Tahadhari: Barabarani toka Moro - Chalinze

Tahadhari: Barabarani toka Moro - Chalinze

kzba

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2014
Posts
1,355
Reaction score
790
Kwa wale wenzangu na mimi tuliojaliwa kupata kausafiri ka miguu minne(magari) tafadhali ukiwa unatoka Morogoro kuelekea Chalinze kama unaenda Dar na kwingineko ukikuta basi limekutangulia mbele yako maeneo ambayo wewe unaamini ni ya salama ukalipita inakula kwako.

Hawa ndugu zetu trafiki kuna kamera wamefunga kila mahali za spidi ambapo ni wewe huwezi dhania na kudharau kwa kuona kibao cha 50 au no overtaking ww ukajiona mjanja na mambio yako usizingatie alama za sehemu husika kwa taarifa yako utapigwa faini mpaka ukome.

Jamaa hawataki rushwa hata uwaombe vipi, maana wanaogopa zile kamera mwisho wa siku mkuu wao anazitrack kujua ni magari mangapi yamevunja utaratibu na hatua gani wamechukua dhidi yao.

Mimi ni mhanga wa hilo jana nilikuwa natoka Dom to Dar yakanikuta hayo na wamechukua faini yangu kiulaini maana nimekuta hadi ambulance liko wanalipiga fain dadadeki.

Nilichogundua watu wa mabasi wanajua hasa ya Abood kuwa sehemu gani ni vimeo.
 
MKUU hao wenye mabasi wanajua sehemu mbaya kwao. ukiona jamaa anapunguza mwendo ujue mbele kuna kitu. pia vile vile kufuata sheria pindi uwapo barabarani ni wajibu, kwa hili huwa tunajisahau sana.
 
...asante kwa Taarifa!
Tunaomba serikali nayo iboreshe barabara kuu, na Tanroad waweke alama zakutosha, naziwe wazi.
 
Daah mkuu nilifikiri mm peke yangu kumbe tuko wengi mkuu...mm pale nimelipishwa fain mara mbili mkuu...kosa la kwanza kuwa over speed ...kosa pili kuover take gari tatu..katika kona..nikawaambia wenzenu washanipiga fain..wakakomaa hivyo hivyo....
 
Hii Ni Nchi Nzima Kwa Sasa, Hata Kosa Ufanye Ukiwa Mpanda Ujue Utakamtwa Popote Kwakuwa Ushahidi Upo, Nguvu Pia Inaelekezwa Dsm Kwa Hawa Wenzetu Wenye Tabia Ya Kutanua. Cha Msingi Watu Tufuate Sheria Za Usalama Barabarani. Kuna Dereva Wa Bus Ya Moro -Dsm Jana Amelipa Fine ya Makosa Saba.
 
Safi sana........wewe kwenye alama ya kukimbia 50 kwa nini ukimbie 100......?......mstari wa kuzuia overtake.........wewe unaovertake kwa nini.....?.......
Polisi kwa mtindo huu wanaweza kufa njaa maskini lakini wacha tunyooshane kwanza.........
Nimeipenda hii.............
 
hela za kampeni zinakusanywa ndio maana rushwa wanakataa wanarekodiwa hii itaisha baada ya uchaguzi
 
Bora wewe umetii wito wa kamanda kuondoka Dom fasta ..wapigwe tu.
 
Tena wapige fain na kupunguza points(kama zipo) kwenye leseni ili heshima ya sheria iwepo.

Safi sana traffick piga fain hao
 
Safi sana........wewe kwenye alama ya kukimbia 50 kwa nini ukimbie 100......?......mstari wa kuzuia overtake.........wewe unaovertake kwa nini.....?.......
Polisi kwa mtindo huu wanaweza kufa njaa maskini lakini wacha tunyooshane kwanza.........
Nimeipenda hii.............

Safi sanaaaaaa
 
Tena wapige fain na kupunguza points(kama zipo) kwenye leseni ili heshima ya sheria iwepo.

Ha ha........mkuu hii kuja bongo itakaa sana.........na rushwa ndio itakuwa imehalalishwa rasmi..........
 
Tatizo ni hawa law enforcers wetu. Wangesimamia sheria, wananchi tungeshika adabu muda mrefu.
Wiki jana nimeshuhudia trafiki akiipokea rushwa ya sh. 1000 (elfu moja)! Ni aibu kwa jeshi la polisi!
 
Sasa wewe kwa nini unataka kuvunja sheria za barabarani? Hivi hizi ajali hamzioni? Au mnadhani zipo kwa ajili ya watu wengine tu ninyi haziwezi kuwagusa?! Ingekuwa busara uwapongeze na ufuate sheria na ujue sio polisi tu wenye hizo kamera kuna kikosi kazi cha raia waliochoswa na ajali zisizoisha wapo kazini kuhakikisha sheria za barabarani zinafuatwa ipasavyo.

Kumbuka kufuata sheria za barabarani ni faida kwako na watumiaji wengine wa barabarani. Mambo mengine kama haya hatukupaswa hata kusubiri kupigwa faini na polisi bali tungepaswa kuhamasishana umuhimu wake katika jamii.
 
Juzi tu trafic kala buku 5 na afari ikaendelea, walikuotea ty mkuu.
 
Tungewapa traffic likizo ya walau miezi mitatu halafu JWTZ wangeshika hii kazi kwa muda huo ili kujenga nidhamu na uzalendo kwa madereva. Maana Bongo hatufuati sheria bila shuruti.
 
Back
Top Bottom