Tahadhari: Wanawake kuweni makini.

Royal Warrior

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2015
Posts
1,166
Reaction score
2,144
hello ladies.... gentlemen naomba mpite pembeni mada haiwahusu.

Kumekua na tabia ambayo inashamiri kwa kasi sana siku hizi.
Tabia hiyo si nyingine bali ni wanawake kujipiga picha za uchi au kujirekodi video za uchi na kisha kuzituma kwa ma "boyfriend" wao kupitia mitandao kama whatsapp n.k

Wengi wao hawajui athari zake na ndio maana nimeona leo nitoe elimu ya bure kuhusu hili suala.
wengi wao waliofanya hili jambo, wamejikuta wanajutia big time.

Miongoni mwa athari zake ni hizi hapa

1} Kwanza ni dhambi, dini zote zinakataza juu ya hili.

2} Utakosa uhuru baadae, boyfriend wako atatumia hizo picha kama leverage ya kuku control.

3} kuna uwezekano mkubwa sana wa hizo picha kuvuja, vuta picha tu sura yako utaiweka wapi.

4} Unakua unatumika tu. I hate to dissapoint you, lakini tilia mashaka sana upendo wake kwako. wanawake wengi wanao ombwa picha za uchi wanakuwa used tu kama "sex tool".(na ujue haupo peke ako unaemtumia picha hizo.)

5} kuna siku utajuta tu.(incase you have a future). majuto ni mjukuu. kipindi unaitwa "mama" then mitandaoni zipo picha zako za utupu.

hasara zipo nyingi sana,.. hizi ni chache tu.

Mwenye kuelimika na aelimike.
 
Mwenye macho haambiwi tazama...mwenye masikio haambiwi sikiliza haya tuyaweke kama msimamo utu (dignity) comes first
 
Duuuuu mi mbn nimewahi kutuma tena juzi tuuu
 
Aahh mm hata selfie shida kwangu......siwezi mm hivo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…