Na hiyo ni maeneo mengi sana ya Tanzania mkuu sio machache
Vijijini hali inatisha ila hao viongozi wetu wanapambana kuunda tume za kilaji kila siku huku matokeo ya tume hizo wakiwa hawayapendi wala hawayafanyii kazi zaidi ya kuwatukana walioteuliwa na wao wenyewe
Ni hatari sana mkuu BAK
BAK hapa wewe unasemaje au uko upande gani au unataka kubaki upande wa Mzee Mwanakijiji unajiuliza na wewe nani mmiliki wa UDA
Sasa kama bunge halijui nani mmiliki wa uda na wao wanapaswa kusimamia serekali hii inatupa picha gani.
Ndiyo hivyo Mkuu Mr Rocky na MACCM AKA #Maintarahamwe yamedhamiria kubaki madarakani milele kwa kutumia kitengo chao cha vyombo vya dola, miaka mingine 52 Taifa letu litastahili kuitwa Taifa la Wapumbavu maana elimu yenyewe ndiyo hiyo inazidi kuporomoka kila mwaka.
Hivi ni kweli serikai ikitaka kujua kuwa kampuni flan inamilikiwa na nani, ni mpaka iundwe tume?
Mpaka 2015 sijui tutabakiwa na nini kama chetu.
Mkuu Mani Hapo ndio ujiulize nani mmiliki wa UDA mpaka bunge halijui
Mkuu Mr Rocky, fisadi Mkapa akishirikiana na Yona walijimilikisha Kiwira Coal Mining kiwiziwizi Wabunge hawakujua lolote walikuwa busy kubwabwaja mjengoni. Angalia mabilioni ya Uswiss mwezi ujao itakuwa ni mwaka wa pili tangu Serikali itangaze kwamba "uchunguzi unaendelea" na ufuatiliaji wa Wabunge kwenye hili ni SIFURI, na wahusika wameanza kuyachota mabilioni yale kwa fujo huku Serikali ikiwa kimyaaaa "inaendelea na uchunguzi" ikifikia mwisho wa 2015 si ajabu kusikia mabilioni hayo hayapo tena yameshayeyuka.
Hii nchi hii.....