Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,242
- 34,903
04/03/2017
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI JUU YA UNYANYASAJI NA UDHALILISHWAJI WA MADAKTARI NCHINI.
Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) ni chama cha kitaaluma cha Madaktari wa binadamu kilicho anzishwa mwaka 1965 kwa madhumuni ya kuendeleza na kuwalea wanataaluma kimaadili na ueledi wa kitaaluma na kusimamia taaluma ya udaktari nchini Tanzania. Hivyo basi chama hiki kinajukumu la kuwasimamia kwa kushirikiana na Baraza la Madaktari Tanganyika katika kutoa huduma iliyotukuka kama inavyokusudiwa na jamii.
MAT na Madaktari kwa ujumla wamepokea kwa masikitiko matukio mbalimbali ya Madaktari na wafanyakazi wengine wa afya kunyanyaswa na viongozi mbalimbali nchini, ikiwemo kuwekawa ndani(lockup) kwa baadhi ya Waganga Wakuu wa Wilaya hapa nchini.
Imeonekana kama viongozi wengi hasa wakuu wa wilaya na mikoa wanatoa matamko ambayo kwa namna moja ni ya kuwadhalilisha madaktari na wahudumu wa afya, MAT ambacho ni chama kinachosimamia maadili na ueledi wa wanataaluma nchini TUNASIKITISWA SANA KWA VITENDO HIVI NA HATUTAKUBALINA NA UONEVU HUU HATA KIDOGO.
Tukio la lililosikitisha la hivi karibuni ni lile ya Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Bwana Christopher Emil Ngumbiagai ambapo mbele ya wafanyakazi na kamera za wandishi wa habari alimuamuru OCD kumuweka ndani (lock up) Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Dr. Vitalis Katalyeba, sababu ikiwa hakuwa na barua ya kusimamishwa kazi.
Ambapo kitaratibu inafahamika Mkurugenzi wa wilaya ndiye aliyepaswa kumpa Mkuu wa wilaya barua ya kumsimamisha kazi Daktari. Kwanini Daktari awekwe ndani kwa kosa lisilo lake, na kwanini isiwe Mkurugenzi ndio akamatwe na kuwekwa ndani?!!
Tukio lingine lilitokea Singida vijiji ambapo mkuu wa mkoa wa Singida Dr. Rehema Nchimbi alimuweka ndani (lock up)_ Mganga Mkuu wa Wilaya ya Singida mjini Dr. Erick Bakuza. Pamoja na kuwa kulikuwa na mapungufu ya kiutendaji, haikuwa sahihi hata kidogo kumuweka lock up mganga mkuu wa wilaya ila taratibu za kinidhamu zilitakiwa kufuatwa.
Tukio la tatu linamhusu Mganga Mkuu wa a wilaya ya Monduli na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Ndugu Mrisho Gambo ambaye alimtaka mganga mkuu wa wilaya ya Monduli kutoa maelezo ya juu ya malipo ya malimbikizo mbalimbali ya stahiki za watumishi wa afya pamoja ucheleweshwaji wa kupandishwa vyeo/madaraja kwa watumishi wa afya huku akijua siyo jukumu la mganga mkuu wa wilaya.
WITO
Udhalilisha huu USITISHWE mara moja nchi nzima.
Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Bwana Christopher Emil Ngumbiagai ajitathmini mwenyewe kabla hatujamchukulia hatua kwa udhalilishaji alioufanya. Tunawataka madaktari wote nchini kutompa ushirikiano Bwana Christopher Emil Ngumbiagai kwa sababu ni adui wa taaluma ya udaktari nchini na adui wa maendeleo ya afya wa watanzania.
Hatutavumilia tena uonevu na udhalilishaji wa madaktari kama huu, tutachukua hatua stahiki ya kulinda taaluma yetu ambayo inaheshimika ulimwenguni kote kwa manufaa ya umma.
Serikali itekeleze wajibu wake wa kulipa stahiki za watumishi wa afya pamoja na kuwapandisha vyeo/ madaraja watumishi wa afya na kuacha kuwasingizia waganga wakuu wa wilaya kwenye majukumu yasiyo yao pale inaposhindwa kutekeleza wajibu wake.
Tararatibu za kiutumishi na utawala zifuatwe pindi panapoonekana kuna changamoto katika utendaji au ufanyaji kazi katika sekta ya afya.
Pamoja na mambo mengine tunamtaka Waziri wa Afya maendeleo ya jamii, jinsi, wazee na watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu kuwasilisha Muswaada wa Madaktari, Madaktari wa Meno na wanataalamu shirikishi wa afya Bungeni kwenye Bunge lijalo hata ikibidi kwa hati ya dharula
Kwa kuwa muswada huo una manufaa makubwa ya kuilinda jamii inayohudumiwa na wataalamu wa afya. Pia Muswada huo utaleta dhana ya uwajibikaji na weledi kupitia elimu endelevu na kuboresha utoaji huduma za afya nchini. MAT pamoja na wadau wengine wa afya hatukubaliani na ucheleweshaji wa muswada huu.
MAT tunaiomba serikali kutoa kibali cha ajira kwa madaktari wenye sifa takribani 1794(elfu moja mia saba tisini na nne) ambao wapo mtaani bila ajira kwa kuzingatia uhitaji wa Mikoa hasa ile yenye uhaba mkubwa wa madaktari.
Katika kuzingatia uadilifu na huduma bora ya afya kutoka kwa Madaktari Tanzania, MAT tunaunga mkono tamko la chama kikuu cha wafanyakazi TUCTA la kupinga makato ya asilimia 15% ya mishahara ya baadhi ya wafanyakazi wanaodaiwa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya juu.
Tunawaomba na kuwasihi madaktari kote Nchini kuendelea kufanya kazi kwa mujibu ya maadili na miiko ya kidaktari ili kutoa huduma bora kwa wagojwa.
IMETOLEWA NA CHAMA CHA MADAKTARI TANZANIA – MAT
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI JUU YA UNYANYASAJI NA UDHALILISHWAJI WA MADAKTARI NCHINI.
Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) ni chama cha kitaaluma cha Madaktari wa binadamu kilicho anzishwa mwaka 1965 kwa madhumuni ya kuendeleza na kuwalea wanataaluma kimaadili na ueledi wa kitaaluma na kusimamia taaluma ya udaktari nchini Tanzania. Hivyo basi chama hiki kinajukumu la kuwasimamia kwa kushirikiana na Baraza la Madaktari Tanganyika katika kutoa huduma iliyotukuka kama inavyokusudiwa na jamii.
MAT na Madaktari kwa ujumla wamepokea kwa masikitiko matukio mbalimbali ya Madaktari na wafanyakazi wengine wa afya kunyanyaswa na viongozi mbalimbali nchini, ikiwemo kuwekawa ndani(lockup) kwa baadhi ya Waganga Wakuu wa Wilaya hapa nchini.
Imeonekana kama viongozi wengi hasa wakuu wa wilaya na mikoa wanatoa matamko ambayo kwa namna moja ni ya kuwadhalilisha madaktari na wahudumu wa afya, MAT ambacho ni chama kinachosimamia maadili na ueledi wa wanataaluma nchini TUNASIKITISWA SANA KWA VITENDO HIVI NA HATUTAKUBALINA NA UONEVU HUU HATA KIDOGO.
Tukio la lililosikitisha la hivi karibuni ni lile ya Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Bwana Christopher Emil Ngumbiagai ambapo mbele ya wafanyakazi na kamera za wandishi wa habari alimuamuru OCD kumuweka ndani (lock up) Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Dr. Vitalis Katalyeba, sababu ikiwa hakuwa na barua ya kusimamishwa kazi.
Ambapo kitaratibu inafahamika Mkurugenzi wa wilaya ndiye aliyepaswa kumpa Mkuu wa wilaya barua ya kumsimamisha kazi Daktari. Kwanini Daktari awekwe ndani kwa kosa lisilo lake, na kwanini isiwe Mkurugenzi ndio akamatwe na kuwekwa ndani?!!
Tukio lingine lilitokea Singida vijiji ambapo mkuu wa mkoa wa Singida Dr. Rehema Nchimbi alimuweka ndani (lock up)_ Mganga Mkuu wa Wilaya ya Singida mjini Dr. Erick Bakuza. Pamoja na kuwa kulikuwa na mapungufu ya kiutendaji, haikuwa sahihi hata kidogo kumuweka lock up mganga mkuu wa wilaya ila taratibu za kinidhamu zilitakiwa kufuatwa.
Tukio la tatu linamhusu Mganga Mkuu wa a wilaya ya Monduli na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Ndugu Mrisho Gambo ambaye alimtaka mganga mkuu wa wilaya ya Monduli kutoa maelezo ya juu ya malipo ya malimbikizo mbalimbali ya stahiki za watumishi wa afya pamoja ucheleweshwaji wa kupandishwa vyeo/madaraja kwa watumishi wa afya huku akijua siyo jukumu la mganga mkuu wa wilaya.
WITO
Udhalilisha huu USITISHWE mara moja nchi nzima.
Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Bwana Christopher Emil Ngumbiagai ajitathmini mwenyewe kabla hatujamchukulia hatua kwa udhalilishaji alioufanya. Tunawataka madaktari wote nchini kutompa ushirikiano Bwana Christopher Emil Ngumbiagai kwa sababu ni adui wa taaluma ya udaktari nchini na adui wa maendeleo ya afya wa watanzania.
Hatutavumilia tena uonevu na udhalilishaji wa madaktari kama huu, tutachukua hatua stahiki ya kulinda taaluma yetu ambayo inaheshimika ulimwenguni kote kwa manufaa ya umma.
Serikali itekeleze wajibu wake wa kulipa stahiki za watumishi wa afya pamoja na kuwapandisha vyeo/ madaraja watumishi wa afya na kuacha kuwasingizia waganga wakuu wa wilaya kwenye majukumu yasiyo yao pale inaposhindwa kutekeleza wajibu wake.
Tararatibu za kiutumishi na utawala zifuatwe pindi panapoonekana kuna changamoto katika utendaji au ufanyaji kazi katika sekta ya afya.
Pamoja na mambo mengine tunamtaka Waziri wa Afya maendeleo ya jamii, jinsi, wazee na watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu kuwasilisha Muswaada wa Madaktari, Madaktari wa Meno na wanataalamu shirikishi wa afya Bungeni kwenye Bunge lijalo hata ikibidi kwa hati ya dharula
Kwa kuwa muswada huo una manufaa makubwa ya kuilinda jamii inayohudumiwa na wataalamu wa afya. Pia Muswada huo utaleta dhana ya uwajibikaji na weledi kupitia elimu endelevu na kuboresha utoaji huduma za afya nchini. MAT pamoja na wadau wengine wa afya hatukubaliani na ucheleweshaji wa muswada huu.
MAT tunaiomba serikali kutoa kibali cha ajira kwa madaktari wenye sifa takribani 1794(elfu moja mia saba tisini na nne) ambao wapo mtaani bila ajira kwa kuzingatia uhitaji wa Mikoa hasa ile yenye uhaba mkubwa wa madaktari.
Katika kuzingatia uadilifu na huduma bora ya afya kutoka kwa Madaktari Tanzania, MAT tunaunga mkono tamko la chama kikuu cha wafanyakazi TUCTA la kupinga makato ya asilimia 15% ya mishahara ya baadhi ya wafanyakazi wanaodaiwa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya juu.
Tunawaomba na kuwasihi madaktari kote Nchini kuendelea kufanya kazi kwa mujibu ya maadili na miiko ya kidaktari ili kutoa huduma bora kwa wagojwa.
IMETOLEWA NA CHAMA CHA MADAKTARI TANZANIA – MAT