TANROAD: Wekeni "Round About" Kupaenzi Sukamahela

TANROAD: Wekeni "Round About" Kupaenzi Sukamahela

Wickama

Platinum Member
Joined
Mar 8, 2009
Posts
1,568
Reaction score
1,350
Wakuu, muda mrefu tumeelezwa kuwa Mkoani Singida, Wilayani Manyoni, kijiji cha Sukamahela ndipo katikati ya Tanganyika. Tumeelezwa pia kwamba ma-surveyor wa mkoloni (niliambiwa wakijerumani) walichimbia alama (beacon) juu ya jabali kupatambua. Hii point na jabali ipo jirani na highway ya Dodoma-Singida. Kwa bahati mbaya haijageuzwa kuwa kivutio cha kitalii wala cha kiburudani kwa wasafiri. Yaani hata kijiji husika hakifaidi chochote. Kiufupi kwa sasa ni "chokambaya".

Screenshot_20250920_113246_Chrome~2.jpg

Screenshot_20250920_113441_Google~2.jpg

Screenshot_20250920_113551_Google~2.jpg


Mimi nawashauri Tanroads na mamlaka zingine hii sehemu ijengwe Round About kubwa itakayobeba sehemu za wasafiri kupumzika, kula, kupiga picha, stori, mikutano, harusi na mengineyo ili kupaenzi na kuieleza jamii yetu na hata wageni jiografia yetu. Kiasi hata wakazi wa hapo Sukamahela wafaidi jiografia yao.

Zipo nchi zimetengeneza roundabout kubwa kama hizo na zinavutia sana na kuingiza vipato (hii hapa chini ni Western Australia)
A4930-10-biggest-roundabouts-in-the-world-Image-15.jpg.webp

Picha: Nimezitoa Mitandaoni. Nawashukuru walioziweka
 
Inategemeana na kiongozi wa nchi anaona nini, Kiongozi wa nchi anaweza kuamuru ujenzi na ukaanza haraka. Hawa TANROAD wenyewe kama wenyewe hawajengi mpaka waamuriwe amri itoke juu
 
Hapo manyoni juu pale ndo patengenezwe round about.
kuna njia ya itigi,singida ,tabora.kwenye single face haiwezekani.hiyo batabara hapo ni njia ya singida.
we sema waweke vivutio tu vya watalii na wageni wanaopita hapo kupumzika.
 
Kwamba wakoloni walikuwa na muda wa kutafiti wajue katikati ya koloni lao!! Ili iweje sasa?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom