Stan Bakora ajibu mapigo

worldboss

JF-Expert Member
Jun 30, 2015
2,225
2,287
Mchekeshaji maarufu Stan Bakora amefunguka juu ya povu
lililomtoka Barakah The Prince siku kadhaa baada ya
kuachia parody ya wimbo ‘Nisamehe’.
Kupitia kipindi cha Friday Night Live cha EATV, Stan
amesema kuwa kama asingefanya vile video ingekuwa ya
kawaida tu na isingeleta maana.
Barakah ameshindwa kuelewa. Kama nisingefanya vile ile
video isingeleta maana, lazima uonyeshe uhalisia. Kwani
Baraka si mweusi kweli?,” amesema Stan. Stan aliendelea
kwa kumtania Barakah kwa kumwambia kuwa hapa mjini
[Dar es Salaam] ndio kwanza ana Christmas mbili.
Awali baada ya Stan kuachia parody hiyo, Barakah aliandika
kwenye Instagram: Matani ni mazuri ila yakizidi yanaweza
kuleta matatizo… heshima ichukue nafasi yake tafadhali
mzee utani huu sijaupenda iwe mwanzo na mwisho
tafadhali.”
 
Hahahaha! Eti ana krismasi mbili ,kweli jamaa ni mchekeshaji aisee! Hebu mwenye picha yake aiweke hapa tumuone.
 
Baraka hana akili saaana.
Nenda kaangalie kina Bart Baker na Alphacat, hawa ni makomedian wakimarekani wanafanya parody za wanamuziki za kuwazalilosha na kuwakashifu kabisa..
Lakini watu kimya. Ila mtu mmoja mweusi achukia kuectiwa mweusi watu weusi bana....
 
Back
Top Bottom