Ta Muganyizi
R I P
- Oct 19, 2010
- 5,361
- 2,734
Huu Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) siuungi mkono maana nimeshtuka baada ya kufatilia wanachama wake. Kihistoria Umoja huo ulianzishwa enzi za TANU mpaka hivi sasa CCM na majukumu yao ni kulinda maslahi ya CCM. Kwa vile sasa tuko kwenye mfumo wa vyama vingi ni vizuri jina libadilike na kuwa UWCT yaani Umoja wa Wanawake wa CCM wa Tanzania au Umoja wa wanawake wa CCM basi. Swali najiuliza hivi watu kama Halima Mdee......au........Josephine Mushumbusi.......au mke wangu ambaye ni mwana CDM hastahili kuitwa mwamake wa Tanzania? Umoja huu unaweza kutumia jina hili kuwadanganya hata mataifa ya nje kuwa ni ya wanawake wote walioko Tanzania kumbe ni ya wanawake wa MAGAMBA!!!
Kwenye website ya CCM imeelezwa wazi kuwa
"Katiba ya Kwanza ya TANU (1964) ilitambua nafasi ya wanawake, "Kutakuwa na upande wa Wanawake katika Chama, Mwanamke akishaingia katika Chama papo hapo atakuwa amekwisha kuwa mwanachama kuwa upande wa wanawake …. Kila Tawi la Chama litakuwa na upande wa wanawake na litakuwa katika Chama chini ya Uongozi wa Halmashauri ya Tawi. Wanachama wanawake na wanaume wote watakuwa sawa". Sehemu ya Wanawake iliundwa katika TANU 1955 chini ya Uongozi wa Bibi Titi Mohamed.
Majukumu yaliyotekelezwa na Sehemu ya Wanawake yalikuwa:
(1) Kuhamasisha wanawake kujiunga na TANU;
(2) Kueneza TANU mijini na vijijini kwa njia ya kujitolea;
(3) Kulinda Viongozi wa TANU: Katika hali ya kulinda Chama dhidi ya maadui, wanawake walijipenyeza kwenye vyama vya siasa na vikundi vya upinzani.
(4) Kuimarisha TANU kifedha kupitia shughuli halali mbalimbali ikiwa ni pamoja na dansi.(my take : Ndio maana kampeni zote za Magamba midundiko na dansi muhimu, haikuanza leo maana ni sehemu ya kipato)
(5) Kuendeleza wanachama wanawake kijamii na kiuchumi. Wanawake walianzisha madarasa ya kushona na kufuma, elimu ya watu wazima, biashara ya maduka na migahawa na vikundi vya ushirika"
Ukitoa neno TANU liite sasa hivi CCM. Kwa hiyo wanawake wanaozungumziwa hapa ni wanawake wa Tanzania ila wale wa CCM. wale wote ambao ni wanawake kwenye vyama vya upinzani si wanawake wa Tanzania!!!!! Na kazi ya umoja wa wanawake wa sasa kama nilivyoweka RED hapo juu ni kudeal na maadui vikiwemo vikundi vya upinzani.
Itabidi iundwe tume ichunguze ione ma -proposal yenu huwa yanaandikwa vipi na kujitambulisha vipi kwa wafadhili wenu. Msijekuwa mnapata shavu kwa jina la wanawake wa Tanzania kumbe ni wa magamba tu. Nimeishtukia hii.
Kwa hiyo msisitizo wangu ni kuwa, Jina hilo libadilishwe ili itambulike kuwa hao ni wanawake wa CCM au Umoja huu uvunjwe na uundwe utakaoweza kuacommodate wanawake wote wa Tanzania kama inavyosomeka sasa. Nawasilisha.