Serikali inavyo vyombo vya kutosha kuweza kupata taarifa za vihatarishi vya amani na usalama wa nchi. Kwa kutumia taarifa hizo ndipo jukumu la kujilinda au kuzuia usalama wa nchi usipotee hutekelezwa.
Kwa ugumu wa viongozi ambao hutakiwa kuchukua hatua wanaacha kufanya majukumu yao ya kuchukua hatua na hatimaye nchi nyingi inaingia katika matatizo yasiyo ya lazima kutokea. Wananchi wanapotoa madai yao ya msingi dhidi ya serikali hayazingatiwi wala hayatiliwi maanani. Wananchi wanapochoka kurudia madai hayo watayadai kwa nguvu za ziada na hatimaye kuiondoa serikali madarakani.
Tumeona wenzetu katika nchi za Kiafrika kama Tunisia, Misri na Libya na nchi zingine za Kiarabu yaliyowapata. Kwanini inatokea hatua ya wananchi kuingia barabarani na kumwondoa kiongozi wao? Kupata sababu hatuhitaji kwenda kufanya utafiti bali zinafahamika kwa viongozi lakini kumbe wanazembea kuchukua hatua.
Ni wazi kuwa Tanzania tumeanza safari ya kuelekea huku walikofika wenzetu hao wa Tunisia, Misri na Libya. Wananchi wa Tanzania wasidhaniwe kuwa ni watu wa amani kwa maana ya viongozi wetu wanavyotaka tuamini. Kamwe Watanzani wasidhaniwe kuwa wataacha kuiondoa serikali madarakani kwa kigezo cha kuwa nchi hii ni kisima cha amani. Tukiwadhania Watanzania kuwa wako hivyo basi tutakuwa tunapotosha ukweli na kujidanganya wenyewe.
Dalili zilizoanza kujitokeza zisipuuzwe kamwe na wala Watanzani wasidhaniwe kuwa hawana uwezo wa kuichukulia hatua serikali kama walivyofanya wananchi katika nchi zingine. Mdharau mwiba mguu huota tende.
Kwa ugumu wa viongozi ambao hutakiwa kuchukua hatua wanaacha kufanya majukumu yao ya kuchukua hatua na hatimaye nchi nyingi inaingia katika matatizo yasiyo ya lazima kutokea. Wananchi wanapotoa madai yao ya msingi dhidi ya serikali hayazingatiwi wala hayatiliwi maanani. Wananchi wanapochoka kurudia madai hayo watayadai kwa nguvu za ziada na hatimaye kuiondoa serikali madarakani.
Tumeona wenzetu katika nchi za Kiafrika kama Tunisia, Misri na Libya na nchi zingine za Kiarabu yaliyowapata. Kwanini inatokea hatua ya wananchi kuingia barabarani na kumwondoa kiongozi wao? Kupata sababu hatuhitaji kwenda kufanya utafiti bali zinafahamika kwa viongozi lakini kumbe wanazembea kuchukua hatua.
Ni wazi kuwa Tanzania tumeanza safari ya kuelekea huku walikofika wenzetu hao wa Tunisia, Misri na Libya. Wananchi wa Tanzania wasidhaniwe kuwa ni watu wa amani kwa maana ya viongozi wetu wanavyotaka tuamini. Kamwe Watanzani wasidhaniwe kuwa wataacha kuiondoa serikali madarakani kwa kigezo cha kuwa nchi hii ni kisima cha amani. Tukiwadhania Watanzania kuwa wako hivyo basi tutakuwa tunapotosha ukweli na kujidanganya wenyewe.
Dalili zilizoanza kujitokeza zisipuuzwe kamwe na wala Watanzani wasidhaniwe kuwa hawana uwezo wa kuichukulia hatua serikali kama walivyofanya wananchi katika nchi zingine. Mdharau mwiba mguu huota tende.