Tafsiri ya Niliyoyasikia njiani nilimopita kumhusu Magufuli

Kuna watu wanataka mabadiliko lakini pia wana watu WAO mahsusi wanataka wayalete hayo mabadiliko, tofauti na hapo watayapinga hayo mabadiliko. Natumai mkuu Nguruvi sio kati ya watu hao.

Ni mapema sana kumuita Magufuli mkombozi au kumpa sifa za kiongozi ambaye ameshafanikiwa. Ila ndani ya muda mfupi kwa mtu mwenye tamaa ya mabadiliko atampa kitu kinaitwa "benefit of doubt". Ni kweli unachosema kuhusu mfumo, lakini pia ni kweli huo mfumo unaesema hauwezi kuja ndani ya mwezi mmoja wa kuwa madarakani. Hata baraza lake ya mawaziri hajatangaza unategemea tayari mfumo utakuwa umebadilika? Tena una mtabiria na KUFELI juu?! Labda anaweza kuja badilika na asimalize kama alivyo anza, lakini kama unataka kuzungumza haki, kwa kipindi hiki kifupi ameonesha yeye anataka kuwa raisi wa aina gani. Na kwa hilo mimi binafsi nampa benefit of doubt.

Labda kwa maono yako, ili abadili huo mfumo unausema ndani ya kipindi hiki kifupi alikuwa anatakiwa amesha tekeleza jambo gani yeye kama raisi? Je alitakiwa asifanye haya aliyoyafanya mpaka sasa mpaka huo mfumo mpya utakapo kuwa tayari? Je hakuna uwezekano wa yeye kufanya aliyoyafanya mpaka sasa na bado akaja WEZESHA kupatikana kwa huo mfumo ndani ya miaka mitano ya uongozi wake?

Si kweli kuwa hatuhitaji kufukuza wakurugenzi na makamishna. Katika huo mfumo unauosema hii inaitwa ACCOUNTABILITY. Hakuna mfumo utakao kuhakikishia hutapata mkuregenzi ambaye pamoja na kuwa CV inayomuonesha kuwa ni competent ikakupa guarantee hatakuja kufanya makanjanja. Kufukuza na baadae kuacha sheria ichukue mkondo wake huko ndio kunaitwa KUMUAJIBISHA mtu. Hilo sio suala la kimfumo peke yake, ni suala UTENDAJI makini. Mfumo unaweza kuwa mzuri tu ila kama kila anaetakiwa kuhakikisha huo mfumo unafanya kazi akikosa umakini na uzalendo katika utendaji wake huo mfumo hauwezi kufanya kazi.

Najua tumeng'atwa na nyoka, unyasi unatutatiza lakini sisi bado ni taifa changa na tuna kila sababu ya kuwa Optimistic. Hebu tusubiri walau serikali yake ipitishe bajeti ya kwanza halafu tuone hakuna dalili ya huo unaitwa mfumo kubadilika then tuje hapa kuongea ila kwa sasa haya maandiko yetu na malalamiko yetu ni PREMATURE na kuwa wengine watakuwa na haki ya kuyaona yako FULL OF PREJUDICE.

#BEINGOPTIMISTIC #CHANGETANZANIA
Ni mmoja wa wale wanaotaka mabadiliko, lakini si mabadiliko tu, bali mabadiliko ya kweli na ya kudumu.

Si mtu wa kuchora mstari kwa kutumia nukta moja. Ninataka kuona ramani nzima na points between ili nichore mstari.

So far hakuna ramani hakuna sketch diagram bali ni political stunt.
Nitasimama kwa hilo hata kama nitapewa label ya uzezeta, zumbukuku n.k. Ninaamini katika muda mfupi na mrefu

Umesema vema kabisa, na mfano wako unaweza kuonekana vema katika uzi wa leo wa The Boss

The Boss ameonyesha jinsi bodi za TRA zilivyo na matatizo katika uteuzi wake
Kilichofanyika kwa bosi wa TRA ni sahihi, lakini hakijawa solution kama tunavyoaminishwa na Magufulimania zealots

Wengi wanashindwa kuelewa kuwa kuwajibika hakuwezi kuwa mabadiliko.

Kama tunampa benefit of doubt ya kuwajibika sina tatizo, lakini hilo haliwezi kuwa mabadiliko.

Lakini pia kuna mwingiliano kati ya kuwajibika na kutengeneza mfumo.
Tumeona DC akasweka watu ndani bila sababu na kukiuka haki za binadamu kwa kutowafikisha mbele ya sheria, kwa kutotumia sheria za kazi n.k. Ni kwasababu hakuna mfumo bali kutegemea nani yupo magogoni

Tumeona anafukuza watu TRA , lakini je, amejiuliza kwanini Bosi wa TRA alikuwa na majina na hakuyafanyika kazi?

Je, DCI, DPP, PCCB walikuwa wapi? Mbona hakuna kuwajibishwa kwa muda mfupi sambamba na TRA?

Hili tu linaonyesha kuwa hakuna ramani ya kutengeneza mabadiliko.
Kilcihopo ni kukurupuka ndiyo maana ninasema kwa mwendo alio nao, kuwajibika pekee kutapeleka KUFELI.

Timu kama ya Brazili inatandaza kandanda safi si kwasababu wachezaji wake ni w wenye maguvu bali wanatumia maarifa kuwashinda wenye maguvu

Anachofanya sasa hivi ni kutuonyesha mapungufu ya mfumo yanayopelekea matatizo yanayoibuliwa.

Tumpe benefit of doubt ya kuweka wazi uozo wa mtangulizi wake, lakini hayo si MABADILIKO kama tunavyoaminishwa.

Ni majukumu yake ya kuwajibika. Mabadiliko tutayaona pale atakapobadili mfumo na kuja na kitu tofauti

Mabadiliko ya kweli ni kufumua mfumo wa kutegemea mtu mmoja, na kumuacha Rais atazame nchi kwa ujumla wake si kukimbizana na vitanda na MRI.

Kama bodi ya Muhimbili imefeli, mkurugenzi amefeli na wote waliteuliwa na Rais aliyeondoka, ni wazi kwa mfumo huo huo naye atafeli. Uteuzi wake na kutoa bilioni 3 hapo hapo unaonyesha tatizo si Mkurugenzi, bali mfumo uliopelekea mkurugenzi kushindwa. Je alifanya utafiti kubaini tatizo lilianzaje na nani anahusika? Ikiwa hazina hawakutoa pesa, huoni kama tatizo ni pana kuliko mkurugenzi

Muhimbili ili feli kwasababu mfumo wa kupata watu makini unategemea mtu

Tunataka mfumo utakaomwezesha yeye kusimama na kuangalia 'muhimbili' zote nchini na si MRI mmoja

Hilo litawezekana ikiwa tu tutakuwa na mifumo inayomwajibisha kila mmoja wetu. Kwasasa mtu mmoja ndiye mfumo
 
Last edited by a moderator:
GalaxyS3,

..asante kwa posting yako #74 na napenda nakubaliana nayo kwa kiasi kikubwa.

..Dr.Magufuli ni Raisi wetu na hilo halina ubishi. Lakini pia hakuna ubishi kwamba Raisi wetu alipokuwa waziri alishiriki ktk baadhi ya ufisadi[uuzwaji ya nyumba za serikali], alifumbia macho ufisadi wa kila aina ambao anauibua sasa hivi, na zaidi alikuwa akizibeza waziwazi harakati[maandamano, hoja] za wapinzani kupinga ufisadi.

..Sasa mtu kama huyu anapobadilika ndani ya miezi michache, akianza kwenda kinyume na wale aliokuwa akiwaunga mkono kwa muda[20 years] mrefu, sioni ajabu wakitokea watu ambao hawatamuamini kabisa, au watakuwa wazito ku-join the bandwagon.

..Kwa uzoefu tulioupata kutoka kwa awamu za uongozi zilizopita, nadhani ktk awamu hii tunapaswa kuwa makini zaidi na kuhoji kila uamuzi unaochukuliwa na viongozi wetu. Lazima tutambue kwamba UMMA ndiyo mwajiri wa viongozi waliopigiwa kura.

cc Nguruvi3
 
Last edited by a moderator:
GalaxyS3,

..asante kwa posting yako #74 na napenda nakubaliana nayo kwa kiasi kikubwa.

..Dr.Magufuli ni Raisi wetu na hilo halina ubishi. Lakini pia hakuna ubishi kwamba Raisi wetu alipokuwa waziri alishiriki ktk baadhi ya ufisadi[uuzwaji ya nyumba za serikali], alifumbia macho ufisadi wa kila aina ambao anauibua sasa hivi, na zaidi alikuwa akizibeza waziwazi harakati[maandamano, hoja] za wapinzani kupinga ufisadi.

..Sasa mtu kama huyu anapobadilika ndani ya miezi michache, akianza kwenda kinyume na wale aliokuwa akiwaunga mkono kwa muda[20 years] mrefu, sioni ajabu wakitokea watu ambao hawatamuamini kabisa, au watakuwa wazito ku-join the bandwagon.

..Kwa uzoefu tulioupata kutoka kwa awamu za uongozi zilizopita, nadhani ktk awamu hii tunapaswa kuwa makini zaidi na kuhoji kila uamuzi unaochukuliwa na viongozi wetu. Lazima tutambue kwamba UMMA ndiyo mwajiri wa viongozi waliopigiwa kura.

cc Nguruvi3
 
Last edited by a moderator:
mbona chadema mlibadilisha gia angani kwa kusajili fisadi kuu...ambalo mliliita nyie kubwa la mafisadi...

sasa leo mnashangaa magufuli kupambana na mafisadi eti kwakuwa alifumbia macho ufisadi wakati akiwa waziri..

ni kuwa vita anayopigana magufuli sio cha mtoto tunajua wapo watu kama nyie mlinufaika na mnanufaika na ufisadi mtampinga na hatutawashangaa...
 
GalaxyS3,

..asante kwa posting yako #74 na napenda nakubaliana nayo kwa kiasi kikubwa.

..Dr.Magufuli ni Raisi wetu na hilo halina ubishi. Lakini pia hakuna ubishi kwamba Raisi wetu alipokuwa waziri alishiriki ktk baadhi ya ufisadi[uuzwaji ya nyumba za serikali], alifumbia macho ufisadi wa kila aina ambao anauibua sasa hivi, na zaidi alikuwa akizibeza waziwazi harakati[maandamano, hoja] za wapinzani kupinga ufisadi.

..Sasa mtu kama huyu anapobadilika ndani ya miezi michache, akianza kwenda kinyume na wale aliokuwa akiwaunga mkono kwa muda[20 years] mrefu, sioni ajabu wakitokea watu ambao hawatamuamini kabisa, au watakuwa wazito ku-join the bandwagon.

..Kwa uzoefu tulioupata kutoka kwa awamu za uongozi zilizopita, nadhani ktk awamu hii tunapaswa kuwa makini zaidi na kuhoji kila uamuzi unaochukuliwa na viongozi wetu. Lazima tutambue kwamba UMMA ndiyo mwajiri wa viongozi waliopigiwa kura.

cc Nguruvi3
Thank you Sir, na kwa kuongezea kidogo , katika bunge ameahidi kumalizia kiporo cha katiba
Katiba iliyoandikwa na wana mfumo kwa lengo la kulinda masilahi yao. Na hakuna historia inayoonyesha Magufuli aliwahi kupingana na serikali kuhusu mambo anayoyatekeleza. Zaidi alikuwa anasifia

Leo tunaambiwa huyu ndiye 'masiah' aliyekuwa anasubiriwa na Taifa. Masiah aliyetumikia mfumo mbovu na ambaye mfumo huo huo umemwezesha. Anataka kubadilika na tunaambiwa na wapiga filimbi, mabadiliko

Tunataka mabadiliko ya kimfumo si sura za makatibu wakuu. Hatutaki mazoea na maguvu, tunataka system inayo operate bila kuwa na msukumo wa mtu au wanaharakati wanaaogeuka kuwa watendaji
 
Kwa hiyo unataka kusema awape nchi mataahira ukawa? Haiwezekani!
Atabadili mfumo koutendaji, na kama ni kichama basi kiibuke chama kingine chenye nia ya dhati, hapo watapokezana kwa kigezo cha nini umewafanyia wananchi!
 
mfumo tulionao tanzania ni mzuri ila tulikosa msimamizi makini wa mfumo huo na matokeo yake tumekuwa ni watu wa kulalamika...

hata uwe na mfumo wa namna gani kama huna wasimamizi wazuri wa sheria na taratibu huo mfumo sio lolote sio chochote...

kikubwa tushukuru tumempata rais wa kusimamia sheria na taratibu ambazo zinaunda mfumo tunaouzungumzia...sasa jamii inaenda inatambua kuwa kazi ndio uti wa mgongo wa uchumi wa nchi kustawi...bila kufanya kazi tutabaki watu wa kulalamika tuuuu.
kama mfumo ulikuwa mzuri iliwezekanaje basi kuwepo loopholes zilizowezesha kuwa na wasimamizi wabovu?tunahitaji mfumo imara unaoweza kujisimamia,na unaoweza kuwasimamia na kuwadhibiti watovu wa nidhamu za kiuongozi,na ikiwezekana uende mbali zaidi kwa kuminya mianya inayowezesha kupatikana viongozi wabovu,huo ndiyo mfumo bora.
 
Kwanza naomba kukufahamisha kuwa kila Rais ana style Yake ya uongozi. Kusema Dr. Magufuli atafeli hayo ni maoni yako hivyo tuyaache. Wengine tunaamini atafanikiwa tena sana tu na tunamuombea Mungu amsaidie.

Pili nimekufahamisha kuwa Sijapinga hoja yako kuwa anatakiwa kubadili mfumo. Issue hapa ni namna anavyobadilisha huo mfumo. Sio lazima afanye au atumie kanuni unayotaka wewe.

Elewa kwamba Mhe. Rais amejipanga na hayo yote anayafahamu. Kwa sasa anaweka msingi, kadri tunavyoendelea msingi unaendelea kujengenga na tumeona mambo ya business as usual yakaanza kutoweka.

Serikali iko makini iachwe ifanyw kazi badala ya kila kukicha kukosoa na kutoa unabii wa kuzimu mara ooooh!! atashindwa mara Oooohhhhh..... tuache longolongo jamani. Hata haya aliyoyafanya mpaka sasa ni mfumo tofauti na yote ILIYOPITA.

Queen Esther
Queen kila mtu ana haki ya kutoa maoni yake, nami ninatoa yangu.
Ima maoni yanakera hilo linabaki kuwa suala la mtu.

Kinyume cha kufeli ni kufaulu.Endapo unataka afaulu, huna budi kukubali neno kufeli kutumiwa na mwingine

Ninaposema atafeli haina maana nataka afeli, bali namsaidia kuona anguko mbele yake

Historia ni mwalimu mzuri , na kama hatujifunzi basi vichwa vyetu vinahitaji mabadiliko, tutamuomba aangalie na hilo pia

Mfumo anaohangaika nao ameuhudumia kwa miaka 20. Hakuna mahali penye kumbu kumbu za kuonyeshwa amekerwa

Ima anataka kuubadili hilo ni jema, tunachosema hapa ni kuwa utendaji na majukumu ni kazi za kila siku si mabadiliko

Mabadiliko ni mageuzi katika namna za jinsi tunavyopanga na kutenda mambo yetu.
Lakini pia kumbuka, mabadiliko yanaweza kuwa mabovu tu si lazima yawe mazuri

Mfumo ulioweka TRA , Bodi, PCCB, DCI,DPP n.k. ni ule ule.

Kuweka msingi si kufukuza wakurugenzi au kurepea MRI

Ni kuanza na kujenga taratibu zitakazomwezesha kufanya mabadiliko ya dhati na ya kudumu 'game changer'

Ni kuulize, hivi mkuu wa idara ya rushwa anawezaje kuwajibika kwa mkuu wake aliyemteua?

PCCB wanaweza kukwaza kwasababu tu ya kimemo kidogo cha mstari mmoja 'acha hiyo issue'

Ninauliza tena na tena, kwanini bosi wa TRA alikiri kuwa na majina na hakuyafanyia kazi?
Kwanini vyombo vingine vilijua na havikufanyia kazi?

Msingi upi unaojengwa wa kumfukuza bosi wa TRA anayeweza kupewa kimemo cha 'acha makontena ' bila maelezo?
Je hiyo haikuwa fursa ya kufumua na kuonyesha uozo mzima wa mfumo, na hapa kukubaliana nasi!

Niliwahi 'kusikia' tetesi tu za wapiga domo, kuna shirika lina mradi na anaye supply vifaa ni kujana wetu.
PCCB waende kumchunguza kijana wetu, TRA wazuie mali za kijana wetu na Bandari wacheleweshe mzigo wa kijana!!! Nani asiyejipenda kiasi hicho!

Tunaweza kuona uzembe bila kuangalia unatokea wapi. Jiulize, kwanini wapinzani waliposema PCCB iwajibike kwa chombo kingine hoja yao ilikataliwa. Jiulize kwanini walikataa rasimu na kuandika yao kama ya 1977.

Jibu ni rahisi, kubadili mfumo ni kubadili maisha yao.Kama Rais hataanza kubadili mfumo, ataishia kubadili wakurugenzi

Ili kupambana na mambo kama rushwa na ufisadi, lazima utoe uhuru kwa vyombo husika

Unaona jinsi ya kutenda mambo bila utaratibu yanavyolitia Taifa aibu.
Leo wafanyakazi wanaswekwa mahabusu, wengine wanakataliwa likizo kwasababu tu watu wanataka na si utaratibu, yaani 'fire work'

kwamba king'ora kikilia magari yote yanakwenda eneo moja kuzima moto kwa haraka , kisha wanarudi ofisini kupumzika

Na mwisho, tuvumiliane katika majadiliano. Inauma lakini ukweli usemwe.

Tumevumilia miaka 50 kila mwaka tukitoa benefit of doubt.

Tutaendelea hadi lini bila sisi kusimama na kusema 'tunaona tatizo mbele ya safari'? a.k.a kufeli

Kuna ubaya gani kuelekeza njia badala ya kubeba makuyamba na manyanga, vibwebwe na mapambio bila kutumia kiungo juu ya mabega?
 
Thank you Sir, na kwa kuongezea kidogo , katika bunge ameahidi kumalizia kiporo cha katiba
Katiba iliyoandikwa na wana mfumo kwa lengo la kulinda masilahi yao. Na hakuna historia inayoonyesha Magufuli aliwahi kupingana na serikali kuhusu mambo anayoyatekeleza. Zaidi alikuwa anasifia

Leo tunaambiwa huyu ndiye 'masiah' aliyekuwa anasubiriwa na Taifa. Masiah aliyetumikia mfumo mbovu na ambaye mfumo huo huo umemwezesha. Anataka kubadilika na tunaambiwa na wapiga filimbi, mabadiliko

Tunataka mabadiliko ya kimfumo si sura za makatibu wakuu. Hatutaki mazoea na maguvu, tunataka system inayo operate bila kuwa na msukumo wa mtu au wanaharakati wanaaogeuka kuwa watendaji



Kuna mtu kasema labda Magufuli alete 'maridhiano' kwanza
manake tukianza kuchimba kila palipo na uozo na yeye tumuulize
kivuko kibovu cha MV Daresalaam..laiti kama system ingekuwa hai pengine asingekuwa Rais now..
 
Hiki tunakiongea kila siku. Kwa bahati mbaya wapambe na wasaka tonge hawataki kusikia ukweli.Wanachotaka ni kusikia Magufuli anasifiwa.

Sisi wengine tunasema kama hatabadili mfumo, hataleta Watanzania pamoja kwa kuwasikiliza, ATAFELI muda si mrefu

Nchi haibadilishwi na mtu bali watu. Na nchi haibadilishwi kwa kiboko bali kubadili Mifumo ikiwemo ile inayolinda masilahi yake. Huo ndio ukweli!

Hatuhitaji kufukuzwa wakurugenzi au makamishna. Tunataka mfumo utakaohakikisha hatupati makamishna wabovu na wakipataika kwa bahata mbaya mfumo utawaondoa bila kupoteza muda

Kwa hili nakubaliana na Maggid, kwamba suala si Magufuli na fukuza fukuza.

Suala ni kuwa kuna mifumo itakayohakikisha haturudii makosa ya nyuma?

Mfumo utakaoziba mianya ya viongozi ku abuse ofisi kama tulivyoona miaka 6 iliyopita

Mkuu huo mfumo ni upi?
 
Queen kila mtu ana haki ya kutoa maoni yake, nami ninatoa yangu.
Ima maoni yanakera hilo linabaki kuwa suala la mtu.

Kinyume cha kufeli ni kufaulu.Endapo unataka afaulu, huna budi kukubali neno kufeli kutumiwa na mwingine

Ninaposema atafeli haina maana nataka afeli, bali namsaidia kuona anguko mbele yake

Historia ni mwalimu mzuri , na kama hatujifunzi basi vichwa vyetu vinahitaji mabadiliko, tutamuomba aangalie na hilo pia

Mfumo anaohangaika nao ameuhudumia kwa miaka 20. Hakuna mahali penye kumbu kumbu za kuonyeshwa amekerwa

Ima anataka kuubadili hilo ni jema, tunachosema hapa ni kuwa utendaji na majukumu ni kazi za kila siku si mabadiliko

Mabadiliko ni mageuzi katika namna za jinsi tunavyopanga na kutenda mambo yetu.
Lakini pia kumbuka, mabadiliko yanaweza kuwa mabovu tu si lazima yawe mazuri

Mfumo ulioweka TRA , Bodi, PCCB, DCI,DPP n.k. ni ule ule.

Kuweka msingi si kufukuza wakurugenzi au kurepea MRI

Ni kuanza na kujenga taratibu zitakazomwezesha kufanya mabadiliko ya dhati na ya kudumu 'game changer'

Ni kuulize, hivi mkuu wa idara ya rushwa anawezaje kuwajibika kwa mkuu wake aliyemteua?

PCCB wanaweza kukwaza kwasababu tu ya kimemo kidogo cha mstari mmoja 'acha hiyo issue'

Ninauliza tena na tena, kwanini bosi wa TRA alikiri kuwa na majina na hakuyafanyia kazi?
Kwanini vyombo vingine vilijua na havikufanyia kazi?

Msingi upi unaojengwa wa kumfukuza bosi wa TRA anayeweza kupewa kimemo cha 'acha makontena ' bila maelezo?
Je hiyo haikuwa fursa ya kufumua na kuonyesha uozo mzima wa mfumo, na hapa kukubaliana nasi!

Niliwahi 'kusikia' tetesi tu za wapiga domo, kuna shirika lina mradi na anaye supply vifaa ni kujana wetu.
PCCB waende kumchunguza kijana wetu, TRA wazuie mali za kijana wetu na Bandari wacheleweshe mzigo wa kijana!!! Nani asiyejipenda kiasi hicho!

Tunaweza kuona uzembe bila kuangalia unatokea wapi. Jiulize, kwanini wapinzani waliposema PCCB iwajibike kwa chombo kingine hoja yao ilikataliwa. Jiulize kwanini walikataa rasimu na kuandika yao kama ya 1977.

Jibu ni rahisi, kubadili mfumo ni kubadili maisha yao.Kama Rais hataanza kubadili mfumo, ataishia kubadili wakurugenzi

Ili kupambana na mambo kama rushwa na ufisadi, lazima utoe uhuru kwa vyombo husika

Unaona jinsi ya kutenda mambo bila utaratibu yanavyolitia Taifa aibu.
Leo wafanyakazi wanaswekwa mahabusu, wengine wanakataliwa likizo kwasababu tu watu wanataka na si utaratibu, yaani 'fire work'

kwamba king'ora kikilia magari yote yanakwenda eneo moja kuzima moto kwa haraka , kisha wanarudi ofisini kupumzika

Na mwisho, tuvumiliane katika majadiliano. Inauma lakini ukweli usemwe.

Tumevumilia miaka 50 kila mwaka tukitoa benefit of doubt.

Tutaendelea hadi lini bila sisi kusimama na kusema 'tunaona tatizo mbele ya safari'? a.k.a kufeli

Kuna ubaya gani kuelekeza njia badala ya kubeba makuyamba na manyanga, vibwebwe na mapambio bila kutumia kiungo juu ya mabega?
Queen kila mtu ana haki ya kutoa maoni yake, nami ninatoa yangu.
Ima maoni yanakera hilo linabaki kuwa suala la mtu.

Kinyume cha kufeli ni kufaulu.Endapo unataka afaulu, huna budi kukubali neno kufeli kutumiwa na mwingine

Ninaposema atafeli haina maana nataka afeli, bali namsaidia kuona anguko mbele yake

Historia ni mwalimu mzuri , na kama hatujifunzi basi vichwa vyetu vinahitaji mabadiliko, tutamuomba aangalie na hilo pia

Mfumo anaohangaika nao ameuhudumia kwa miaka 20. Hakuna mahali penye kumbu kumbu za kuonyeshwa amekerwa

Ima anataka kuubadili hilo ni jema, tunachosema hapa ni kuwa utendaji na majukumu ni kazi za kila siku si mabadiliko

Mabadiliko ni mageuzi katika namna za jinsi tunavyopanga na kutenda mambo yetu.
Lakini pia kumbuka, mabadiliko yanaweza kuwa mabovu tu si lazima yawe mazuri

Mfumo ulioweka TRA , Bodi, PCCB, DCI,DPP n.k. ni ule ule.

Kuweka msingi si kufukuza wakurugenzi au kurepea MRI

Ni kuanza na kujenga taratibu zitakazomwezesha kufanya mabadiliko ya dhati na ya kudumu 'game changer'

Ni kuulize, hivi mkuu wa idara ya rushwa anawezaje kuwajibika kwa mkuu wake aliyemteua?

PCCB wanaweza kukwaza kwasababu tu ya kimemo kidogo cha mstari mmoja 'acha hiyo issue'

Ninauliza tena na tena, kwanini bosi wa TRA alikiri kuwa na majina na hakuyafanyia kazi?
Kwanini vyombo vingine vilijua na havikufanyia kazi?

Msingi upi unaojengwa wa kumfukuza bosi wa TRA anayeweza kupewa kikujana wetu.
PCCB waende kumchunguza kijana wetu, TRA wazuie mali za kijana wetu na Bandari wacheleweshe mmemo cha 'acha makontena ' bila maelezo?
Je hiyo haikuwa fursa ya kufumua na kuonyesha uozo mzima wa mfumo, na hapa kukubaliana nasi!

Niliwahi 'kusikia' tetesi tu za wapiga domo, kuna shirika lina mradi na anaye supply vifaa ni zigo wa kijana!!! Nani asiyejipenda kiasi hicho!

Tunaweza kuona uzembe bila kuangalia unatokea wapi. Jiulize, kwanini wapinzani waliposema PCCB iwajibike kwa chombo kingine hoja yao ilikataliwa. Jiulize kwanini walikataa rasimu na kuandika yao kama ya 1977.

Jibu ni rahisi, kubadili mfumo ni kubadili maisha yao.Kama Rais hataanza kubadili mfumo, ataishia kubadili wakurugenzi

Ili kupambana na mambo kama rushwa na ufisadi, lazima utoe uhuru kwa vyombo husika

Unaona jinsi ya kutenda mambo bila utaratibu yanavyolitia Taifa aibu.
Leo wafanyakazi wanaswekwa mahabusu, wengine wanakataliwa likizo kwasababu tu watu wanataka na si utaratibu, yaani 'fire work'

kwamba king'ora kikilia magari yote yanakwenda eneo moja kuzima moto kwa haraka , kisha wanarudi ofisini kupumzika

Na mwisho, tuvumiliane katika majadiliano. Inauma lakini ukweli usemwe.

Tumevumilia miaka 50 kila mwaka tukitoa benefit of doubt.

Tutaendelea hadi lini bila sisi kusimama na kusema 'tunaona tatizo mbele ya safari'? a.k.a kufeli

Kuna ubaya gani kuelekeza njia badala ya kubeba makuyamba na manyanga, vibwebwe na mapambio bila kutumia kiungo juu ya mabega?
Kwa hisani ya RAIA MWEMA Raia Mwema - Siri ya Kikwete TRA yaanikwa
Queen Esther umeona jinsi tunavyoona umbali zaidi ya pua zetu

Kwa wale waliobeza kauli yetu ya mfumo ndio tatizo hapa mnasemaje?

Je, bado mna mtima wa kushanglia?

Nyani Ngabu JokaKuu Jasusi Mchambuzi dolevaby Pasco
 
Last edited by a moderator:
Wewe ndie unayeona mwisho wa pua yako.

Nakushauri katafute hotuba ya Rais MSTAAFU Dr. JMK siku ya 9 Dec ndio uje uchangie tena. Hao Home Shopping Centre nao wametoa maelezo.

My point is, wafanyakazi wa Serikali tuzingatie maadili ya kazi. Unaweza kurukwa maili 100 unabaki unatoa macho. Issue ni sisi wenyewe tunaharibu mfumo. Pia Kama kuna mwenye ki note cha wakubwa, basi mahakamani ndio mahala penyewe ili mbivu na mbichi zijulikane.

Narudia tena wafanyakazi wa Serikali na Mashirika ya Umma wakifuata sheria za kazi na maadili mfumo utaji align automatically. The do's and don't s of course. Shida wengi nao walikuwa wapiga deal wala usiwatetee. Ngoja JPM aweke misingi IMARA Kama anavyofanya na utaona nyumba (mfumo) unavyojengeka kwa kufuata michozo ya msingi. The rest ni decorations (mbwembwe).

Queen Esther

Kwa hisani ya RAIA MWEMA Raia Mwema - Siri ya Kikwete TRA yaanikwa
Queen Esther umeona jinsi tunavyoona umbali zaidi ya pua zetu

Kwa wale waliobeza kauli yetu ya mfumo ndio tatizo hapa mnasemaje?

Je, bado mna mtima wa kushanglia?

Nyani Ngabu JokaKuu Jasusi Mchambuzi dolevaby Pasco
 
Watu wamekazana na mfumo..mfumo,mfumo. Hata kama ukibadili mfumo.... kama 'mindset' za watu zitabaki zilezile ni bure. Kenya wamebadili kila kitu. katiba,mfumo .lakini wapi. Ufisadi Kenya ndio kwanza unapamba moto.
 
Watu wamekazana na mfumo..mfumo,mfumo. Hata kama ukibadili mfumo kama 'mindset' za watu zitabaki zilezile ni bure. Kenya wamebadili kila kitu. katiba,mfumo .lakini wapi. Ufisadi Kenya ndio kwanza unapamba moto.
Jamii na Queen Esther sina uhakika kama mumesoma taarifa mkaielewa kwa undani.
Kuna kusoma habari na kuelewa habari ni vitu viwili tofauti

Ukisoma kwa umakini utaona maelezo yanayosema 'watendaji waaminifu wakakatishwa tama' Maana yake , hawakuwa na uwezo zaidi baada ya kufanya kazi zao. Mafaili yalitua eneo husika kwa hatua yakakaliwa tu

Mfumo ungekuwa upo sawa haya tunayoyaona yasingetokea. Kama tutakubaliana kuwa hizi ndizo hatua zinazopaswa kuchukuliwa, baada ya miaka 5 tutagundua mafaili mengine yamekaliwa hivi hivi.

Sababu kubwa ni kuwa uwezo wa kushiriki katika kutatua matatizo upo mikononi mwa mtu mmoja, that's wrong

Ingalikuwa kwa wenzetu uchunguzi ungefanyika na mafaili yaliyopo yangepitiwa kuona nani amebofoa
Kwetu sisi tunashangilia hatua za reja reja na si za jumla

DCI,DPP au PCCB zingekuwa ni vyombo huru tungeweza kujua kwa uhakika nani amehusika na kwa njia ipi

Vyombo vyote hivyo vinaripoti kwa mtu mmoja, ambaye ana nguvu zaidi yao. Hiyo ni sawa kweli?

Hatuwezi kuchukua Kenya kama role model, tuangalie kwa upana wake.
Kwanini tusiangalie Scotland Yard, FBI, nchi kama Denmark, na zile za Scandinavia ambazo zimefanikiwa kupunguza tatizo

Ukisoma habari hiyo na kuunganisha na hotuba ya Rais utaona kuna jambo.

Rais alipoongea na wafanyabiashara aliwapa siku 7 walipe kodi.
Inawezekana nia yake ni njema, kwamba tupate mapato ya kodi na kuzuia mianya

Tatizo linakuja, hawezi kuchukua hatua zaidi kwasababu mafaili yamekaliwa ofisini na mtu asiyewezi kumchukulia hatua. Rais amefika mahali hawezi kwenda mbali zaidi, kwa lugha nyingine amekwama au amefeli

Anaweza kuwa na nia njema, hana vitendea kazi au mazingira ya kumwezesha kuziba mianya na kwa ufumbuzi wa kudumu

Kuhusu wafanyakazi, lazima muelewe kuwa sheria zipo kwa kutambua uwepo wa watu wenye nia mbaya.
Huwezi kulaumu wakosefu wa maadili ukidhani una solve tatizo.

Mhalifu nia yake ni uhalifu, lugha ya kuongea naye si kumbeleza awe mzalendo.

Ukishakuwa mhalifu ni mhalifu tu , hivyo kushauri waombewe dua misikitini na makanisani ni ufupi wa fikra

Mhalifu anafikishwa mahali stahiki ili kukabiliana na sheria. Sheria kama hazitoi nafasi ya kusimamiwa ni kazi bure

Tofauti yangu na yenu ni moja, mnataka kazi za zimamoto , ninataka sustainable solution

Mzee Warioba kaongea juzi na kusisitiza kuwa alishindwa kupambana na rushwa kwasababu mfumo wetu haukumpa nafasi. Mind you huyu ni waziri mkuu na makamu wa Rais mstaafu. Yeye anajua ugumu aliopambana nao

Mzee Warioba akasema, kama hatutabadili mfumo, kazi inayofanyika haitakuwa na matunda

Hebu nielezeni, katika mazingira yafutayo tutawezaje kupambana na rushwa?

DCI, DPP, PCCB wanaripoti kwa Rais. Kamishna wa TRA anaripoti kwa Rais, IGP anaripoti kwa Rais, Bodi ya TRA inachaguliwa na Rais, Watendaji wa TRA wanateuliwa na Bodi. Waziri wa Fedha ni mteule wa Rais. Intelejensia ya nchi inaripoti kwa Rais.

Nauliza, checks and balances ipo wapi wandugu? Hili si kama gulio tu kila mtu ana lake!

Hatuwezi kujitawala kama gulio, kwanini tusijaribu kujipanga ili tuwe kama Super Market
 
Last edited by a moderator:
prove me wrong dude

Haitoshi kusema wrong ukiwa huna hoja za kuonyesha kwanini ni wrong

Hebu mpuuze huyo ndg ili asihamishe mada.
Watz nasi tusaidie kujenga misingi ya mfumo mpya imara kwa kupuuza mayowe ya watu wasio na hoja. Twende mbele kwa kutambua nini kiwemo katika katiba mpya, na hatimae sheria zetu, ili kujenga tena uadilifu na uwajibikaji uliyopotea.
 
Back
Top Bottom