tafadhali soma hapa

mama pita

Member
Joined
Jul 20, 2012
Posts
97
Reaction score
140
natumain mu wazima kwa wagonjwa polen

nilikua na mahusiano na kaka mmoja kifupi tulipenda bt baada ya kupata ujauzito tukawa hatuelewan bila hata sababu ugomvi kila siku hata usiokua na maana hatukua tunaishi pamoja tulikua tunaishi mikoa tofauti

kama wiki 3 zimepita mdogo wake katusululisha yameisha na nimeamua nikae nae mpaka hapo nitakapojifungua nitaona cha kufanya ujauzito una miez 5
point
tangu nimefika mwenzangu hana kabisa mapenzi na mimi, mapenzi yamepungua kabisa kwangu tangu nimepata ujauzito napenda kula udongo jana kauona kasema SITAKI UDONGO NYUMBANI NDANI KWANGU.
nimejaribu kumuelewesha unatokea nataman tu hata mimi siipendi hanielewi kabisa inshort hana mapenzi na mimi
wanajamvi nifanyeje nimrudishe katika hali yake ya kawaida??? nifanyeje ili upendo urudi najitahidi sana kumuonyesha nampenda namjali bt hayumo kabisa niongeze wapi ndugu zanguni????
SAMAHANI KWA KUWACHOSHA TUVUMILIANE TU JAMANI.
 
....kwani hana "hela"mbona hayo mambo madogo tu wewe vumilia.....
 

Inavyoonekana alikua anakupenda kwa ajili ya kumstarehesha n hakua na plan na wewe for future. Amejilazimisha kukuweka ndani na kuilea mimba na hana mapenzi kabisa. Ubaya wake ni kuwa anaonyesha kabisa kuwa hakupendi
 
pole sana dea usiumize kichwa huyo hana mpango na ww,kama unajiweza kujitunza rudi tu kwako hapo kakupend alikuwa anakutumia tu
 
Mimi ni mwanamume, nitakachokuambia ni sahihi kwa asilimia 93.
Huyo jamaa hana mapenzi na wewe kabisaa, hakuwahi kuwa na mpango wa kukuowa na hiyo mimba imeingia bila nyie kupanga kwamba sasa mzae, amekupokea kwa sababu tu hana jinsi, vinginevyo asingekupokea kabisa. Hapop kuna mawili, huenda ukishazaa mtoto anaweza kurejea kwenye furaha yake nakukubali matokeo kwamba tayari ameshakamatika na hana jinsi, baadaye mazowea yatachukua nafasi na kukubali reality. Au kama ni kichwa ngumu basi ndiyo utaishi kwa shida tu namna hiyo.
Ushauri wangu kwako.
Kaa naye mfungukie wazi, mwambie kwa upole akueleze kwa nini hakupendi na amebadilika baada ya wewe kupata ujauzito. Muulize ni nani aliyeingilia furaha yenu, ni huyo mgeni aliyeko tumboni, ni wewe umeishiwa mvuto,ni mapenzi tu yamefika ukomo au kuna mtu mwingine pembeni, usipepese jicho na useme ukiwa umemkodolea bila kurembua jicho. Muulize ni plan gani aliyonayo kwa kuzingatia kwamba kuna mgeni anakuja. Jaribu kushirikisha akil yakokung'amua ukweli.

Mwisho wa siku maisha yako ni wewe, kama mpenzi haeleweki subiri mpenzi wako wa kweli yuko tumboni atakufariji kwa kila kitu, labda kama hauna kipato hilo ni jaribu jingine. Mtoto huwa anakuja na baraka zake, hopefully ukizaa mambo yatakaa sawa, yasipokaa sawa angalia ustaarabu.
 
 
Acheni kutegeshea watu mimba kwa kudhani ndio penzi litaongezeka.

Kumbe ndio mnavyowaza???? Mkistareheshana hamkujua kuna ujauzito ??? Hapo hakuna cha kulaumiana wote wana makosa wavumiliane
 
Pole dear wanaume wengine ni vigeugeu hawana msimamo na maisha yao wakati mwingine wanashindwa kuamua hatma ya maisha yao, isiwe kigezo cha kukupeleka kwao na kutambulishwa kanisani akijazwa maneno na ndugu zake kuhusu ww na akawaamini huwa yanatokea hayo yaliokukuta. Yalisha nikuta nilitambulishwa mpaka kwa kadinali miaka ya nyuma mm na huyo mkaka tulikuwa tunaishi mikoa tofauti alikuja kwetu nikapelekwa kwao taratibu zikafuatwa na kanisani nikapelekwa na sala juu tukafanyiwa na kadinal yaliokuja kufuata ni kila mtu na maisha yake chokochoko za mawifi ndizo zilizo tutenganisha nikaona isiwe tabu kila nikijaribu kumweka mwanaume kwenye msatri anasikiliza ndugu zake nika sepa zangu sasa hivi nina maisha mapya nima mume anaye nijali na kunithamini kma nn. huyo kaka mpaka ya leo hajaoa amezaa tu kila mwanamke anaye peleka kwao mawifi wanamkataa na hajifunzi makosa yake ya kusikiliza madada zake na anaizidi kuzeena mwaka wa 45 hana future na maisha yake mpaka kesho.
 
Kukatazwa Kula udongo imekuwa nongwa??!! Acha hizo ww, lea mimba uzae.
 
kifupi ni kwamba Hakuitaji tena ila analazmika kuwa na wewe kwa sababu ya huo usuruhish amemuheshmu huyo ndugu yako. Na hayo ndo madhara ya kukurupuka kuaminiana na kutambulishana mapema
 
Pole ila ndo wanaume we omba Mungu ujfungue salama utajua cha kufanya
 
Kumbe ndio mnavyowaza???? Mkistareheshana hamkujua kuna ujauzito ??? Hapo hakuna cha kulaumiana wote wana makosa wavumiliane

Ndio maana kuna kinga...kama naww huwa unaenda unajiachia tu bila kuwa makini...Badilika
 
Kiufupi hamkupendana.....

Bali ulimpenda....

Mwenzio alikuwa anaponea tu... saaa hivi ndo anaona unamkera...

Chakufanya mama pita (mama yake na pita) tafuta ustaarabu wako mdogo mdogo kiufupi jipange namna utakavyoishi baada ya kujifungua.... then ukiwa tayari mpange na mwenzio jinsi mtakavyomlea mtoto

La sivyo utaendelea kunyanyasika tu hapo
 
Last edited by a moderator:

ivi kwani MWAFIKIRI NI RAHISI SANA KU LET GO, KULEA MTOTO MWENYEWE DUNIA HII BILA MSAADA WA MUME SI RAHISI, MSIRAHISISHE, WENGI MNAKUJA MWASEMA ETI JIPANGE, HUWEZI LEA MWANAO NA BLAH BLAH KIBAO,
ITS NT EASY.
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…