QUALITY
JF-Expert Member
- Sep 27, 2010
- 853
- 115
Kila mwaka kuanzia mwezi Juni hadi August Bunge letu hukaa dodoma kwa kiasi cha siku zisizopungua sitini huku wakijadili makadirio ya mapato na matumizi na kupitisha makadilio hayo kuwa bajeti ya serikali katika wizara mbalimbali. katika vikao hivyo, tunaona sura za kisiasa na chuki dhidi ya vyama vingine na wakati mwingine mtu (mbunge) kushambuliwa binafsi. Tunaona taswira ya upendeleo kwa chama fulani kutoka kwa spika au naibu wake, mawaziri na kadharika.
Pamoja na kuwa wabunge hujadili kwa hisia sana wakati mwingine hata kuapa kuwa bajeti haitapita, wengi wao hasa wa CCM huishia kusema naunga mkono mia kwa mia. wengine kabla ya kuanza kuongea anasema "kwanza kabisa niseme kuwa naunga mkono hoja" kisha anaanza kujimwaga... hana jipya.
Swali, Tangu bajeti ya kwanza inapowasiliswa mpaka ya mwisho, ni kwa kiasi gani michango na hoja za wabunge huchukuliwa maanani na kusababisha badiliko katika hizo bajeti zinazopitishwa?
Asilimia ngapi inayoongezeka kwenye bajeti ya wizara fulani au kupungua ikiwa ni matokeo ya majadiliano hayo na ya Bunge?
Nawasilisha
Pamoja na kuwa wabunge hujadili kwa hisia sana wakati mwingine hata kuapa kuwa bajeti haitapita, wengi wao hasa wa CCM huishia kusema naunga mkono mia kwa mia. wengine kabla ya kuanza kuongea anasema "kwanza kabisa niseme kuwa naunga mkono hoja" kisha anaanza kujimwaga... hana jipya.
Swali, Tangu bajeti ya kwanza inapowasiliswa mpaka ya mwisho, ni kwa kiasi gani michango na hoja za wabunge huchukuliwa maanani na kusababisha badiliko katika hizo bajeti zinazopitishwa?
Asilimia ngapi inayoongezeka kwenye bajeti ya wizara fulani au kupungua ikiwa ni matokeo ya majadiliano hayo na ya Bunge?
Nawasilisha