Nitakumegea kiduchu tu. Marekani ni nchi iliyogawanyika kiitikadi, kiutamaduni na kisiasa vile vile. Kuna majimbo ambayo daima yanapiga kura Republican, kama vile Kansas, Missouri, Nebraska, na kuna majimbo ambayo daima yanapiga kura Democratic, kama vile New York, California, Connecticutt, etc. Sasa swing states ni majmbo ambayo yanapiga kura kufuatana na ushabiki wa mgombea, anaweza kuwa Republican au Democrat, lakini amewakonga nyoyo wapiga kura katika majimbo hayo. Kwa mwaka huu hayo ni pamoja na Colorado, Ohio, Virginia, ambalo kwa muda mrefu lilikuwa Republican, Florida, Wisconsin, Minnesota na New Hampshire. Huko ndiko kura zinapogombaniwa hivi sasa kuelekea uchaguzi wa wiki ijayo na ndio maana unaona Romney na timu yake na Obama na timu yake wanazungukia hayo majimbo kwa sababu wanajua katika yale majimbo mengine wanaongoza kwenye kura ya maoni.
Early voting ni ruhusa ya kupiga kura mapema kabla ya siku ya uchaguzi, ambayo kwa mujibu wa katiba ni lazima iwe jumanne ya kwanza ya mwezi Novemba. Majimbo kadha wa kadhaa huruhusu early voting ili kupunguza msongamano siku ya upigaji kura. Kuhusu electoral college ni idadi ya kura alizopata mgombea kutokana na ushindi wa jimbo kwa jimbo. Kila jimbo lina idadi yake ya electoral votes kutokana na idadi ya watu. Kwa kifupi ni hivyo.