Swali kwa Wazazi

Swali kwa Wazazi

Kwa kusema hilo, mtoto anakuwa amekuambia vingi;

1. Hajiamini na anajihukumu sana.

2. Bado hajajenga maisha yake ya kijamii. Hajajitambua, anapata shinikizo kubwa la kuiga maisha ya watu ili akubalike.

Kwanza mzazi unatakiwa uweke juhudi kwenye kutambua ni vitu gani vinamfurahisha mwanao iwe ni michezo, dini nk. na umpe motisha.

Pili, kaa naye umtulize na umueleze kuwa ni sawa tu, hakuna mashindano kwenye hayo mambo. Atafanya pale atakapokuwa tayari.

Mimi sio mzazi lakini.
 
Nitaongea nae ili ajue thamani yake au uanaume wake haupungui kwa kigezo cha kwamba hajawahi kushiriki hilo tendo. Pia nitamuonesha picha za wagonjwa wa magonjwa ya ngono ili ajue akiingia huko hicho ndo anachokitafuta maana kwa umri wa vijana wadogo kuchukua tahadhari kujikinga hamnaga na pia kuna magonjwa ambayo kondomu haizuii.
Nikiona haelewi nitamtafutia mwanasaikolojia amueleweshe maana wao wana utaalamu zaidi bila kusahau kushushia mistari ya Biblia inayokataza zinaa na uasherati.
 
Nitamwambia asifuate maneno ya watu, asubiri muda wake angalau akiwa 18+.... Lakini pia nitampa elimu ya ngono salama. Maana mtoto hata umkanye itafika siku atajaribu tu mwenyewe, cha muhimu apatiwe elimu sahihi.
 
Back
Top Bottom