Sitta na Mwakyembe wamejitwalia umaarufu kwa muda mrefu kama makamanda wa kupinga ufisadi ndani ya chama cha majoka. Lakini ufisadi ktk ccm ni namna tu ya kawaida ya kutenda kazi...ni mfumo ambao hakuna jinsi ya kujitenga nao ukiwa ndani. Sasa ni kweli hawa jamaa hawajui kwamba huwezi kusukuma gari ukiwa ndani yake, au wanajificha humo ili kulinda ulaji wao? Kweli mtu mzalendo mwenye uchungu na taifa hili anaweza kuendelea kukaa katika chama hiki? Sitta alisema juzi kwamba inamgharimu kushikilia misingi ya baba wa taifa ndani ya chama chake,lakini hawezi kutoka hadi kieleweke; kwani baba wa taifa aliweka misingi hiyo kwa chama au kwa taifa zima? Kwani kushiikilia misingi hiyo ni lazima uwe ndani ya ccm? Nachelea kwamba hawa wazee wamepoteza hadhi yao ya uadilifu wa dhati.