Slaa apangua safu ya uongozi Chadema Mbeya

Slaa apangua safu ya uongozi Chadema Mbeya

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,361
Baraza Kuu la CHADEMA mkoani hapa limepangua safu ya uongozi wa juu wa mkoa kwa kuwateua viongozi wa muda watakaokiongoza chama hicho hadi Mei.
Kikao hicho kizito kilifanyika karibu usiku mzima chini ya usimamizi wa Dk. Slaa ambaye baadaye alitangaza safu mpya ya uongozi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Nzovwe mjini hapa.
Dk. Slaa alimtangaza Peter Mwamboneke kuwa kaimu mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Mbeya, nafasi ambayo ilikuwa wazi baada ya aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho Sambwee Shitambala kuhamia Chama cha Mapinduzi (CCM)
Diwani wa kata ya Forest katika halmashauri ya jiji la Mbeya, Boid Mwabulanga, alitangazwa kuwa kaimu katibu wa chama hicho akichukua nafasi ya Eddo Mwamalala Makata.
Dk. Slaa alimtaja Joseph Kasambala kuwa ameteuliwa kuwa Kaimu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana (BAVICHA) mkoa wa Mbeya, akichukua nafasi ya Exavery Mwalyembe.
Seleman Simbayanje ameteuliwa kuwa Kaimu Katibu wa Baraza la Wazee wakati Tamali Mbarasya alitagazwa kuwa mratibu wa wanawake wa chama hicho.
Juzi usiku Dk. Slaa ambaye ameambatana na Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa chama hicho, Wilfred Rwakatare, alihamia kwenye kikao cha Baraza la Chama hicho wilaya ya Mbeya Mjini, ambako baadhi ya wanachama walidai kwamba hawana imani na Mwenyekiti wa CHADEMA Mbeya Mjini, David Mwambigija, maarufu kwa jina la Mzee wa Upako.
Habari kutoka ndani ya mkutano huo zimeeleza kuwa wajumbe wa baraza hilo waliamua kumweka kando mzee wa upako na kisha kupiga kura ya kutokuwa na imani naye.
Kwa mujibu wa chanzo chetu kura zilizopigwa zilikuwa 231 na ni kura tano tu ndizo zilizomkataa Mwambigija huku kura 226 zikimkubali.
“Kura ya kutokuwa na imani na Mzee wa Upako ilifanyika lakini wajumbe wengi wameoyesha kumwamini na hivyo anaendelea na wadhifa wake,” kilisema chanzo chetu. Habari zimesema kuwa kufanyika kwa mabadiliko hayo, kutaongeza kasi zaidi ya utendaji kazi hasa kwa kuzingatia kuwa mwaka huu ni wa uchaguzi ndani ya chama hicho

SOURCE:TANZANIA DAIMA
 
huko ni kutapatapa baada ya mambo kuanza kuwashinda.na bado.someni na vyanzo vingine vya taarifa mjue ukweli sio mnasoma gazeti la mbowe tz daima pekee,mnakosa mengi.
 
huko ni kutapatapa baada ya mambo kuanza kuwashinda.na bado.someni na vyanzo vingine vya taarifa mjue ukweli sio mnasoma gazeti la mbowe tz daima pekee,mnakosa mengi.

Tuambie basi. Hilo gazeti lingine limesemaje?
 
hongereni kwa kufanya mabadiliko hayo mapema kabla chama hakijaumia
 
Baraza Kuu la CHADEMA mkoani hapa limepangua safu ya uongozi wa juu wa mkoa kwa kuwateua viongozi wa muda watakaokiongoza chama hicho hadi Mei.
Kikao hicho kizito kilifanyika karibu usiku mzima chini ya usimamizi wa Dk. Slaa ambaye baadaye alitangaza safu mpya ya uongozi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Nzovwe mjini hapa.
Dk. Slaa alimtangaza Peter Mwamboneke kuwa kaimu mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Mbeya, nafasi ambayo ilikuwa wazi baada ya aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho Sambwee Shitambala kuhamia Chama cha Mapinduzi (CCM)
Diwani wa kata ya Forest katika halmashauri ya jiji la Mbeya, Boid Mwabulanga, alitangazwa kuwa kaimu katibu wa chama hicho akichukua nafasi ya Eddo Mwamalala Makata.
Dk. Slaa alimtaja Joseph Kasambala kuwa ameteuliwa kuwa Kaimu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana (BAVICHA) mkoa wa Mbeya, akichukua nafasi ya Exavery Mwalyembe.
Seleman Simbayanje ameteuliwa kuwa Kaimu Katibu wa Baraza la Wazee wakati Tamali Mbarasya alitagazwa kuwa mratibu wa wanawake wa chama hicho.
Juzi usiku Dk. Slaa ambaye ameambatana na Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa chama hicho, Wilfred Rwakatare, alihamia kwenye kikao cha Baraza la Chama hicho wilaya ya Mbeya Mjini, ambako baadhi ya wanachama walidai kwamba hawana imani na Mwenyekiti wa CHADEMA Mbeya Mjini, David Mwambigija, maarufu kwa jina la Mzee wa Upako.
Habari kutoka ndani ya mkutano huo zimeeleza kuwa wajumbe wa baraza hilo waliamua kumweka kando mzee wa upako na kisha kupiga kura ya kutokuwa na imani naye.
Kwa mujibu wa chanzo chetu kura zilizopigwa zilikuwa 231 na ni kura tano tu ndizo zilizomkataa Mwambigija huku kura 226 zikimkubali.
"Kura ya kutokuwa na imani na Mzee wa Upako ilifanyika lakini wajumbe wengi wameoyesha kumwamini na hivyo anaendelea na wadhifa wake," kilisema chanzo chetu. Habari zimesema kuwa kufanyika kwa mabadiliko hayo, kutaongeza kasi zaidi ya utendaji kazi hasa kwa kuzingatia kuwa mwaka huu ni wa uchaguzi ndani ya chama hicho

SOURCE:TANZANIA DAIMA


Kumbe Rwekatare yupo hivi naona siku hizi amekuwa bubu kabisaaaaaaaaa.
 
huko ni kutapatapa baada ya mambo kuanza kuwashinda.na bado.someni na vyanzo vingine vya taarifa mjue ukweli sio mnasoma gazeti la mbowe tz daima pekee,mnakosa mengi.
Huna lolote zaidi ya unafiki tu unataka tukasome gazeti la uhuru?
 
huko ni kutapatapa baada ya mambo kuanza kuwashinda.na bado.someni na vyanzo vingine vya taarifa mjue ukweli sio mnasoma gazeti la mbowe tz daima pekee,mnakosa mengi.

pole ndugu yangu...
 
huko ni kutapatapa baada ya mambo kuanza kuwashinda.na bado.someni na vyanzo vingine vya taarifa mjue ukweli sio mnasoma gazeti la mbowe tz daima pekee,mnakosa mengi.
Unataka tusome 'UHURU'?!!!! Siwezikupoteza muda wangu kusoma gazeti la uhuru. nipo tayari ni-cost kusafiri kwenda Mbeya kufuatilia mwenyewe habari hizi kuliko kuzipata kupitia gazeti la uhuru.
 
Kumbe Slaa, yeye ndio anapanga viongozi kila sehemu hakuna uchaguzi wala nini zidumu fikra za Katibu Mkuu!
 
Kumbe Slaa, yeye ndio anapanga viongozi kila sehemu hakuna uchaguzi wala nini zidumu fikra za Katibu Mkuu!
Soma uelewe ndio uchangie co kukurupuka tu kama magamba wenzio.
Baraza Kuu la CHADEMA mkoani hapa limepangua safu ya uongozi wa juu wa mkoa kwa kuwateua viongozi wa muda watakaokiongoza chama hicho hadi mei. Kikao hicho kizito kilifanyika karibu usiku mzima chini ya usimamizi wa Dk. Slaa ambaye baadaye alitangaza safu mpya ya uongozi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Nzovwe mjini hapa.
 
Asante Mungu kumnyima Urais maana angekuwa anasindikizwa na ving`ora asingepata muda wa kukijenga chama ila 2015 tukichukua nchi chama kitakuwa kimeimarika
 
Asante Mungu kumnyima Urais maana angekuwa anasindikizwa na ving`ora asingepata muda wa kukijenga chama ila 2015 tukichukua nchi chama kitakuwa kimeimarika

Una viroba pembeni au vp? Maana unanipa wasiwasi mkuu
 
Kumbe Slaa, yeye ndio anapanga viongozi kila sehemu hakuna uchaguzi wala nini zidumu fikra za Katibu Mkuu!

Hivi unasomaga habari kwa uangalifu kweli au ukoje wewe?
 
Back
Top Bottom