TAMISEMI ninyi ndio chanzo cha rushwa na utapeli ajira za walimu

msovero

JF-Expert Member
Jun 30, 2019
839
1,472
Prof. Shemdoe ambaye ni katibu mkuu ofisi ya Rais-TAMISEMI amesema tokea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alipoielekeza Ofisi hiyo kufanya mchakato wa kuajiri walimu 6,000 ili kufidia baadhi ya watumishi hao kwa sababu mbali mbali, kumezuka wimbi la matapeli na wengine kuwadanganya watu wanaoomba ajira kwamba watawasaidia kupata ajira hizo.

“Nimepata taarifa kutoka kwa wasamaria wema kuwa, wapo baadhi ya watu kwa nia ovu wamekuwa wakiwatapeli kwa kuwaomba fedha baadhi ya walimu wanaotaka kuomba ajira na kuwataka watoe pesa ili zifikishwe Wizarani kwa ajili ya kuwapatia ajira, nipende kusema wazi kwamba jambo hili halipo,” amesema Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe na kuongeza kwamba, vishoka wote watakaobainika kutekeleza utapeli huo watachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kufikishwa kwenye vyombo vya dola, huku akiwataka wale wote watakaokumbana na adha hiyo kutosita kutoa taarifa ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa.

Pamoja na kauli za vitisho alizotoa Prof. Shemdoe, ukweli ni kwamba ofisi anayoiongoza ndio chanzo cha utapeli huo kwa sababu tangu Rais atoe tamko la kuajiri walimu 6000 kwa haraka ili kuziba nafasi za walimu waliostaafu, kufariki au kuacha kazi, wizara iko kimya haijatolea ufafanuzi wowote kuhusiana na ajira hizo.

Mtakumbuka mwezi September aliyekuwa Rais kwa wakati huo, hayati JPM alipotangaza kibali cha kuajiri walimu elfu 13 jioni yake aliyekuwa waziri wa TAMISEMI kwa wakati huo Bw. Suleiman jaffo alijitokeza na kutangazia umma siku dirisha la maombi litakapofunguliwa ili walimu waweze kutuma maombi yao na kweli ikawa hivyo.

Lakini cha kushangaza tangu mhe. Samia Suluhu atoe tamko la kuajiri walimu 6000 siku ya tarehe 6/4/2021 hadi sasa hakuna utaratibu wowote umetolewa kuhusiana na ajira hizo, si katibu mkuu au waziri Ummy Mwalimu wote wako kimya.

Kitendo cha waziri na katibu wake kuwa kimya ndio kimepelekea kuibuka kwa utapeli kwa sababu mpaka sasa waombaji hawajui utaratibu utakaotumika kama wataajiriwa kwa kutumia majina yalipo kwenye database au dirisha la maombi litafunguliwa upya.

Sasa basi ili kukomesha tabia hii ya kitapeli ni muda muafaka waziri Ummy Mwalimu na katibu wake prof. Shemdoe wajitokeze hadharani kutoa utaratibu utakaotumika kwenye hizi ajira. Kama dirisha linafunguliwa upya waeleze wazi ni lini litafunguliwa ili kuwaondoa hofu waombaji na kuwaepusha kurubuniwa na matapeli.

Nawasilisha kwenu ma-GT
 
Kwa hapa tulipofikia suala la rushwa na utapeli kwenye ajira halikwepeki! Maana waombaji ni wengi lakini nafasi ni chache! Hata hivyo wizara itolee mwelekeo wa hizi ajira ili watu tujue moja!!
 
Kwa hapa tulipofikia suala la rushwa na utapeli kwenye ajira halikwepeki! Maana waombaji ni wengi lakini nafasi ni chache! Hata hivyo wizara itolee mwelekeo wa hizi ajira ili watu tujue moja!!
Huo ndio ukweli wenyewe na suluhisho pekee naloliona ni kurudisha utaratibu aliotumia kikwete wa kujairi wahitimu wote kwa mkupuo
 
Majina ya walimu wanaojitolea yametumwa kwa maana wao ndio watapewa kipaumbele katika ajira hizo,sema wangetangaza utaratibu tukajua moja...walimu wanaojitolea tz nzima hawawez fika 6000
 
Utendaji kazi wa sasa ni wa slow slow sana compared na kipindi kile Hayati JPM alipotoa maagizo ya ajira tarehe 04/09/2020 na iliwachukua siku 3 tu na wakaruhusu watu waapply lkn Mh.Rais SSM aliwaagiza tarehe 06/04 wafanye haraka ajira za replacement lakini mpaka leo hawaeleweki kama watachukua majina ya kwenye database au wataruhusu application upya.Wao kila siku kwenye vyombo vya habari.
 
Majina ya walimu wanaojitolea yametumwa kwa maana wao ndio watapewa kipaumbele katika ajira hizo,sema wangetangaza utaratibu tukajua moja...walimu wanaojitolea tz nzima hawawez fika 6000
Hayo majina yamejaa udanganyifu mkubwa. Watu wanajiandika majina mitandaoni na kuyatuma wenyewe tamisemi.
Thread 'Anton mtweve ni nani huko TAMISEMI?' Anton mtweve ni nani huko TAMISEMI?
 
Prof. Shemdoe ambaye ni katibu mkuu ofisi ya Rais-TAMISEMI amesema tokea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alipoielekeza Ofisi hiyo kufanya mchakato wa kuajiri walimu 6,000 ili kufidia baadhi ya watumishi hao kwa sababu mbali mbali, kumezuka wimbi la matapeli na wengine kuwadanganya watu wanaoomba ajira kwamba watawasaidia kupata ajira hizo.

“Nimepata taarifa kutoka kwa wasamaria wema kuwa, wapo baadhi ya watu kwa nia ovu wamekuwa wakiwatapeli kwa kuwaomba fedha baadhi ya walimu wanaotaka kuomba ajira na kuwataka watoe pesa ili zifikishwe Wizarani kwa ajili ya kuwapatia ajira, nipende kusema wazi kwamba jambo hili halipo,” amesema Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe na kuongeza kwamba, vishoka wote watakaobainika kutekeleza utapeli huo watachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kufikishwa kwenye vyombo vya dola, huku akiwataka wale wote watakaokumbana na adha hiyo kutosita kutoa taarifa ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa.

Pamoja na kauli za vitisho alizotoa Prof. Shemdoe, ukweli ni kwamba ofisi anayoiongoza ndio chanzo cha utapeli huo kwa sababu tangu Rais atoe tamko la kuajiri walimu 6000 kwa haraka ili kuziba nafasi za walimu waliostaafu, kufariki au kuacha kazi, wizara iko kimya haijatolea ufafanuzi wowote kuhusiana na ajira hizo.

Mtakumbuka mwezi September aliyekuwa Rais kwa wakati huo, hayati JPM alipotangaza kibali cha kuajiri walimu elfu 13 jioni yake aliyekuwa waziri wa TAMISEMI kwa wakati huo Bw. Suleiman jaffo alijitokeza na kutangazia umma siku dirisha la maombi litakapofunguliwa ili walimu waweze kutuma maombi yao na kweli ikawa hivyo.

Lakini cha kushangaza tangu mhe. Samia Suluhu atoe tamko la kuajiri walimu 6000 siku ya tarehe 6/4/2021 hadi sasa hakuna utaratibu wowote umetolewa kuhusiana na ajira hizo, si katibu mkuu au waziri Ummy Mwalimu wote wako kimya.

Kitendo cha waziri na katibu wake kuwa kimya ndio kimepelekea kuibuka kwa utapeli kwa sababu mpaka sasa waombaji hawajui utaratibu utakaotumika kama wataajiriwa kwa kutumia majina yalipo kwenye database au dirisha la maombi litafunguliwa upya.

Sasa basi ili kukomesha tabia hii ya kitapeli ni muda muafaka waziri Ummy Mwalimu na katibu wake prof. Shemdoe wajitokeze hadharani kutoa utaratibu utakaotumika kwenye hizi ajira. Kama dirisha linafunguliwa upya waeleze wazi ni lini litafunguliwa ili kuwaondoa hofu waombaji na kuwaepusha kurubuniwa na matapeli.

Nawasilisha kwenu ma-GT
Hizo ajira zina urasimu wa kufa mtu yaani wa kutoshea si ajabu washajiandaa na pdf lao kabisa halafu wanasubiri kuwasumbua vijana kuwa tumeni maombi pumbavu kabisa
 
Utendaji kazi wa sasa ni wa slow slow sana compared na kipindi kile Hayati JPM alipotoa maagizo ya ajira tarehe 04/09/2020 na iliwachukua siku 3 tu na wakaruhusu watu waapply lkn Mh.Rais SSM aliwaagiza tarehe 06/04 wafanye haraka ajira za replacement lakini mpaka leo hawaeleweki kama watachukua majina ya kwenye database au wataruhusu application upya.Wao kila siku kwenye vyombo vya habari.
Nafikiri kuna big deal wanaplan kuifanya through hizi ajira maana samia alisema ajira hizi ni replacement zitangazwe haraka lakini bwana Silinde akajibu kuwa ni mpaka mwezi wa sita. Nadhani kuna ishu ipo chini ila wao ndo wanajua
 
Hizo ajira zina urasimu wa kufa mtu yaani wa kutoshea si ajabu washajiandaa na pdf lao kabisa halafu wanasubiri kuwasumbua vijana kuwa tumeni maombi pumbavu kabisa
Mkuu bora dirisha lifunguliwe upya watu waomba ili mfumo wenyewe ndio uchague wenye sifa na kuwapangia vituo lakini ukisema watumie database ya maombi ya mwaka jana pdf itajaa majina ya wanafunzi wa chuo cha eckerford maana hata ajira zilizopita walijaa wao
 
Tusubirini tuone itakuwaje maana walisema mwezi wa sita ndo wanaajiri kama hatutokuemo tutasubir tubanane kwenye zile elf 10+ za mwka wa fedha 2021/2022
Kama mpaka sasa hawajaruhusu watu kutuma maombi usishangae nazo zikasogezwa mbele ionekane ni utekelezaji wa bajeti ya 2021/2022
 
Eti wanaojitolea ndio kipaumbele! Huu ni utapeli wa kiwango cha sgr. wakuu wa shule & wakurugenzi wanafoji majina ya watu wao ili wapate ajira...kuna mtu alikuwa anajitolea shule Fulani kabla hata hajaenda chuo kusomea ualimu eti nae kachomekwa. Tamisemi wanatengeneza mazingira ya rushwa sio siri
 
Hii ndiyo tunaiita Suvival of the fittest according to Charles Darwin!

Only the fittest will survive! while the weakest, will be perished!! Pambaneni vijana. Hakuna namna.
 
Back
Top Bottom