Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Shirika la Umeme Tanzania - TANESCO

Verily Verily

Senior Member
Jan 4, 2007
188
143
Heshima kwenu wakuu,

Hii thread iwe Maalum kwa Maoni, Ushauri na Mapendekezo mbalimbali au kutoa Taarifa na changamoto Mbalimbali kwa Shirika la Umeme Tanzania TANESCO

Vilevile unaweza kutembelea thread hii =>Namba za simu za mameneja wa Wilaya (116) wa TANESCO kwa kila Mkoa

Kwa upande wangu Mimi namuomba, Mkurugenzi mpya wa TANESCO ajipange kudhibiti wizi wa umeme nchi nzima.

1. Mkurugenzi mpya Ndugu Tito Mwinuka ana jukumu kubwa mbele yake.

2. Upatikanaji wa Umeme wa uhakika na wa kutosha ndio ufunguo wa Tanzania ya viwanda.

3. Zaidi ya 50% ya watumiaji wa umeme nchini wamejiunganishia umeme kiholela na hivyo kusababisha hasara kubwa kwa shirika. Kwa hali ilivyo shirika haliwezi kufanya maendeleo iwapo wizi huu utaendelea.

4. Kuna mitaa ya pembezoni mwa jiji na mikoa kwa mfano utakuta karibu nyumba zote zinatumia umeme wa wizi.

5. Mkurugenzi mpya, akijua ana jukumu la kuipeleka nchi kwenye uchumi wa viwanda ajipambanue, ajitofautishe na watangulizi wake. Aanzishe mpango endelevu wa kutembelea nyumba kwa nyumba mtaa kwa mtaa akianzia miji mikubwa mpaka vijini na kuwachukulia hatua kali wezi wa umeme. Atoe adhabu ambayo watu hawatatamani kuiba umeme kamwe. Mpango huu uhusishe vyombo vya dola na sheria. Ikiwezekana bunge litunge sheria mahsusi ya kuliokoa taifa na wizi wa nishati ya umeme.

6. Sanjari na kukamata wezi nchi nzima atathimini bei za umeme ili wananchi hata wa kipato cha chini waweze kulipia badala ya kuiba.

7. Tafadhali Mkurugenzi ndugu Tito Mwinuka na TANESCO jibu hoja hizi kwa faida ya nchi.

Ninaweza kumsaidia kumuonyesha nyumba 3 Dar es salaam zinazotumia mita moja ya umeme na kwa mwezi hutumia umeme usiozidi shilingi 4000.

Pia Mwanza kuna mtu kaunganishiwa umeme bila mita na yeye kafungua tanesco yake kasambaza umeme ktk nyumba kibao,mwisho wa mwezi hao wateja humlipa yeye kiasi cha 10000 kila mmoja bila kujali matumizi yao maana hakuna mita,na yeye muhusika mkuu hutoa posho kwa baadhi ya watumishi wa tanesco wasio waadilifu
Hii huduma ina mambo mengi sana, vifaa ghali sana. wateje wezi wezi sana (wajanja wajanja), kufanikisha ulinzi na usalama wa huduma inaweza kukugharimu sana na kushindwa kufikia hata wanayofikia kwa sasa.

nadhani, elimu itolewe ya kutosha kwa wananchi, waeleweshwe umuhimu wa kulipa na kuacha wizi wa nishati hii muhimu kwa maisha yetu. kila mtu awe mhimili wa ulinzi na usalama wa miundombinu ya umeme.

Pia wangerekebisha tariff zao za manunuzi ya umeme toka kwa wazalishaji binafsi, wanunue kwa bei nzuri ili watu wengi wazalishe na kuwauzia TANESCO.

Nakumbuka hili (Mbeba nguzo mwizi, msoma meter mwizi, karani mwizi, mkurugenzi mwizi, hata mlipa bill (beneficiary)naye mwizi unadhan hapo kuna shirika????????)
Wanabodi kutokana na niliyoyashuhudia tanesco ya kigamboni,ni wazi kabisa jipu ambalo linahitaji kutumbuliwa.

Watu wengi wanaohitaji kufanyiwa survey ili wapate huduma hiyo,mteja huchangishwa kiasi kisichozidi shilingi za kitanzania 7,000/= ili kukodi gari litakalowawezesha kupita maeneo yao kupatiwa huduma hiyo.

Mtu yeyote asiekuwa na kiasi hicho ataishia kupigwa kalenda mpaka ajute kuisikia tanesco.
Serikali yetu tukufu wakati inafanya juhudi ya kuongeza pato la taifa, kwa kuhimiza mashirika ya uma kutafuta vyanzo vipya vya mapato tanesco kigamboni wanazirudisha nyuma jitihada hizo.

Kuna lundo la wateja ambao pamoja kuwa na pesa yao mkononi kwa ajili ya kupatiwa huduma lakini bado wananyanyasika na kutothaminiwa.
Nitowe wito kwa wizara husika wajaribu kufuatilia mwenendo wa tanesco kigamboni dhidi ya wateja wao katika kutoa huduma kwani ni jibu. Nina ushahidi wa kutosha juu ya hili ikiwemo audio na video.
Nitakribani mwaka mpango wa kuweka umeme kweye baadhi ya maeneo umekuwa ukitekelezwa kwa kusua sua.

Tumeshuudia nguzo kubwa wa umeme mkubwa (HT) zikichukua takribani miezi nane na zaidi. Usambazaji wa nguzo za umeme mdogo zimechukua miezi karibia mitano. Transforma zilichelewa mpaka watu wakatishia kuandamana ndo tukaona zina tundikwa.

Sasa cha kushangaza pamoja na juhudi zote hizo upatikaji wa META umekuwa mgumu sana. Vishoka wa Tanesco wanaitaji mpaka shilingi laki moja na nusu ili upata hiyo meta. Ili hali umeme watu wemeisha lipia shilingi laki tatu na elfu ishirini na tisa.

Tafadhali mkuu njoo hapa Tanesco Mbeze uwatumbue hawa watendaji. Tumechoka na majibu yao yanayokatisha tamaa.
 
Afike katika ofisi za zone na regional, huku ndio kumejaa uozo kabisa
 
8.ahakikishe taasisi zote za serikali na serikali kuu wanalipa madeni yao na ikiwezekana wawekewe mita za LUKU.
 
Nakubaliana na hoja kuwa serikali ndiyo imeingiza shirika katika kichaka ambacho ni ngumu kutoka bila ya mkono wa serikali.
 
Hawezi kufanya hayo kama watafanikiwa system nzima ya uongozi. Kuna mameneja wamekaa vituoni wanaona kama ofisi ni za kwao. Wamesahau wajibu.

Kuongeza kipato wafungie watu umeme hata kwa mkopo. Kuliko mtu unalipa service line unakaa miezi saba mpaka mwaka hujafungiwa umeme. Wakopaji umeme daraja la kati wapangwe upya. Huwezi kumuweka mtumiaji wa unit 300 awe daraja moja na anae tumia unit 5000 hii ni kukosa kufikiria.
 
Nimeingia kwenye uzi kwa pupa kwa kudhani huyu jamaa mpya anaanza kwa promo kali hizi atafika kweli?Kumbe ni mswahili katoa conspiracy theories zake tu bila statistics....duh
 
Mie ntamwona wa maana kama maombi ya wanaotaka umeme yanafanyiwa kazi kwa wakati. Mtu kalipia umeme mwezi wa kumi mpaka leo hii hajawekewa umeme. Upuuzi
Bora wewe mwezi wa kumi. Mimi ni mwezi wa sita mwaka jana. Hadi leo hakuna huduma.
 
Maoni mazuri
Pia aangalie Maofisi ya mikoani na Wilayani
Huko kuna matatizo sana
 
Wizi hautaisha ikiwa mafundi wa Tanesco ndo wanafunga umeme kinyemela...siku mnaenda kufanya ukaguzi hao hao mafundi wanawataarifu watu wao wanyofoe nyaya
 
Aturejeshee fedha zetu tulizonunua nguzo kusogeza umeme karibu na nyumbani.Swala la kusema nguzo ni za TANESCO wakati nimelipia mimi halikubaliki.
 
Nguzo zisogezwe karibu na makazi ya watu. MTU unapomwambia alipie nguzo ni sawa na kumuomba mtaji. Watu wanashidwa kulipia nguzo ila wanaweza kulipia bili. Jitahidi uongeze wateja.
 
Mie ntamwona wa maana kama maombi ya wanaotaka umeme yanafanyiwa kazi kwa wakati. Mtu kalipia umeme mwezi wa kumi mpaka leo hii hajawekewa umeme. Upuuzi
Ninakubaliana na wewe.

Ni tanzania tu ambapo TANESCO wanadai wanajiendesha kwa hasara lakini ukitaka wakuunganishie umeme lazima kwanza utoe rushwa au usubiri milele.

Nchi za wenzetu unabembelezwa kuunganishiwa umeme lakini kwetu eti wewe mteja ndio unawabembeleza.
 
Namba 6 Ikifanyiwa Kazi Kama Ulivyo Shauri Nadhani Hiyo Ndiyo Itakuwa Dawa Mbadala Ya Wizi Wa Umeme.
 
Back
Top Bottom