Hii post imenifurahisha sana.Hawa jamaa tabiri zao siziamini kabisa
Sawa mkuu,nashukuru kwa maelezo yako ya kina na yenye ukweli ndani yake,watu wa maeneo ya Pwani ndiyo inawapa uwepesi wa kushuhudiwa na yaliyotabiriwa na Mamlaka ya husika,yule Mama kama sikosei anaitwa Kijazi mkuu.Hii post imenifurahisha sana.
Maana viewers ni 300 ila comment ametoa mtu mmoja na ya pili yangu
Hii ni kuonyesha kwamba Takiwmu iliyotolewa ya watu kutumia muda mwingi kuongelea mambo yasiyo ya msingi hasa wale wa Dar ipo sahihi,hapa ingeandikwa habari zetu zile basi pangejaa,ila habari muhim za maisha ya watu kimyaa,ila likitokea tukio basi uzi unajaa.
Mkuu kwanza hongera kwa kujazia na mleta mada.
Kwa sie watu wa Pwani tunawashukuru saana TMA kwa taarifa zao ambapo mara nyingi tumekuwa tunashuhudia matokea sahihi ya wanachosema.
Unajua ili kujua usahihi wa hili lazima uwe unaishi ukanda husika,kwa visiwani ni rahisi kuona hali hiyo na kugundua tukio la taarifa.Ila Dar baadhi ya maeneo ni ngum kuliona hilo,ikiwemo mfumo wa ujenzi na mji,maana hata upepo ukivuma mtu anaona unapita juu tu,maana hapa nyumba pale choo.
Ila watu wa Oysterbay,Masaki,Kunduchi,Bagamoyo,Mikocheni,Msasani wao wanashabihiana sana na Sie.
Una ujue kwamba katika maeneo yaliyotajwa kama haikutokea kwako basi itatokea kwa mwenzao na ndio maana ya Utabiri wa hali ya hewa,na Yule Mkurugenzi wao yule mama jina nimelisahau,aliwahi kusema kwamba Hali ya hewa hubadilika,sasa tukiolinaweza kuwa kubwa zaidi au likapotea kilingana na ongezeko au mwelekeo wa Mgandamizo wa nini sijui(masanja),(Hapo mambo ya kitaalam jameni)
Nawaombeni Saana wananchi muendelee kuwaamini TMA na muendele kuchukua tahadhari pale mnapopata taarifa na sio kuhadaiwa na maneno ya watu halafu likitokea tunatoa lawama kwa serikali
Tutumieni simu zetu ku google na kupata updates za TMA na ndio faida ya kuwa na simu katika karn hii
Asante mkuuSawa mkuu,nashukuru kwa maelezo yako ya kina na yenye ukweli ndani yake,watu wa maeneo ya Pwani ndiyo inawapa uwepesi wa kushuhudiwa na yaliyotabiriwa na Mamlaka ya husika,yule Mama kama sikosei anaitwa Kijazi mkuu.
Ni Mama mwenye muonekano wa kiheshima,hasa napenda anavyotengeneza nywele zake,wala hasuki wala haweki dawa au mambo mengine ya kipuuzi.Asante mkuu
Sawa sawa anaitwa Kijazi aisee,mie nakumbuka Sura na Mkato wake wa Nywele,mpolee
Namkubali sana