Taasisi ya Didier Drogba kikaangoni kwa kula fedha za wahisani

real G

JF-Expert Member
Feb 7, 2013
5,227
5,296
Ni asilimia 1 katika paundi milioni 1.7 zilizochangwa na mastaa na wafanyabiashara wa Uingereza kwaajili ya kuisaidia taasisi iliyoanzishwa na mchezaji wa zamani wa Chelsea, Didier Drogba, zimewafikia walengwwa, imebainika.
Drogba.jpg

Taasisi hiyo inayosaidiwa pia na Princess Beatrice na David Beckham inachunguzwa. Wachangiaji wakiwemo Bono, Frank Lampard na Christine Bleakley, waliambiwa kuwa fedha hizo zingetumika kujenga hospitali na kuwapa elimu watoto maskini nchini Ivory Coast.

Lakini Mail Online imeripoti kuwa ni £14,115 tu ndizo zilizowafikia walengwa. £439,321 zilitumika kuandaa hafla ya kifahari ya uchangiaji iliyopambwa na burudani za muziki kutoka kwa wasanii wakubwa.

Mastaa wengine wanaoisaidia taasisi hiyo ni pamoja na Pele, John Terry, Roger Federer na Donna Air, girlfriend wa kaka yake na Duchess of Cambridge, James. Mmiliki wa Chelsea, Roman Abramovich naye alidaiwa kuchangia kiasi kikubwa cha fedha.

Pia kuna maswali kuhusu fedha za udhamini kutoka kwa makampuni kama Pepsi, Nike ma Samsung, ambazo Drogba alidai zimeenda kwenye charity.

Taasisi hiyo inayosaidiwa pia na Princess Beatrice na David Beckham inachunguzwa. Wachangiaji wakiwemo Bono, Frank Lampard na Christine Bleakley, waliambiwa kuwa fedha hizo zingetumika kujenga hospitali na kuwapa elimu watoto maskini nchini Ivory Coast.

Lakini Mail Online imeripoti kuwa ni £14,115 tu ndizo zilizowafikia walengwa. £439,321 zilitumika kuandaa hafla ya kifahari ya uchangiaji iliyopambwa na burudani za muziki kutoka kwa wasanii wakubwa.

Mastaa wengine wanaoisaidia taasisi hiyo ni pamoja na Pele, John Terry, Roger Federer na Donna Air, girlfriend wa kaka yake na Duchess of Cambridge, James. Mmiliki wa Chelsea, Roman Abramovich naye alidaiwa kuchangia kiasi kikubwa cha fedha.

Footballer Drogba's charity and £1.7m that's not reached sick Africans
 
Afrika ni moja.

Viongozi wetu ni taswira ya sisi tulivyo.

Hata kwa Drogba sishangai.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom