoni kama hili ni tatizo,au hizo alama mwanzo zilichorwa kimakosa au wanataka watu wagongwe na magari/toyo wakivuka kwenye sehemu hizo ambazo madereva wengi wahasimami maana hakuna alaza ya Zebra tena?
Leo nitataja barabara mbili tu ambazo zilikuwa na Zebra na imefutika kwa muda mrefu sasa.
1.Barabara ya Namanga/Nairobi jirani na Triple A Night club
2.Barabara ya inayopita jirani na chuo cha ufundi Arusha(ATC) jirani na ghorofa za NHC (Kambi ya fisi)
Kama wao hawajui wapi palikuwa na alama hizo na zimefutika,nipo tayari kuwatembeza ili wajue na watuondolee kero hii inayotia aibu kwa mji kama wa Arusha tunaoita wa kitalii,lakini pia askari wa usalama barabarani nao hawaoni hili tatizo au wao wapu busy kuangalia over speed na kutofunga mkanda nk?
Tuna safari ndefu sana kuiona Tz tuitakayo!