Mkuu haya ni mawe halisi,muundo wake niwa slate na hujulikana kama slate stones na nimaarufu kama Tanga stones kwa sababu hupatikana zaidi mkoa wa Tanga. Kwa kifupi ni mawe ambayo hutumika kwa urembo wa nyumba na maofisi,yanapendeza sana kwa finishing,unaweza kutumia chini badala ya pavers blocks,unaweza kutumia kwenye kuta za fensi vile vile unaweza kutumia kama tiles za jikoni,sebuleni,bafuni n.k kulingana na matakwa yako