Noti mpya tz
JF-Expert Member
- Mar 23, 2011
- 974
- 247
Tunawaomba wakazi wa Arusha na wanachama wetu wote waendelee kudumisha utulivu, umoja na amani vitu ambavyo ndivyo hasa tabia yetu na kamwe tusishiriki katika vurugu na tusiharibu mahusiano yetu na jeshi la polisi ambao tunawatarajia watafanya kazi zao kwa haki. Wakazi wa Arusha tufanye kazi na tujitume kwa bidii kwa maendeleo ya jimbo letu.
Mungu Ibariki Arusha, Mungu Ibariki Tanzania.
Amani Golugwa
KATIBU WA CHAMA MKOA ARUSHA.
Mungu Ibariki Arusha, Mungu Ibariki Tanzania.
Amani Golugwa
KATIBU WA CHAMA MKOA ARUSHA.
Kwa style hii namshangaa kila mmoja anaeamini kuwa jeshi la polisi hili la ccm linaweza kubadilika na kutenda haki kwa hapo siwaungi mkono na mmepotoka.
Binafsi nilitegemea sana muwahimize wananchi kuitafuta haki yao kwa njia yoyote ambayo haivunji sheria na kwa hatua iliyofikia sasa ni bora wananchi waambiwe waifuate haki mitaani na tuone kama watatuua wote, jamani tuacheni kudhani kuwa ccm inaweza kusaidia watu wapate haki zao huo ni upungufu wa fikra (UWF), jeshi la polisi liko kwa ajili ya watawala na si raia sasa tuamke na tuifuate haki ilipo ni lazima tukubali kujeruhiwa ili hata kama italazimu kufa basi historia ya taifa hili itaandikwa upya na haitatuacha sisi.