Baraza Kuu la CHADEMA mkoani hapa limepangua safu ya uongozi wa juu wa mkoa kwa kuwateua viongozi wa muda watakaokiongoza chama hicho hadi Mei.
Kikao hicho kizito kilifanyika karibu usiku mzima chini ya usimamizi wa Dk. Slaa ambaye baadaye alitangaza safu mpya ya uongozi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Nzovwe mjini hapa.
Dk. Slaa alimtangaza Peter Mwamboneke kuwa kaimu mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Mbeya, nafasi ambayo ilikuwa wazi baada ya aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho Sambwee Shitambala kuhamia Chama cha Mapinduzi (CCM)
Diwani wa kata ya Forest katika halmashauri ya jiji la Mbeya, Boid Mwabulanga, alitangazwa kuwa kaimu katibu wa chama hicho akichukua nafasi ya Eddo Mwamalala Makata.
Dk. Slaa alimtaja Joseph Kasambala kuwa ameteuliwa kuwa Kaimu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana (BAVICHA) mkoa wa Mbeya, akichukua nafasi ya Exavery Mwalyembe.
Seleman Simbayanje ameteuliwa kuwa Kaimu Katibu wa Baraza la Wazee wakati Tamali Mbarasya alitagazwa kuwa mratibu wa wanawake wa chama hicho.
Juzi usiku Dk. Slaa ambaye ameambatana na Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa chama hicho, Wilfred Rwakatare, alihamia kwenye kikao cha Baraza la Chama hicho wilaya ya Mbeya Mjini, ambako baadhi ya wanachama walidai kwamba hawana imani na Mwenyekiti wa CHADEMA Mbeya Mjini, David Mwambigija, maarufu kwa jina la Mzee wa Upako.
Habari kutoka ndani ya mkutano huo zimeeleza kuwa wajumbe wa baraza hilo waliamua kumweka kando mzee wa upako na kisha kupiga kura ya kutokuwa na imani naye.
Kwa mujibu wa chanzo chetu kura zilizopigwa zilikuwa 231 na ni kura tano tu ndizo zilizomkataa Mwambigija huku kura 226 zikimkubali.
Kura ya kutokuwa na imani na Mzee wa Upako ilifanyika lakini wajumbe wengi wameoyesha kumwamini na hivyo anaendelea na wadhifa wake, kilisema chanzo chetu. Habari zimesema kuwa kufanyika kwa mabadiliko hayo, kutaongeza kasi zaidi ya utendaji kazi hasa kwa kuzingatia kuwa mwaka huu ni wa uchaguzi ndani ya chama hicho
SOURCE:TANZANIA DAIMA
Kikao hicho kizito kilifanyika karibu usiku mzima chini ya usimamizi wa Dk. Slaa ambaye baadaye alitangaza safu mpya ya uongozi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Nzovwe mjini hapa.
Dk. Slaa alimtangaza Peter Mwamboneke kuwa kaimu mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Mbeya, nafasi ambayo ilikuwa wazi baada ya aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho Sambwee Shitambala kuhamia Chama cha Mapinduzi (CCM)
Diwani wa kata ya Forest katika halmashauri ya jiji la Mbeya, Boid Mwabulanga, alitangazwa kuwa kaimu katibu wa chama hicho akichukua nafasi ya Eddo Mwamalala Makata.
Dk. Slaa alimtaja Joseph Kasambala kuwa ameteuliwa kuwa Kaimu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana (BAVICHA) mkoa wa Mbeya, akichukua nafasi ya Exavery Mwalyembe.
Seleman Simbayanje ameteuliwa kuwa Kaimu Katibu wa Baraza la Wazee wakati Tamali Mbarasya alitagazwa kuwa mratibu wa wanawake wa chama hicho.
Juzi usiku Dk. Slaa ambaye ameambatana na Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa chama hicho, Wilfred Rwakatare, alihamia kwenye kikao cha Baraza la Chama hicho wilaya ya Mbeya Mjini, ambako baadhi ya wanachama walidai kwamba hawana imani na Mwenyekiti wa CHADEMA Mbeya Mjini, David Mwambigija, maarufu kwa jina la Mzee wa Upako.
Habari kutoka ndani ya mkutano huo zimeeleza kuwa wajumbe wa baraza hilo waliamua kumweka kando mzee wa upako na kisha kupiga kura ya kutokuwa na imani naye.
Kwa mujibu wa chanzo chetu kura zilizopigwa zilikuwa 231 na ni kura tano tu ndizo zilizomkataa Mwambigija huku kura 226 zikimkubali.
Kura ya kutokuwa na imani na Mzee wa Upako ilifanyika lakini wajumbe wengi wameoyesha kumwamini na hivyo anaendelea na wadhifa wake, kilisema chanzo chetu. Habari zimesema kuwa kufanyika kwa mabadiliko hayo, kutaongeza kasi zaidi ya utendaji kazi hasa kwa kuzingatia kuwa mwaka huu ni wa uchaguzi ndani ya chama hicho
SOURCE:TANZANIA DAIMA