Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,777
Askofu Jude Thadeus Ruwa'ichi akizungumza leo Oktoba 14, 2025 katika Misa ya Takatifu ya Hija ya UWAKA kuwategemeza Masista wa Shirika la Dada Wadogo Visiga Pwani, jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam ametoa tamko la baraza la maaskofu kupitia kamati ya haki na amani kuhusu uchaguzi mkuu 2025 na utekaji unaoendelea
"Tunapoazimisha siku ya mwalimu Nyerere na kumkumbuka baba wa taifa tunatafakari pia juu ya nchi yetu na ustawi wa watanzania kwa ujumla wake. Tunatafakari nchi yetu katika historia yake na uchaguzi mkuu. Ndugu zangu tukio la uchaguzi mkuu ni tukio la kikatiba kwani hapo ndipo wananchi wanategemewa kuwapa waliowachagua dhamana ya kutawala na kuongoza nchi."
" Ibara ya nane ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaweka wazi kuwa mamlaka ya nchi yamo chini ya wananchi na serikali huwajibika kwa wananchi, serikali ikiwa na wajibu wa kulea na kuleta ustawi wa watu wote bila ubaguzi wa aina yoyote."
UCHAGUZI MKUU NA MATUKIO YA UTEKAJI YANAYOENDELEA
"Tume ya haki na amani ya baraza la maaskofu katoliki Tanzania ambayo ninaiongoza, kwa kulitazama tukio la uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 inasikitishwa na hali inayoendelea ya kupotea na kutekwa watu. Utekaji huu unaonekana unaendeshwa kwa mpango wa kikundi maalumu ambacho kinatekeleza uovu huu sehemu mbalimbali za nchi yetu. Utekaji huu umepelekea ulinzi wa haki ya uhai ambayo ni haki ya msingi kupotea kwani hatusikii walioapa kulinda uhai wa watanzania kulaani au kukomesha huu utekaji na kutoweka kwa watu."
"Ni takriban zaidi ya miaka miwili matukio haya yamezidi kukithiri na kuwafanya watanzania wajiulize watekaji hawa wawe na nguvu kuliko vyombo vya ulinzi wa watu na kuliko wale wenye mamlaka ya kuwaletea watu matumaini ya kuishi na ustawi wake.
Dalili za kukomesha utekaji hazionekani wala hatusikiii kulaaniwa kwa matukio hayo. Ikumbukwe kuwa uhai wa kila mwanadamu unadhihirisha utukufu wa Mungu. Mwanadamu ameumbwa kwa sura na mfano wa Mungu, ni kiumbe wa pekee ambaye hakuna mwenye haki au mamlaka ya kumuondolea uhai wake kazi ya serikali ni kulinda uhai wa kila mwanadamu.
Kwa mujibu wa ibara ya 14 ya katiba ya Tanzania kila mtu ana haki msingi ya uhai wake na kuhakikishiwa kuwa haki hii inalindwa kwa gharama zozote zile.
Maaskofu tunataka serikali kuhakikishia raia na watu wote usalama wa haki ya uhai kwa kila mtu bila ubaguzi wowote. Uchaguzi mkuu una maana tu endapo watu wanapata viongozi wenye kulinda na wenye kutetea uhai. Wagombea wa vyama na vyama vyao kwa mujibu wa ibara ya tatu na ya tano walipaswa kuonesha uwezo na moyo wa kushinda watekaji na wauaji. Sheria zipo zinazoonesha jinsi ya kushughulikia wahalifu, kwanini basi waliopotea na kutekwa hawapatikani mahabusu?
Tunaitaka serikali izingatie kanuni ya utawala wa sheria na kuheshimu kimatendo haki ya kimsingi ya kila mwanadamu.
WITO KWA RAIA WOTE KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025
Kuelekea uchaguzi mkuu nawaomba raia wote kuongozwa na dhamiri iliyo safi iliyo hai na yenye kuongozwa na ukweli halisi wenye kuzingatia hofu ta Mungu, utu wa mtu, historia nzuri ya taifa letu, umoja na mshikamano wa taifa letu, dhamiri hai na safi yenye kufanya maamuzi sahihi, kuzingatia hofu ya Mungu na utu wa mtu kama Mungu alivyowakilisha kwenye dhamiri yake, na hivyo dhamiri hii ni mahali pa kila mwanadamu kupima na kufanya maamuzi yanayobeba hadhi ya utu na kuwajibika kwake mbele ya Mungu.
Mpiga kura na mpigiwa kura mnaalikwa kuheshimu dhamiri juu ya suala hili la uchaguzi mkuu, msirubuniwe kwa vitisho wala rushwa. usirubuniwe kwa namna yoyote ile.
WITO KWA WANASIASA, VYAMA NA SERIKALI
Tunaiomba serikali na wale wenye mawazo tofauti ya masuala ya uchaguzi muongozwe na utamaduni wa mazungumzano katika kutekeleza haki, msingi za kisiasa kadiri ya ibara ya 21 ambapo kila raia ana haki hizo.
Wanasiasa kupitia vyama na serikali kaeni mzungumze, wahakikishieni watu haki zao. Nguvu ya wananchi ipo kwenye hoja siyo kwenye mabavu na hila. seriksli kupuuza wanaolalamika sio afya wala tija kwa taifa letu, wakati uliokubalika kuzungumza na sasa na wala hamjachelewa.
'Hatuchelewi kujisahihisha wala kutenda mema' Barua ya pili ya Paulo kwa Wakorinto 6:2.
Tunaiomba serikali iwasikilize raia wenye malalamiko yao ya haki zao za kisiasa. Unyenyekevu mbele ya Raia hujengeka kwenye ukweli na uwazi. Kiongozi wa watu akiwa mnyenyekevu ni mkweli na anaaminika na watu wote. tukumbuke kuwa historia ya uchaguzi katika nchi yetu kuanzia 1962 mpaka 2015 zilithibitika na ziliaminika viongozi wakapatikana hata kama zilikuwa na mapungufu yake.
Nawatakieni uchaguzi mkuu wa haki, wa ukweli, wa uhuru na wa kuaminika mwaka huu 2025"
"Tunapoazimisha siku ya mwalimu Nyerere na kumkumbuka baba wa taifa tunatafakari pia juu ya nchi yetu na ustawi wa watanzania kwa ujumla wake. Tunatafakari nchi yetu katika historia yake na uchaguzi mkuu. Ndugu zangu tukio la uchaguzi mkuu ni tukio la kikatiba kwani hapo ndipo wananchi wanategemewa kuwapa waliowachagua dhamana ya kutawala na kuongoza nchi."
" Ibara ya nane ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaweka wazi kuwa mamlaka ya nchi yamo chini ya wananchi na serikali huwajibika kwa wananchi, serikali ikiwa na wajibu wa kulea na kuleta ustawi wa watu wote bila ubaguzi wa aina yoyote."
UCHAGUZI MKUU NA MATUKIO YA UTEKAJI YANAYOENDELEA
"Tume ya haki na amani ya baraza la maaskofu katoliki Tanzania ambayo ninaiongoza, kwa kulitazama tukio la uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 inasikitishwa na hali inayoendelea ya kupotea na kutekwa watu. Utekaji huu unaonekana unaendeshwa kwa mpango wa kikundi maalumu ambacho kinatekeleza uovu huu sehemu mbalimbali za nchi yetu. Utekaji huu umepelekea ulinzi wa haki ya uhai ambayo ni haki ya msingi kupotea kwani hatusikii walioapa kulinda uhai wa watanzania kulaani au kukomesha huu utekaji na kutoweka kwa watu."
"Ni takriban zaidi ya miaka miwili matukio haya yamezidi kukithiri na kuwafanya watanzania wajiulize watekaji hawa wawe na nguvu kuliko vyombo vya ulinzi wa watu na kuliko wale wenye mamlaka ya kuwaletea watu matumaini ya kuishi na ustawi wake.
Dalili za kukomesha utekaji hazionekani wala hatusikiii kulaaniwa kwa matukio hayo. Ikumbukwe kuwa uhai wa kila mwanadamu unadhihirisha utukufu wa Mungu. Mwanadamu ameumbwa kwa sura na mfano wa Mungu, ni kiumbe wa pekee ambaye hakuna mwenye haki au mamlaka ya kumuondolea uhai wake kazi ya serikali ni kulinda uhai wa kila mwanadamu.
Kwa mujibu wa ibara ya 14 ya katiba ya Tanzania kila mtu ana haki msingi ya uhai wake na kuhakikishiwa kuwa haki hii inalindwa kwa gharama zozote zile.
Maaskofu tunataka serikali kuhakikishia raia na watu wote usalama wa haki ya uhai kwa kila mtu bila ubaguzi wowote. Uchaguzi mkuu una maana tu endapo watu wanapata viongozi wenye kulinda na wenye kutetea uhai. Wagombea wa vyama na vyama vyao kwa mujibu wa ibara ya tatu na ya tano walipaswa kuonesha uwezo na moyo wa kushinda watekaji na wauaji. Sheria zipo zinazoonesha jinsi ya kushughulikia wahalifu, kwanini basi waliopotea na kutekwa hawapatikani mahabusu?
Tunaitaka serikali izingatie kanuni ya utawala wa sheria na kuheshimu kimatendo haki ya kimsingi ya kila mwanadamu.
WITO KWA RAIA WOTE KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025
Kuelekea uchaguzi mkuu nawaomba raia wote kuongozwa na dhamiri iliyo safi iliyo hai na yenye kuongozwa na ukweli halisi wenye kuzingatia hofu ta Mungu, utu wa mtu, historia nzuri ya taifa letu, umoja na mshikamano wa taifa letu, dhamiri hai na safi yenye kufanya maamuzi sahihi, kuzingatia hofu ya Mungu na utu wa mtu kama Mungu alivyowakilisha kwenye dhamiri yake, na hivyo dhamiri hii ni mahali pa kila mwanadamu kupima na kufanya maamuzi yanayobeba hadhi ya utu na kuwajibika kwake mbele ya Mungu.
Mpiga kura na mpigiwa kura mnaalikwa kuheshimu dhamiri juu ya suala hili la uchaguzi mkuu, msirubuniwe kwa vitisho wala rushwa. usirubuniwe kwa namna yoyote ile.
WITO KWA WANASIASA, VYAMA NA SERIKALI
Tunaiomba serikali na wale wenye mawazo tofauti ya masuala ya uchaguzi muongozwe na utamaduni wa mazungumzano katika kutekeleza haki, msingi za kisiasa kadiri ya ibara ya 21 ambapo kila raia ana haki hizo.
Wanasiasa kupitia vyama na serikali kaeni mzungumze, wahakikishieni watu haki zao. Nguvu ya wananchi ipo kwenye hoja siyo kwenye mabavu na hila. seriksli kupuuza wanaolalamika sio afya wala tija kwa taifa letu, wakati uliokubalika kuzungumza na sasa na wala hamjachelewa.
'Hatuchelewi kujisahihisha wala kutenda mema' Barua ya pili ya Paulo kwa Wakorinto 6:2.
Tunaiomba serikali iwasikilize raia wenye malalamiko yao ya haki zao za kisiasa. Unyenyekevu mbele ya Raia hujengeka kwenye ukweli na uwazi. Kiongozi wa watu akiwa mnyenyekevu ni mkweli na anaaminika na watu wote. tukumbuke kuwa historia ya uchaguzi katika nchi yetu kuanzia 1962 mpaka 2015 zilithibitika na ziliaminika viongozi wakapatikana hata kama zilikuwa na mapungufu yake.
Nawatakieni uchaguzi mkuu wa haki, wa ukweli, wa uhuru na wa kuaminika mwaka huu 2025"