Tambuwa kuwa na kifriji tumbo kubwa

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,318
33,125


!
Karibu watu 9 kati ya 10 hawaelewi hatari inayowakabili kwa kuwa wanene hasa sehemu za tumboni na katika nyonga.


Uchunguzi uliofanywa kwa kuwashirikishwa watu 12,000 wa nchi za Ulaya, umeonyesha kwamba, wengi wao hawajui kwamba kuwa na wanene sehemu za tumbo na nyonga ni dalili ya kuwa na ongezeko la mafuta kwenye viungo mbalimbali tumboni.

Mafuta hayo yanayojulikana kitaalamu kama ‘visceral fat’ yanauhusiana moja kwa moja na ugonjwa wa kisukari aina ya pili na magonjwa ya moyo.

Wataalamu wanasema kuwa, watu hawajui kwamba mafuta yanayokusanyika ndani ya mwili na kuzunguka viungo mbalimbali mwilini, ambayo hatuyaoni kwa macho au kuyahisi, ni yenye hatari kubwa.

Hatari ya mafuta hayo inaweza kuwa ni kutoa protini na homoni ambazo zinaweza kuharibu mishipa ya damu, kuingia katika ini na kuathiri jinsi mwili unavyovunja vunja sukari na mafuta.

Watu wengi waliokuwa wanene wanajihisi tu kuwa tatizo lao ni jinsi wanavyoonekana au namna wanavyopendeza na wala sio tatizo la kiafya.

Uchunguzi umeonyesha kuwa, mzunguko wa kiuno au nyonga, ni ishara nzuri ya kukutambulisha kiwango cha mafuta ya visceral uliyonayo, na jinsi mzunguko huo unavyokuwa mkubwa ndivyo mafuta hayo yanavyoongezeka.

Suala hilo huonyesha kwa kiasi gani mtu anaweza kupatwa na ugonjwa wa kisukari kinachotokana na unene.

Wakati mtu anapopunguza uzito mafuta hayo yanayozunguka kiuno na tumbo ni huyeyeyuka kwa rahisi, kuliko mafuta ambayo yako chini ya ngozi, na hata kupunguza uzito kwa kiasi kidogo kunapunguza mafuta hayo.

Ni muhimu kujua kwamba, mafuta yanayozunguka tumbo yana hatari kubwa kw afya, na watu wanatakiwa wajitahidi kuwa na uzito unaotakiwa ili kutunza afya zao.
 
Solution ya hili tatizo ni nini? yani mtu afanye nini ili iyo fat ipungue au kwisha kabisa?
Copy: MziziMkavu
Kunywa Maji ya Uvuguvugu Asubuhi kunywa glasi 2 kabla ya kupiga

mswaki na baada ya kupiga mswaki kunywa maji ya uvuguvugu glasi 1tia ndani yake kamuwa limau moja na Asali kijiko 1 ,kisha kaa baada ya saa 1

kula au kunywa chai chakula cha asubuhi. Na Mchana knywa glasi 2 za maji ya uvuguvugu kisha

kaa baada ya saa moja kupita ndio waweza kula. Na wakati wa usiku kunywa tena Maji ya

uvuguvugu glasi 2 kisha kaa baada ya saa moja kula chakula na wakati wa kulala kunywa tena

maji ya uvuguvugu glasi 1 kisha lala .Fanya hivyo kila siku utapunguwa hilo tumbo na mafuta

ukitaka Dawa ya haraka kupunguza mafuta unene,tumbo na kilo mwilini hebu tembelea bonyeza

hapa https://www.jamiiforums.com/jf-doct...zito-wa-mwili-na-unene-na-mafuta-mwilini.html
 
Shukrani kwa darasa.

Kunywa Maji ya Uvuguvugu Asubuhi kunywa glasi 2 kabla ya kupiga

mswaki na baada ya kupiga mswaki kunywa maji ya uvuguvugu glasi 1tia ndani yake kamuwa limau moja na Asali kijiko 1 ,kisha kaa baada ya saa 1

kula au kunywa chai chakula cha asubuhi. Na Mchana knywa glasi 2 za maji ya uvuguvugu kisha

kaa baada ya saa moja kupita ndio waweza kula. Na wakati wa usiku kunywa tena Maji ya

uvuguvugu glasi 2 kisha kaa baada ya saa moja kula chakula na wakati wa kulala kunywa tena

maji ya uvuguvugu glasi 1 kisha lala .Fanya hivyo kila siku utapunguwa hilo tumbo na mafuta

ukitaka Dawa ya haraka kupunguza mafuta unene,tumbo na kilo mwilini hebu tembelea bonyeza

hapa https://www.jamiiforums.com/jf-doct...zito-wa-mwili-na-unene-na-mafuta-mwilini.html
 
Back
Top Bottom