KIBURUDISHO
JF-Expert Member
- Mar 28, 2011
- 1,002
- 274
WanaJF wenzangu habari za majukumu tafadhali naombeni kwa wanaofahamu tiba ya ugonjwa huu wa kupooza upande mmoja uliompata mama yangu anateseka.Kwa mara ya kwanza ulimtokea mwezi wa 5 akapewa dawa za kienyeji akapata nafuu.Lakini ilipofika leo asubuhi hiyo hali imejirudia upya yaani anapitisha tu udenda tunaambiwa ugonjwa huu haupaswi mgonjwa akadungwa sindano sasa najiuliza wapi nitakapopata tiba ya kumponya mamaangu naombeni ushauri wenu.