Taarifa kwa umma


Tunawaomba wakazi wa Arusha na wanachama wetu wote waendelee kudumisha utulivu, umoja na amani vitu ambavyo ndivyo hasa tabia yetu na kamwe tusishiriki katika vurugu na tusiharibu mahusiano yetu na jeshi la polisi ambao tunawatarajia watafanya kazi zao kwa haki. Wakazi wa Arusha tufanye kazi na tujitume kwa bidii kwa maendeleo ya jimbo letu.
Mungu Ibariki Arusha, Mungu Ibariki Tanzania.

Amani Golugwa

KATIBU WA CHAMA MKOA – ARUSHA.

[/QUOTE]

Kwa style hii namshangaa kila mmoja anaeamini kuwa jeshi la polisi hili la ccm linaweza kubadilika na kutenda haki kwa hapo siwaungi mkono na mmepotoka.
Binafsi nilitegemea sana muwahimize wananchi kuitafuta haki yao kwa njia yoyote ambayo haivunji sheria na kwa hatua iliyofikia sasa ni bora wananchi waambiwe waifuate haki mitaani na tuone kama watatuua wote, jamani tuacheni kudhani kuwa ccm inaweza kusaidia watu wapate haki zao huo ni upungufu wa fikra (UWF), jeshi la polisi liko kwa ajili ya watawala na si raia sasa tuamke na tuifuate haki ilipo ni lazima tukubali kujeruhiwa ili hata kama italazimu kufa basi historia ya taifa hili itaandikwa upya na haitatuacha sisi.
 
Hakuna chenye mwanzo kisicho na mwisho na mwisho wa ubaya ni fedhea. So wana cdm 2endelee 2 kumlilia mungu one day wote waliofanywa vipofu na ccm wataona kisha watajuta na kuangua vilio kwani hawataamini kama wao ndio waliokua wakitenda ubaya wote waliotenda. May our lord stand with us up to the last point 2ckate tamaa wala 2cogope.
 
Umeongea kiingereza kigumu kiasi sijaelewa umeongea nini. Hizi lugha za watu ni wito.

Mwita mimi naamini wewe ni mwerevu uliyezidi kiwango cha wastani na ambaye unatambua kuwa lugha za watu wengine ukiweza kuzizungumza na kuziandika kisanifu ni heri kwako lakini kwa namna yoyote ile akili pevu hujaribu kuelewa wazo linalobebwa na maneno aliyotumia mwandishi.
Wakati mwingine mimi nimewahi kupata shida sana kuunganisha jargons zako ili kupata ujumbe uliokusudia na nilifanya hivyo kwa shida sana lakini sijawahi kukulaumu kwa sababu najua wakati fulani inawezekana wakati unaandika maneno unayaacha kichwani mwako. Great thinkers of which i guess you belong look at the concept and forget about gramatical errors. Let us learn to be objective in approaching other pepoles' views and work so as as to remain connected as great thinkers by concept and not by well versed essays though if it happens makes communication more perfect. Any attempt to revile other people by evaluating the connectivity of used words and grammar is to create a fear to section of the JF who want to communicate but they are masters of no language.


WASALIMIE WENGINE WANAOFANANA NA WEWE KATIKA KUCHAMBUA KAZI ZA WENGINE
 

Nguvu ya umma ya wabunge 23?
 
Kwani lazima uandike kiingereza? au ndio tayari? maana wengine Kiingereza hupanda pale tu wanapokuwa ya 5.

Ninyi ndio mnaorudisha nyuma maendeleo ya watu kutumia lugha wanazojifunza. Amejifunza kiinglish, sasa atatumia wapi kama si hapa? Mbona hatushangai na kuwacheka wahindi kusema bana badala ya bwana? Wazungu wangevunjika mbavu tunavyoharibu lugha yao, lakini wako wavumilivu na waelewa. Kwani alichoongea hujakielewa? Na hapa wengi wanaandika haraka wakiwa katika shughuli zao, na mara nyingi hawana nafasi ya kutumia tools kuhakiki system ya mjengo wa english structure hali kadhalika spelling mimi nikiwa mmoja wapo. Wengi hapa wanaandika mada au kuchangia wakiwa safarini, kazini muda unapowaruhusu wakati wakisubiria karabasha la kazi. We angalia maudhuri yaliyoletwa, maana hili si jukwaa la uchambuzi wa lugha bali ni jukwaa la kujadili mambo ya siasa. Mambo haya ndiyo yanayotujengea watanzania tabia ya kukosa kuvumiliana katika mambo madogo kisha kuyakuza kuwa makubwa na makubwa yakutisha kuyaogopa kwa sababu kasumba ya hewala hewala, aka utwa na utwana. Mpaka wengi tufikie hali ya kujikomboa kifikra ipo patashika ya nguo kuchanika.
 
Ujasiri huu wa Lema ni wa mfano na wa kuigwa.Tummunge mkono tuikomboe nchi yetu.
 
huyu OCD kama anabusara NZURI za kiukweli anapaswa kuwaomba msamaha RAIA aidha mamlaka ya juu yake imhamishe kwani Jeshi la polisi kwa sasa linategemea sana ulinzi shirikishi na polisi jamii kwa hali hii kazi itakuwa ngumu sana kushirikiana na PANYA
 
Kwani lazima uandike kiingereza? au ndio tayari? maana wengine Kiingereza hupanda pale tu wanapokuwa ya 5.

Nadhani wewe ndio huji Kiingereza na hasa Lugha yoyote ya mawasiliano huna, ndio maana badala ya kujadili hoja iliopo unaleta ya kwako ya kujifanya mtaalam wa Lugha angali hujui lolote wala chochote.
 
Waraka huu unapaswa kusambazwa kwa kadri muwezavyo Arusha pana na vitongoji vyake labda pia ukasomwe kwenye hizo FMs za Arusha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…