Star TV mnaboa

ishobo

Member
Joined
Jan 3, 2014
Posts
16
Reaction score
10
Hivi star tv hamna watangazaji au ni ukiritimba wa hii mizee? Jitu lina mapengo meno yameng'oka eti ndo presenter wa habari!!! Hivi nyie si ndio wataalam wa PR au? Achaneni na huyo kibogoyo Jacob Marcus.

Nawasilisha
 
Acha chuki zisizo na msingi wewe kama huna kazi tafuta na wewe utapata...by the way sio mapengo ni mwanya na hata kama ni mapengo mungu ndiokaamua awe hivyo sasa hali hiyo wewe inakukera nini? Mitanzania yani kila kukicha ni wivu usio na maana.
 
Hivi wewe ishobo Mapengo yangu na utangazaji wangu unakuhusu nini? Chamsingi tizama taarifa ya habari upite alaaah!
 
Last edited by a moderator:
Huyu Ishobo anashobokea pengo hilo atashikwa ta...kkoo
 
Acha chuki zisizo na msingi wewe kama huna kazi tafuta na wewe utapata...by the way sio mapengo ni mwanya na hata kama ni mapengo mungu ndiokaamua awe hivyo sasa hali hiyo wewe inakukera nini? Mitanzania yani kila kukicha ni wivu usio na maana.

Tukienda Kitaaluma Jacob Marcus Hapashwi Kuwa Tv Anchor Na Kubwa Zaidi Huo Mwanya Wake Na Kuna Mwingine Nae Ni Mdada Yupo TBC1 Nae Hafai Kutangaza Kwani Ana Kigugumizi ILA Ki Bongo Bongo Wanapeta Tu Na Ndiyo Maana Hata Runinga Za Kitanzania Ni Takataka Kwa Runinga Za Wenzetu Tena Hawa Wa Karibu Tu Kenya, Uganda Na Rwanda.
 
alaaaa kumbe ishobo mbaguzi jinsi hiyo????
Hivi star tv hamna watangazaji au ni ukiritimba wa hii mizee? Jitu lina mapengo meno yameng'oka eti ndo presenter wa habari!!! Hivi nyie si ndio wataalam wa PR au? Achaneni na huyo kibogoyo Jacob Marcus.

Nawasilisha
 
media zetu hasa tv bado sana...tatizo kujuana.
 
Sura huwa hainipi matatizo kinachonipa matatizo kinachosemwa na mleta habari...mleta habari huyo umsemaye alipata aibu ya mwaka kwa kusema sema hovyo kwa mtindo wa mashabi wa kibongo bongo, enzi za Maximo wa Taifa Stars. Kipindi hicho Maximo alikuwa ameshikia kidedea nidhani ya wachezaji ndani ya timu...kutokana na nidhamu mbovu ya wachezaji wazoefu, Maximo aliamua kuwatema na kuchukuwa wachezaji wasio na majina na kuipeleka timu kwenye pambano la kiushidani huko Africa magharibi (nchi sikumbuki vizuri ni hipi).

Basi huku nyuma mleta habari huyo...aanza kumkashfu na kumkebehi Maximo kupitia vipindi vya michezo vya Star TV kwa kushirikiana na watangazaji na waandishi makanjanja wa habari za Michezo.....Kikosi cha maximo kilishida mechi ya Ugenini 1-0 nina kumbuka vizuri sana .....kwa aibu kubwa Star TV hawakumpa jukwaa tena kwenye masuala ya michezo karibu miezi sita.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…