Tamko: CHAMA cha ACT-Wazalendo kinalaani vikali uamuzi wa Jeshi la Polisi kuzuia mikutano ya hadhara

ACT Wazalendo

JF-Expert Member
May 5, 2014
628
1,561
CHAMA cha ACT Wazalendo kinalaani vikali uamuzi wa jeshi la polisi kuzuia mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa uliotangazwa leo na Kamishna wa Polisi-Operesheni na Mafunzo Nsato M Msanzya-CP.

Ikumbukwe kuwa uamuzi huu wa jeshi la Polisi unafuatia kuzinduliwa kwa “Operesheni Linda Demokrasia” baada ya Wabunge saba wa vyama vya upinzani kusimamishwa Bungeni baada ya kupinga Kitendo cha Serikali kuzuia kurushwa kwa matangazo ya Bunge moja kwa moja.

Mikutano ya “Operesheni Linda Demokrasia” inayoratibiwa na Chama chetu ilipangwa kufanyika kwenye mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Kigoma, Katavi, Rukwa, Mbeya na Morogoro. Hadi sasa umeshafanyika mkutano mmoja jijini Dar es Salaam.

Pia Kiongozi wa Chama Ndugu Zitto ameitwa Polisi kituo cha Kati leo tarehe 7/6/2016. Ndugu Zitto ameitwa na Mkuu wa Upelelezi wa Kanda Maalumu ya Dar Es salaam Bwana. Wambura. Ameomba asiende leo kwa kuwa ni karibu na masaa ya kufuturu. Atakwenda kesho saa tatu asubuhi.

Chama chetu kinapinga vikali uamuzi huu wa jeshi la polisi kwa sababu hauna mashiko kwa kuwa haki ya vyama vya siasa kufanya mikutano ni ya kisheria kama ilivyoelezwa katika Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 1992 (kifungu cha 11(1)

Uamuzi huu wa Jeshi la Polisi unavunja haki ya raia kutoa maoni (Ibara ya 18(a) na uhuru wa kukusanyika (Ibara ya 20(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Sababu iliyotolewa na Jeshi la Polisi kuwa mikutano hii inalenga kuchochea wananchi kutotii sheria ni mwendelezo wa visingizio vya serikali vinavyolenga kuminya uhuru wa wananchi kuikosoa serikali na sasa Jeshi la Polisi limejiingiza katika kuisaidia serikali kutimiza matakwa yake ya ukandamizaji wa Demokrasia unaofanywa ndani na nje ya Bunge

Chama cha ACT-Wazalendo kinawasiliana na wanasheria wetu ili kupata tafsiri ya kimahakama ya uhalali wa jeshi la polisi kuzuia mikutano ya vyama vya siasa ambayo inatambuliwa na kulindwa na katiba.

Tunalikumbusha Jeshi la Polisi na serikali kwa ujumla kuwa hila hii ya kuzuia mikutano ya hadhara ya vyama vya upinzani kamwe haitazuia nia njema tuliyonayo wala kushusha ari yetu ya kuitetea na kuilinda misingi ya demokrasia inapokandamizwa na serikali.

Ado Shaibu,

Katibu Itikadi, Mawasiliano na Uenezi

ACT Wazalendo

Imetolewa leo tarehe 07 Juni 2016
 
Vyama vyote unganeni katika hii kesi tumechoka na haya mabavu.Polisi watoe ushahidi wa hizo taarifa zao za kintelijensia mahakamani.

UKAWA, pia fungueni kesi kuhoji uhalali wa fedha za umma zinazodaiwa kuokolewa/zilizobaki kutoka kwenye Taasisi za umma kukabidhiwa kwa Raisi badala ya kurudishwa Hazina.

Pia,muiombe mahakama izuie matumizi ya aina yoyote ya hizo fedha mpaka kesi ya msingi iishe.
 
CHAMA cha ACT Wazalendo kinalaani vikali uamuzi wa jeshi la polisi kuzuia mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa uliotangazwa leo na Kamishna wa Polisi-Operesheni na Mafunzo Nsato M Msanzya-CP.

Ikumbukwe kuwa uamuzi huu wa jeshi la Polisi unafuatia kuzinduliwa kwa “Operesheni Linda Demokrasia” baada ya Wabunge saba wa vyama vya upinzani kusimamishwa Bungeni baada ya kupinga Kitendo cha Serikali kuzuia kurushwa kwa matangazo ya Bunge moja kwa moja.

Mikutano ya “Operesheni Linda Demokrasia” inayoratibiwa na Chama chetu ilipangwa kufanyika kwenye mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Kigoma, Katavi, Rukwa, Mbeya na Morogoro. Hadi sasa umeshafanyika mkutano mmoja jijini Dar es Salaam.

Pia Kiongozi wa Chama Ndugu Zitto ameitwa Polisi kituo cha Kati leo tarehe 7/6/2016. Ndugu Zitto ameitwa na Mkuu wa Upelelezi wa Kanda Maalumu ya Dar Es salaam Bwana. Wambura. Ameomba asiende leo kwa kuwa ni karibu na masaa ya kufuturu. Atakwenda kesho saa tatu asubuhi.

Chama chetu kinapinga vikali uamuzi huu wa jeshi la polisi kwa sababu hauna mashiko kwa kuwa haki ya vyama vya siasa kufanya mikutano ni ya kisheria kama ilivyoelezwa katika Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 1992 (kifungu cha 11(1)

Uamuzi huu wa Jeshi la Polisi unavunja haki ya raia kutoa maoni (Ibara ya 18(a) na uhuru wa kukusanyika (Ibara ya 20(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Sababu iliyotolewa na Jeshi la Polisi kuwa mikutano hii inalenga kuchochea wananchi kutotii sheria ni mwendelezo wa visingizio vya serikali vinavyolenga kuminya uhuru wa wananchi kuikosoa serikali na sasa Jeshi la Polisi limejiingiza katika kuisaidia serikali kutimiza matakwa yake ya ukandamizaji wa Demokrasia unaofanywa ndani na nje ya Bunge

Chama cha ACT-Wazalendo kinawasiliana na wanasheria wetu ili kupata tafsiri ya kimahakama ya uhalali wa jeshi la polisi kuzuia mikutano ya vyama vya siasa ambayo inatambuliwa na kulindwa na katiba.

Tunalikumbusha Jeshi la Polisi na serikali kwa ujumla kuwa hila hii ya kuzuia mikutano ya hadhara ya vyama vya upinzani kamwe haitazuia nia njema tuliyonayo wala kushusha ari yetu ya kuitetea na kuilinda misingi ya demokrasia inapokandamizwa na serikali.

Ado Shaibu,

Katibu Itikadi, Mawasiliano na Uenezi

ACT Wazalendo

Imetolewa leo tarehe 07 Juni 2016
SO SAD HII NDO CCM SIKIVU MKUU.
 
CHAMA cha ACT Wazalendo kinalaani vikali uamuzi wa jeshi la polisi kuzuia mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa uliotangazwa leo na Kamishna wa Polisi-Operesheni na Mafunzo Nsato M Msanzya-CP.

Ikumbukwe kuwa uamuzi huu wa jeshi la Polisi unafuatia kuzinduliwa kwa “Operesheni Linda Demokrasia” baada ya Wabunge saba wa vyama vya upinzani kusimamishwa Bungeni baada ya kupinga Kitendo cha Serikali kuzuia kurushwa kwa matangazo ya Bunge moja kwa moja.

Mikutano ya “Operesheni Linda Demokrasia” inayoratibiwa na Chama chetu ilipangwa kufanyika kwenye mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Kigoma, Katavi, Rukwa, Mbeya na Morogoro. Hadi sasa umeshafanyika mkutano mmoja jijini Dar es Salaam.

Pia Kiongozi wa Chama Ndugu Zitto ameitwa Polisi kituo cha Kati leo tarehe 7/6/2016. Ndugu Zitto ameitwa na Mkuu wa Upelelezi wa Kanda Maalumu ya Dar Es salaam Bwana. Wambura. Ameomba asiende leo kwa kuwa ni karibu na masaa ya kufuturu. Atakwenda kesho saa tatu asubuhi.

Chama chetu kinapinga vikali uamuzi huu wa jeshi la polisi kwa sababu hauna mashiko kwa kuwa haki ya vyama vya siasa kufanya mikutano ni ya kisheria kama ilivyoelezwa katika Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 1992 (kifungu cha 11(1)

Uamuzi huu wa Jeshi la Polisi unavunja haki ya raia kutoa maoni (Ibara ya 18(a) na uhuru wa kukusanyika (Ibara ya 20(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Sababu iliyotolewa na Jeshi la Polisi kuwa mikutano hii inalenga kuchochea wananchi kutotii sheria ni mwendelezo wa visingizio vya serikali vinavyolenga kuminya uhuru wa wananchi kuikosoa serikali na sasa Jeshi la Polisi limejiingiza katika kuisaidia serikali kutimiza matakwa yake ya ukandamizaji wa Demokrasia unaofanywa ndani na nje ya Bunge

Chama cha ACT-Wazalendo kinawasiliana na wanasheria wetu ili kupata tafsiri ya kimahakama ya uhalali wa jeshi la polisi kuzuia mikutano ya vyama vya siasa ambayo inatambuliwa na kulindwa na katiba.

Tunalikumbusha Jeshi la Polisi na serikali kwa ujumla kuwa hila hii ya kuzuia mikutano ya hadhara ya vyama vya upinzani kamwe haitazuia nia njema tuliyonayo wala kushusha ari yetu ya kuitetea na kuilinda misingi ya demokrasia inapokandamizwa na serikali.

Ado Shaibu,

Katibu Itikadi, Mawasiliano na Uenezi

ACT Wazalendo

Imetolewa leo tarehe 07 Juni 2016
Mnatupotezea muda,, muda wa kampeni ulishaisha, huu ni wakati wa maendeleo
 
Hii gia ya taarifa za kiintelejensia ni hadaa tu!Wanashindwa kuwalinda raia wanaouwawa wanakalia siasa,jeshi limekosa weledi kabisa!
 
Ni lazima sasa kila mmoja wetu atumie kila njia inayofaa kupingana waziwazi na Udikteta huu.

Tanzania is gradually sliding into Dictatorship.

We must tame the dictatorship and mockery of Democracy.

Baada ya Vyama vya ACT-Wazalendo na CHADEMA kupanga mikutano ya Hadhara na Chama Cha ACT-Wazalendo kufanya Mkutano wa hadhara Dar Es Salaam kwa mafanikio na pia CHADEMA kuanza mikutano ya hadhara leo Jeshi la Polisi limeingia kiwewe na kutoa taarifa ya kupiga mikutano ya hadhara eti "Taarifa za Kiintelijensia zinaonyesha Dalili za Uvunjifu wa Amani"

Sio mara ya Kwanza Jeshi la Polisi kufanya hivyo.Lilifanya hivyo hata kwenye msiba wa Marehemu Mawazo na Ikabidi Tuende Mahakamani na mahakama ikaaamua kuwa Jeshi la Polisi halikua na uhalali wa kutoa amri za kuzuia mikusanyiko

Kisingizio kuwa tunachochea wananchi kuvunja sheria(Civil Disobedience) hakina Mashiko

Ni lazima tulinde misingi ya Demokrasia ambayo Katiba yetu imeweka

Ni haki ya watanzania kukusanyika na kutoa maoni yao kama ilivyo katika Ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ya Mwaka 1977.

Haki hii haiwezi kuporwa kwa amri zinazotolewa pasipokuwa na ushahidi wa kutosha au kwa matakwa ya watu fulani tu

Haki hii haiombwi bali inadaiwa

Utawala usiokubali kukosolewa Bungeni au kwa njia nyingine za kidemokrasia nje ya Bunge hauwezi kuwa salama madarakani

Jeshi la Makaburu la Afrika Kusini pamoja na kuwa na askari katili na wenye vifaa halikuweza kufua dafu mbele ya Umma wa Watu wa Afrika Kusini.Muda wote Serikali dhalimu ya Afrika kusini ilitetea sera yao ya ubaguzi wa Rangi na Makaburu hao wakawa wanajitetea kuwa wanatoa amri na kuongoza nchi kwa mujibu wa sheria(Chini ya Sera za Kibaguzi)

Watanzania kwa ujumla wetu sasa,Asasi za kiraia na jumuiya ya Kimataifa ni lazima tuungane dhidi ya Ukandamizaji huu wa Demokrasia na Udikteta unaochipua kwa nguvu nchini.Tusiogope

Naona hata kwenye mitandao humu nguvu kubwa inatumika kufungia watu wanaotoa maoni ya kuikosoa Serikali na wengine kukamatwa kwa kutumia sheria mbovu na kandamizi ya kwenye mitandao.Kama wanadhani tutaogopa wanakosea sana sana. Hatutaacha kuikosoa Serikali.Kama hawataki kukosolewa basi wasikibali kushangiliwa.Mbali na Mwenyezi Mungu na Malaika wake kwa sisi wanadamu na hasa watawala Ni dikteta pekee anayedhani yeye ni mkamilifu

Ni lazima tuwe tayari kutumia mbinu zote za kisiasa,Kiharakati na Kisheria kukabiliana na Udikteta huu

Hatupo Korea ya Kaskazini kwa Kim Jong-Un wala enzi za Utawala wa Idd Amin kule Uganda

Tupo katika mfumo wa vyama Vingi.Polisi kama wanataka kujiingiza kwenye siasa wavue Magwanda waje majukwaani badala ya kuvamia mikutano ya vyama vya siasa kwa mabomu ,Risasi na Maji ya Kuwashawasha

Wanaweza wakatuua lakini Risasi zao hazitatosha


Aluta Continua,Victory Ascerta....

Ben Saanane
 
Sasa hivi vijana wa Lumumba hawamsifii tena Magufuli, wanachofanya sasa ni kukanusha shutuma dhidi yake, mfano madai kwamba yeye ni dikteta na shutuma nyinginezo. Ile kauli mbiu ya "Hapa Kazi Tu" ishatoweka kwenye masikio ya watanzania. Hizo ndo siasa za Bongo bhana. Sasa subiri uone mashambulizi yanayotokana na kuzuiwa kwa mikutano ya hadhara. Hii serikali haitafanya chochote cha maana.
 
Ni lazima sasa kila mmoja wetu atumie kila njia inayofaa kupingana waziwazi na Udikteta huu.

Ben Saanane
Hivi mnapocomment vitu kama hivi halafu mnageuza mambo huwa mnaona kila mtu ni mjinga? Hebu waambie wabunge wako kwamba sheria na kanuni za bunge hazikuwekwa kama mapambo. Kama wanaona zinawabana basi ni wao ndio wenye fursa ya kuzibadili na siyo kulalamika wakati walizitunga wenyewe. Acheni mambo ya kujifanya mnajua sana hata kwenye vitu ambavyo viko wazi. Mmevunja sheria na kanuni za bunge mlitaka mchekewe tu? Nyie ni kina nani hadi mfike mahali mchekewe tu pale mnapovunja kanuni? Halafu eti mnajifanya kwenda kuandamana sijui na mikutano ili kiwe nini? Kama siyo kushawishi wananchi kutotii sheria basi ni nini hicho? Taratibu za bunge zipo wazi, kwamba ukiadhibiwa na hujaridhika ufuate utaritibu gani sasa huko kuandamana na mikutano ndio taratibu za bunge hizo?
 
Hivi mnapocomment vitu kama hivi halafu mnageuza mambo huwa mnaona kila mtu ni mjinga? Hebu waambie wabunge wako kwamba sheria na kanuni za bunge hazikuwekwa kama mapambo. Kama wanaona zinawabana basi ni wao ndio wenye fursa ya kuzibadili na siyo kulalamika wakati walizitunga wenyewe. Acheni mambo ya kujifanya mnajua sana hata kwenye vitu ambavyo viko wazi. Mmevunja sheria na kanuni za bunge mlitaka mchekewe tu? Nyie ni kina nani hadi mfike mahali mchekewe tu pale mnapovunja kanuni? Halafu eti mnajifanya kwenda kuandamana sijui na mikutano ili kiwe nini? Kama siyo kushawishi wananchi kutotii sheria basi ni nini hicho? Taratibu za bunge zipo wazi, kwamba ukiadhibiwa na hujaridhika ufuate utaritibu gani sasa huko kuandamana na mikutano ndio taratibu za bunge hizo?
Kanuni hizi ambazo wabunge wa CCM wametunga....acha unazi.
 
Back
Top Bottom