Taarifa Muhimu: Rais Magufuli alishukuru Bunge

Nami naungana na Mh. Rais kulipongeza Bunge letu tukufu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutekeleza wajibu wake kwa 100%.
 
Kuna kiongozi mmoja wa nchi ya mashariki ya mbali alikua anapenda sana kusifiwa hata akifanya majukumu yake tu ya kawaida!
 
Bunge linashirikiana na rais kuficha ufisadi ulioibuliwa na CAG, bunge linakubali rais atumie pesa za umma nje ya budget iliyopitishwa na wawakilishi wa wananchi, bunge limechafuka wajibu wa kuisimamia serikali bali limekubali kusimamiwa na rais, kifupi ni bunge dhaifu kuwahi kutokea, spika dhaifu kiafya na kiakili
 
Novemba 5 Bunge kwa kauli moja lilimpongeza Mh Rais J. P. Magufuli kwa kupokea Uwenyekiti wa Nchi za SADC, halafu kwa nafasi ya Spika kama Spika alimpongeza kwa kuongeza nchi Salama na Amani. Sasa Mh Rais John Pombe Magufuli naye anamshukuru Spika J. Ndugai na Bunge kwa kumpongeza.

Nahisi Bunge lijalo Februari 2020 Bunge tena litampongeza tena Mh Rais J. P. Magufuli kwa kuwapongeza.
 
Hahaha haiwezi kuwa Bongo. Itakua nchi nyingine
Kuna nchi fulani ya Afrika nimeona kwenye taarifa ya habari ya jana jioni kuwa Rais wake ameiweka mihimili yote mitatu mfukoni kwake nikashangaa sana!
 
Hakika tunamepata Rais

Mungu aendelee kukupa afya njema ili uwatumikie Watanzania
 
Duh.Sio kwa maneno hayo.
 
Pale Rais na serikali wanapoungana kumchunguza CAG. Only in a certain particular country East Africa
 
Mkuu ungeona Jana wakati hili bunge dhaifu linafanya hicho kinachoitwa Azimio la kumpongeza rais ungelia sana.Yani hovyo kabisa kabisa kabisa.Watanzania wote wana safari ndefu sn
Habari zingine ni kichefuchefu nisingefungua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…