Smile 4G LTE is No longer

Smile 4G LTE is No longer

MVUMBUZI

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2011
Posts
5,182
Reaction score
2,330
Nilipoanza kutumia Smile mwaka mmoja uliopita nilikuwa radhi kuweka hata shs laki moja kwa siku kwa sababu ilikuwa inalipa. Ilikuwa very fast na uki download hata video ya GB 2 ilikuwa haichukui dakika 5.

Nipo Arusha na kuanzia mwezi wa July mwishoni mtandao wa smile umekuwa chini kuliko ile tunaoyotumia maofisini . Sioni tena kama ni 4G LTE na wala siyo 3G kwani spidi ni ndogo na hata kufungua page ya website it takes years.

Nimeshakwenda ofisi ya smile mara tatu wakitoa majibu yale yale eti kuna interference. Hawa jamaa nahisi wamebana bandwidth bila kutuambia kwa sababu wazijuazo wao. Na hii ina implication kwenye market.

Ninaomba ambao hamjanunua Smile msipoteze muda kwani inakoelekea ni kukumalizia hela otherwise smile watuambie watarudisha lini $G LTE ile iliyokuwepo miezi sita iliyopita.

Uzoefu unaonionyesha masaa 14 kati ya 24 smile iko chini sana kiasi kwamba huwezi kuitumia hata kujibu email.
 
Thank you for the information, wanabana speed ni wahujumu na wanapaswa kishtakiwa. Mwaka jana verizon walishitakiwa marekani kwa sababu ya kubania speeed
 
Hizo laki ulizokuwa unaweka kwa siku kwanin usingeenda kwa ISP wa kueleweka wakakupa internet ya uhakika?
 
Mbona natumia kila siku speed powa. Angalia labda virus kwa computer au badilisha usb port
 
tumia Airtel OMG ina speek kubwa sana na haipungui iko konstant. Ila optimize modem yako uone speed ilivyo kali
 
Nimeshakwenda ofisi ya smile mara tatu wakitoa majibu yale yale eti kuna interference. Hawa jamaa nahisi wamebana bandwidth bila kutuambia kwa sababu wazijuazo wao. Na hii ina implication kwenye market.

Swala sio kubana bandwidth, hawa jamaa hawawezi sema ukweli ila ukweli ni kwamba wana infrastructure ndogo na idadi ya watu kuongezeka imewashinda kuhandle watu wengi kwa wakati mmoja, kuhandle watu wengi ni kazi sana inahitaji pesa ya kutosha, hizo ni sacrifices wanafanya la si hivyo wataingia loss, na wabongo wagumu kweli kutoa pesa
 
SMILE tuwaachie makampuni sisi wenye hela za mawazo tukomae na AIRTEL bando za chuo...2.GB kwa 1,000 TSHS.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom