Tairi confortable zaidi


Kuna mdau keshakujibu hapa.

https://www.jamiiforums.com/showthread.php?p=14200139

Kama unataka tairi pana kwa ajili ya show nzuri na stability barabarani recomended size ni 225/60/R16
Au 225/55/R16 ila hii inashusha gari kidogo kama unatumia rough road itakupa shida kidogo.

Pia size 235/50/R17 ni tairi pana kidogo recomended na Subaru wenyewe.

Zingatia ukitumia tairi ya size 225 au 235 lazima rim yako iwe size 7.5J.

Kwa kuwa Forester ni gari yenye nguvu (torque) unatakiwa kununua brand nzuri kwa dealer kama vile Kumho, Good year, Michelin, Pirreli. Etc.
Achana na mchina wa bei nafuu utakula hasara ndani ya miezi 6.
 
kuna kitu kinaitwa rule of thumb katika tires kuwa jinsi unavyoongeza 0.5'' inch inabidi pia uongeze 0.2'' ya tires yako
so 0.5 ya rim 0.4 ya tire otherwise kuna vitu ambavyo gari yako itakuwa tofauti mfano speed,confortability,na braking
 

Asante mkuu. Ila nisaidie kidogo rim size 7.5j naijuaje mkuu
 
Asante mkuu. Ila nisaidie kidogo rim size 7.5j naijuaje mkuu

Zinakuwa zimeandikwa kwenye mzunguko wake.
Maana rim zote zinazobeba tairi pana ni alloy au sport. Ukikosea upana wa rim tairi inaharibika.

Ukipata utata wa kuzisoma waulize tu jamaa wauza pancha watakusome size fasta.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…