Tafuta Msaada Wa Mungu Na Sio Wa Mwanadamu

Tafuta Msaada Wa Mungu Na Sio Wa Mwanadamu

Samson Ernest

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2014
Posts
1,119
Reaction score
1,570
Isa 31:3 SUV
[3] Basi Wamisri ni wanadamu wala si Mungu, na farasi zao ni nyama wala si roho; na BWANA atakaponyosha mkono wake, yeye asaidiaye atajikwaa, na yeye asaidiwaye ataanguka, nao wote pamoja watakoma.

Utajiuliza tuache kuwaomba watu msaada, hapana, tuache kufikiri fulani anaweza kutusaidia, simaanishi hivyo, kinacholeta shida na chukizo mbele za Mungu ni kutafuta msaada wa watu na kuwaona ndio kila kitu, na kuacha kumtegemea Mungu.

Onyo hili kali linalotolewa hapa na nabii Isaya kwa watu wa Yuda, lilikuwa hivi, watu hawa walikuwa wanatafuta msaada wa kijeshi kutoka Misri badala ya kumtegemea Mungu wao.

Kwanini Mungu alichukizwa na hili, Misri lilikuwa taifa lenye nguvu kubwa, ila nguvu zake hazikuwa na chanzo cha kiroho au ki-Mungu. Watu wanaweza wakawa na nguvu kubwa ila wana mipaka yao, kitu ambacho kwa Mungu hakipo.

Kuonekana kwa farasi wa kimisri wenye kasi na wenye nguvu, bado walikuwa ni viumbe wa kimwili tu, hii inatusaidia kuelewa kuwa nguvu za kimwili haziwezi kushindana na nguvu za kiroho.

Mungu akiamua kushughulika na mambo yenu, hata kama mlikuwa mnategemea msaada mkubwa wa watu wengine wenye nguvu za kimwili, anaweza kusambaratisha mpango huo.

Usitegemee msaada wa kibinadamu, bali mtegemee Mungu, tumaini lako lote liwe kwake, hii itakusaidia sana kushinda vita nyingi vinavyoinuka kwako.

Usije ukasahau hili, elewa nguvu za kimwili hazina maana mbele ya nguvu za kiroho, ukijaa nguvu za kiroho unaweza kutembea umbali mrefu na kushinda mengi kuliko nguvu za kimwili.

Kama ulikuwa unafikiri kutegemea nguvu za kimwili zinaweza kukusaidia katika maisha yako, rudi haraka kwa Mungu utubu, na uanze kumtegemea Mungu.

Soma neno ukue kiroho
Liwe jua iwe mvua soma biblia na kutafakari
Mungu akubariki sana
Samson Ernest
 
Back
Top Bottom