Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,346
- 26,138
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai yuko nchini India kwa matibabu ingawa haijulikani yuko hospitali gani na kwa muda gani sasa. Katibu wa Bunge, Dr. Thomas Kashililah amesema kuwa Spika Ndugai amekwenda nje ya nchi kwa ajili ya uchunguzi wa afya yake bila ya kusema amekwenda nchi gani wala ugonjwa unaomsumbua. Amesema kuwa Spika haumwi sana.
Lakini Balozi wa Tanzania nchini India, John Kijazi amekiri kuwa Spika Ndugai uko India kwa matibabu na anaendelea vizuri. Kimsingi, Ofisi ya Bunge imedai kuwa Spika yuko nje ya nchi kwa uchunguzi wa kiafya wakati Ubalozi umesema kuwa Spika yuko India kwa matibabu.
Chanzo: Mwananchi la leo, uk. 3
Lakini Balozi wa Tanzania nchini India, John Kijazi amekiri kuwa Spika Ndugai uko India kwa matibabu na anaendelea vizuri. Kimsingi, Ofisi ya Bunge imedai kuwa Spika yuko nje ya nchi kwa uchunguzi wa kiafya wakati Ubalozi umesema kuwa Spika yuko India kwa matibabu.
Chanzo: Mwananchi la leo, uk. 3