Tabia hizi katika Supermarkets zinaboa

Tabia hizi katika Supermarkets zinaboa

98mzavallah

Member
Joined
Feb 13, 2015
Posts
37
Reaction score
12
Kweli kajitabia cha wafanyakazi wa supermarkets kutorudisha chenji ya shillingi 100 & 200 itakwisha lini?

Utasikia samahani kaka/ dada, sina sh 100. Mi sitaki kuamini ya kwamba mauzo ya siku nzima katika supermarkets inakosekana shilingi 100 na 200!.

Kwa sasa imekua kama ni kamchezo cha kujikusanyia pesa kwa hawa wadada wanaofanya hizi supermarket haswa ile ya Q... pale.

Tabia hiyo inatuboa wateja wenu, acheni.
 
Kila mtu anahaki ya kurudishiwa kitu ambacho ni halali yake, kama unadai shl. 100 ni haki yako, njia za kutunza vzr uchumi wako ni kuwa makini na kila shilingi ambayo ni yako, watu wanachukulia poa ndo maana kila cku wanalia maisha magumu, shilingi ya kitanzania inashuka thamani, hii yote ni kwasababu tunawaachia wengine hela zetu kwa kudharau kwamba ni ndogo au kuona aibu kuzidai
 
Bilioni inaanza na sh 1/=... kwa hyo kila sent ina jasho na thamani yake.
Rudi kwenye shelve chukua kitu cha bei kisha mwambie na ww umepungikiwa. Juhudi atakazo tumia kukubana ulipe ndizi atumie kukutafutia 100
 
Jana tu Uchumi wamenidhulumu mia tatu yangu, dawa yao ninayo, ni kuanza kuchukuwa zile chocolate karibu na cashier halafu unawaambia wewe pesa iliyopelea utawaletea kesho.

Uchumi ndio zao hizo
Naona kuna kafaida ka sirisiri wamegundua kukatengeneza kwa chenji za watu
 
Hao ni wezi tu kwani supermarkets zote duniani huwa zinakuwa na vitu vidogovidogo kama pipi na biskuiti kaunta ili wakikosa chenji ndogo humpa mteje. pia ni jukumu lao kuandaa hizo miamia toka kwenye mabenki
 
Kama hamna chenji ya sh 100 na 200 basi vitu vyao vote bei ya chini ianzie 500...
 
Back
Top Bottom