Mwizukulu wa Buganda
JF-Expert Member
- Nov 19, 2024
- 638
- 1,771
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paul Chacha, amezielekeza taasisi serikali zaidi ya 20 mkoani humo kuandika barua na kujieleza kwa nini zimeshindwa kushiriki katika shughuli muhimu za serikali, zikiwemo za Mwenge wa Uhuru na Maonesho ya Nanenane Kanda ya Magharibi.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya Nanenane yanayofanyika katika viwanja vya Nanenane Ipuli Manispaa ya Tabora, Chacha amesema kitendo hicho kimeleta picha mbaya kwa umma kwani wananchi wamejitokeza kwa wingi, lakini taasisi hizo hazikuonekana kushiriki kama sehemu ya mamlaka ya serikali.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya Nanenane yanayofanyika katika viwanja vya Nanenane Ipuli Manispaa ya Tabora, Chacha amesema kitendo hicho kimeleta picha mbaya kwa umma kwani wananchi wamejitokeza kwa wingi, lakini taasisi hizo hazikuonekana kushiriki kama sehemu ya mamlaka ya serikali.