Juma Jongo
New Member
- Feb 14, 2018
- 4
- 1
USAJILI VITAMBULISHO VYA TAIFA WASHIKA KASI TABORA
Mamlaka ya Vitambulisho Vya Taifa (NIDA) imeendelea kufanya vizuri zoezi la usajili wa Vitambulisho Vya Taifa Mkoani Tabora ambapo Wilaya zote zinafanya zoezi hilo. Afisa Usajili wa Mkoa wa Tabora Bi Grace Msaky amesema kuwa wananchi wamelipokea vizuri zoezi la Usajili na Utambuzi wa watu ili kupata vitambulisho vya Taifa. Grace amesisitiza kuwa zoezi hilo ni muhimu hivyo wanachi wanapofikiwa kwenye kata zao wajitokeze wote kwa wingi ili kukamilisha mchakato huo.
Pia Mwakilishi wa kitengo cha Habari NIDA makao Makuu. Bw. Deodatus Mchaki amesisitiza kuwa Zoezi hilo ni BURE hivyo Mwananchi hatakiwi kuchangia garamayoyote.
Ili kusajiliwa ni lazima Mwananchi afike na nakala (copy) ya nyaraka/viambatanisho muhimu vya kuweza kumtambulisha uraia wake, umri na makazi. Mfano wa nyaraka hizo ni; Kadi ya mpiga kura, cheti cha kuzaliwa, leseni ya udereva, ID ya Mzanzibar mkazi, TIN, Pasi ya kusafiria, vyeti vya elimu nk.
Wananchi wanweza kuwasiliana na NIDA moja kwa moja na kituo cha huduma kwa mteja kwa namba; 0673333444/0687416666, 0779102010, 0743201020, 0765201020, ama namba isiyo na tozo 0800758888, Tuandikie S.L.P 12324, Barua pepe; nida.tanzania@nida.go.tz
Wananchi wa kata ya Ipuli mtaa wa Ipuli Halmashauri ya Wilaya ya Tabora wakiwa kwenye foleni tayari kufanya HAtua ya pili ya kupigwa picha na kuchukuliwa alama za kibaiolojia.
Shaban Yasin mkazi wa mtaa wa Nane nane kata ya Ipuli akichukuliwa alama za Vidole (fingerprint) kwenye zoezi la usajili wa vitambulisho vya Taifa
Mamlaka ya Vitambulisho Vya Taifa (NIDA) imeendelea kufanya vizuri zoezi la usajili wa Vitambulisho Vya Taifa Mkoani Tabora ambapo Wilaya zote zinafanya zoezi hilo. Afisa Usajili wa Mkoa wa Tabora Bi Grace Msaky amesema kuwa wananchi wamelipokea vizuri zoezi la Usajili na Utambuzi wa watu ili kupata vitambulisho vya Taifa. Grace amesisitiza kuwa zoezi hilo ni muhimu hivyo wanachi wanapofikiwa kwenye kata zao wajitokeze wote kwa wingi ili kukamilisha mchakato huo.
Pia Mwakilishi wa kitengo cha Habari NIDA makao Makuu. Bw. Deodatus Mchaki amesisitiza kuwa Zoezi hilo ni BURE hivyo Mwananchi hatakiwi kuchangia garamayoyote.
Ili kusajiliwa ni lazima Mwananchi afike na nakala (copy) ya nyaraka/viambatanisho muhimu vya kuweza kumtambulisha uraia wake, umri na makazi. Mfano wa nyaraka hizo ni; Kadi ya mpiga kura, cheti cha kuzaliwa, leseni ya udereva, ID ya Mzanzibar mkazi, TIN, Pasi ya kusafiria, vyeti vya elimu nk.
Wananchi wanweza kuwasiliana na NIDA moja kwa moja na kituo cha huduma kwa mteja kwa namba; 0673333444/0687416666, 0779102010, 0743201020, 0765201020, ama namba isiyo na tozo 0800758888, Tuandikie S.L.P 12324, Barua pepe; nida.tanzania@nida.go.tz
Wananchi wa kata ya Ipuli mtaa wa Ipuli Halmashauri ya Wilaya ya Tabora wakiwa kwenye foleni tayari kufanya HAtua ya pili ya kupigwa picha na kuchukuliwa alama za kibaiolojia.
Shaban Yasin mkazi wa mtaa wa Nane nane kata ya Ipuli akichukuliwa alama za Vidole (fingerprint) kwenye zoezi la usajili wa vitambulisho vya Taifa