Hahahaha,aisee hii kali.
Ila wengi tunaolalamika ndio hao hao tumeowazoesha.
Wale madada wana tabasam kali,na mtu akienda Supermarket anaenda kinyangema kweli,sasa ukiambiwa hakuna mia unajichekelesha,tehetehetehete,haina shida dada.
Usishangae hata mleta uzi leo tena kaenda kaacha pesa.
Maana ndio Heshma ya Supermarket,tusioweza jamani tununue mitaani,kuna mini supermarket kibaooo,hata change ya hamsini unapewa na vitu ni vilevile.
We umesimama unadai Mia,wakati pembeni kuna mdada yeye kaacha mia nne kabisaa.
Mie nitaendelea kuziacha hizi mia mia saana,maana nimetaka mwenyewe kwenda Supemarket,yaani niambiwe mia sina halafu eti nikomae Counter?aisee acheni zenu wakuu,huko Bar zinaachwa ngapi.
We Supermarket ma Coins ya nini,we huoni baadhi ya bei unaambiwa 99,999,hahaha hujajua tu?
Hembu Zipeni Supermarket heshma,acheni mambo ya vimia mia vyenu,hamuwezi nunue vitu uswahili vipo telee tena bei chee