Wakudadavuwa
JF-Expert Member
- Feb 17, 2016
- 17,506
- 15,997
Ndugu zangu,
Rais Samia kwa nia njema kabisa ametaka TRA waache mabavu kukusanya kodi. Ila kwa uzoefu na hulka ya binadamu huwa hawapendi kulipa kodi. Naam kodi ikusanywe kwa mujibu wa sheria bila uonevu ila kuna haya ya kuangaliwa laa sivyo serikali itakosa zaidi;
Mosi, kukubali hadharani kuwa miezi mitano au sita ijayo mapato ya serikali yatashuka ni ujumbe kwa TRA kuwa wasifanye jitihada kukusanya mapato.Sijajua serikali itafidia vipi upungufu huu wa makusanyo.
Pili, ni hulka ya binadamu kutopenda kulipa kodi sasa kuamini kuwa mfanyabiashara atatoa taarifa zake sahihi kwa TRA hapa kuna shida na hii inatoa mwanya mkubwa kwa watumishi wa TRA na Wafanyabiashara kuamua ngapi ziende Serikalini.
Nimalize kwa kusema kuwa maagizo ya Rais Samia kuhusu kodi yamepata tafsiri potofu na kama serikali isiporekebisha yale malengo ya kukusanya trilioni mbili kila mwezi yatabaki kama matamanio.
Rais Samia kwa nia njema kabisa ametaka TRA waache mabavu kukusanya kodi. Ila kwa uzoefu na hulka ya binadamu huwa hawapendi kulipa kodi. Naam kodi ikusanywe kwa mujibu wa sheria bila uonevu ila kuna haya ya kuangaliwa laa sivyo serikali itakosa zaidi;
Mosi, kukubali hadharani kuwa miezi mitano au sita ijayo mapato ya serikali yatashuka ni ujumbe kwa TRA kuwa wasifanye jitihada kukusanya mapato.Sijajua serikali itafidia vipi upungufu huu wa makusanyo.
Pili, ni hulka ya binadamu kutopenda kulipa kodi sasa kuamini kuwa mfanyabiashara atatoa taarifa zake sahihi kwa TRA hapa kuna shida na hii inatoa mwanya mkubwa kwa watumishi wa TRA na Wafanyabiashara kuamua ngapi ziende Serikalini.
Nimalize kwa kusema kuwa maagizo ya Rais Samia kuhusu kodi yamepata tafsiri potofu na kama serikali isiporekebisha yale malengo ya kukusanya trilioni mbili kila mwezi yatabaki kama matamanio.