*SITASUBIRI KUMPONGEZA CYPRIAN MUSIBA*
Febr 25, 2018
Umevunja ukimwa, umefanya vyema.
Siku zote historia ni mwalimu mzuri na wahenga walinena aisifiae mvua imemnyea.
Naandika kukupongeza Cyprian Musiba kwa kuvunja ukimya. Najua wapo walioanza kukushambulia, najua wameanza kuchimbua mengi uliyowahi kuyasema siku za nyuma, najua watakuita majina mengi. Mimi nasema kwa hili la kuwataja watu 10 hatari kwa Taifa, umeifanya kazi na umetimiza wajibu wako kwa Taifa.
Mwaka 2011 wakati vuguvugu la kumng’oa kiongozi wa Libya Muammar Ghadaff, mataifa ya nje kupitia mbinu mbalimbali kama vile mashirika ya kimataifa, mashirika ya haki za binadamu, waandishi wa habari wa ndani ya Libya na wa nje, vijana waliohemka na baadaye kuingia kwenye vyombo vya usalama vya nchi waliyafanya haya haya uliyoyasema.
Waliwatumia wanasiasa wa ndani ya Libya kuanzisha mtafaruku na baadaye wakawa wanaungwa mkono na mashirika, vyombo vya habari, mitandao ya kijamii ikatumika sana kumshambulia Rais Ghadaff.
Vitendo vya hatari hivyo vilibezwa na Rais Ghadaff mwenyewe hakutilia mkazo zaidi ya kutambua kuwa hao ni vibaraka wanaotumiwa na mataifa ya magharibi.
Walikuwepo wananchi wa Libya waliokuwa wanaishi Marekani na Ulaya walioendesha kampeni za kumchafua Ghadaff na Serikali ya Libya kwamba ni ya kidikteta na kuwahamasisha wananchi wa Libya waungane kuitoa madarakani.
Mashirika ya kimataifa yaliitisha mikutano ya vyombo vya habari ndani na nje ya Libya kuushambulia utawala wa Ghadaff na kuhamasisha watu wafanye vurugu dhidi ya Serikali.
Mataifa ya nje yaliwaita wanasiasa na kwenda nchini kwao kuwafundisha mbinu za kumng’oa Ghadaff kama wanavyofanyiwa akina Zitto Kabwe, Julius Mtatiro, John Mrema, John Mnyika, Godbless Lema, Joshua Nassari na wengine wengi.
Walitumika Walibya waliopo nje ya Libya hasa Ulaya na Marekani kama ilivyo kwa Mange Kimambi.
Walihamasishwa vijana wasirudi nyuma hadi wammalize Ghadaff.
Najua historia hii wengi wanaijua na vijana wengi hawaijui.
Kampeni hii ilifanyika ikabezwa na matokeo yake Muammar Ghadaff walimuua. Lakini kwa kuwa walifanya kwa mihemko bila kujua baada ya hapo kitafuata nini, Libya iliingia kwenye machafuko mpaka leo.
Hii leo Walibya wanaishi kama wapo jehanamu. Wapo radhi wajitose bahari wafe kujiepusha na machafuko yaliyopo nchini kwao. Matumaini waliyoyapata hakuna tena. Waliowahamasisha wafanye waliyoyafanya hawawaoni tena. Hata wale vinara walioipindua Serikali ya Ghadaff wameingia katika mapambano ya wenyewe kwa wenyewe. Hakukaliki hakufai.
Wakati ule wapo waandishi wa habari walioandika na kutahadharisha kama alivyofanya Cyprian Musiba. Kama kawaida walibezwa wakapuuzwa, wananchi waliwazomea na kuwaona wanajipendekeza kwa Ghadaff.
Waandishi wa habari hao waliwataja mpaka vinara wanaotaka kuleta mgogoro Libya lakini wapi. Na badala yake wakawa wanatishiwa maisha.
Hii leo kilichowapata Libya wamefikia mahali wanaota kumpa Urais mtoto wa Muammar Ghaddafi aitwaye Bw. Saif Al-Islam Ghaddafi.
Saif Al-Islam Ghaddafi wakati wa sekeseke lilisababisha kifo cha Baba yake naye alipatwa na msukosuko mkubwa almanusura wamuue lakini wakaamua kumchukulia hatua za kisheria, yamekwenda yamepoa na kwa kilichowakuta kimewafanya hivi sasa Walibya wanaombea apate Urais lakini Libya ikiwa imebomoka kabisa. Wanata aijenge Libya upya kama alivyoijenga Baba yake.
Wanaombea Saif Al-Islam awarudishie Libya iliyokuwa jangwa ikageuzwa kuwa kijani kibichi, iliyokuwa na njaa ikawa na chakula bwelele, iliyokuwa inatoa elimu bure, maji na umeme bure, iliyokuwa inatoa ruzuku kwa wanandoa iliyojengwa na ikawa kinara wa Afrika. Wanaota kuirudisha pepo ya Libya ambayo watu wake hawakupenda kwenda nje ya nchi. Waarabu matajiri wa Afrika.
Namuunga mkono Cyprian Musiba kwa sababu huu upuuzi unaofanywa na Mbowe na genge lake wanasiasa wa CHADEMA, ambao sasa wamejipambanua kuwatumia akina Mange Kimambi, Evarist Chahali na vijana waliowaajiri kufanya uchochezi kwenye mitandao akina Yericko Nyerere na Julius Mtatiro, ukipuuzwa Tanzania hii ambayo ndio kwanza inataka kuinuka itapotea kabisa.
Labda tukumbushane pakichafuka hapa hii reli ya kati (standard gauge) tutaisahau, umeme wa stieglers’ gorge hatutaupata, bandari zinazojengwa hatutaziona, elimu bure tunayoipata tutaisikia bombani, askari na wanajeshi tunawachezea sharubu hawatakuwa na sisi tena, mahakama hazitafanya kazi yao, hospitali hakutakuwa na huduma, wafanyabiashara watafunga biashara zao kuhofia hasara, usafiri wa kutoka sehemu moja kwenda nyingi hautawezekana, huduma katika ofisi za serikali hazitakuwepo.
Kazi itakayokuwepo ni ya Vyombo vya serikali kupambana na wanaoipinga Serikali. Tutawaona wanajeshi, polisi na askari wengine wakiwa na bunduki, vifaru, magari ya washawasha, mabomu na kila aina ya silaha wakiwa mitaani kupambana na wapinzani.
Wakati huo hakutakuwa na msiba, itakuwa mwenzako akiuawa unakimbia kuokoa roho yako, hakutakuwa na familia, kila mmoja atakuwa anahangaika na usalama wake, njia za mawasiliano hazitakuwa zinafanya kazi, watakaokuwa wanawasiliana ni askari waliopo katika mapambano na waasi wanaotengenezwa na akina Mbowe, Mtatiro, Tundu Lissu na Mange Kimambi ambao watakuwa tayari wapo nje ya nchi wamepata hifadhi ya kisiasa kwa hao wanaowatuma.
Ni lazima tujue hatari hii, wakati huo kumuona Mama yako mzazi anabakwa haitakuwa ajabu, kuona mdogo wako anapigwa risasi haitakuwa ajabu, kuona nyumba yenu inachomwa moto na mnabaki hamna pa kulala wala chakula haitakuwa ajabu, hiki chakula kingi tunachokula na kupata nguvu ya kuhamasishana kufanya fujo hakitakuwepo. Koo zitavurugika na maisha yatasimama.
Nataka kukumbusha kuwa haya wanatoyasema akina Mbowe kuwa ni lazima watu wafe kama 100 au 200 haitakuwa hivyo itakuwa ni maelfu kwa maelfu.
Libya aliondolewa Ghaddafi kwa sababu ya utajiri wa mafuta. Hatuna tofauti nao sisi sasa tuna utajiri wa gesi, madini, ardhi na maji ya kutosha. Ukiwa na kiongozi kama Rais Magufuli ambaye amejitoa muhanga kupigania rasilimali za nchi hii mataifa ya magharibi ambao ndio wahusika wakuu wa kunyonya mali hizi lazima watakifanya hiki kinachotokea sasa.
Vibaraka wa kuwaunga mkono ndio hawa wanasiasa na wanaharakati na waandishi wa habari na mashirika ya kimataifa. Sasa kazi ni kwetu Watanzania tunasimama pamoja kukataa ama tunakubali kuingia kwenye mtego huu?
Ndio maana nampongeza Cyprian Musiba kwa kuvunja ukimwa. Maana nashangaa nchi hii ina wasomi lakini wamekaa kimya, sasa sijui wanaujua upuuzi huu ama hawaujui ama ndio wameungana na vibaraka hao?
Nawapongeza wabunge kwa namna wanavyokabiliana na wapuuzi waliotaka kulitumia bunge kutimiza dhamira hii ovu.
Naamini vyombo vya dola vitachukua hatua. Sikatai kukosolewa lakini kukosoa kunakolenga kulibomoa Taifa hakukubaliki.
Na mimi nataka niwaambie Watanzania msitegemee kuwa vyombo vya dola vitakuja kufanya tofauti na anavyotaka Mkuu wa nchi. Tutahamasishwa kuandamana sawa lakini lazima tujue tukiandamana tutapigwa na tena kwa mwendo huu tutapigwa za moto. Tutakuwa tunalia kila siku lakini bila sababu ya msingi.
Hao akina Mbowe hata kama watapewa nchi leo watafanya nini? Wataanzisha jeshi lao? Watakuwa na wafanyakazi wao wa Serikali? Kwa akili gani waliyonayo?
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete aliwahi kusema za kuambiwa changanya na zako.
Febr 25, 2018
Umevunja ukimwa, umefanya vyema.
Siku zote historia ni mwalimu mzuri na wahenga walinena aisifiae mvua imemnyea.
Naandika kukupongeza Cyprian Musiba kwa kuvunja ukimya. Najua wapo walioanza kukushambulia, najua wameanza kuchimbua mengi uliyowahi kuyasema siku za nyuma, najua watakuita majina mengi. Mimi nasema kwa hili la kuwataja watu 10 hatari kwa Taifa, umeifanya kazi na umetimiza wajibu wako kwa Taifa.
Mwaka 2011 wakati vuguvugu la kumng’oa kiongozi wa Libya Muammar Ghadaff, mataifa ya nje kupitia mbinu mbalimbali kama vile mashirika ya kimataifa, mashirika ya haki za binadamu, waandishi wa habari wa ndani ya Libya na wa nje, vijana waliohemka na baadaye kuingia kwenye vyombo vya usalama vya nchi waliyafanya haya haya uliyoyasema.
Waliwatumia wanasiasa wa ndani ya Libya kuanzisha mtafaruku na baadaye wakawa wanaungwa mkono na mashirika, vyombo vya habari, mitandao ya kijamii ikatumika sana kumshambulia Rais Ghadaff.
Vitendo vya hatari hivyo vilibezwa na Rais Ghadaff mwenyewe hakutilia mkazo zaidi ya kutambua kuwa hao ni vibaraka wanaotumiwa na mataifa ya magharibi.
Walikuwepo wananchi wa Libya waliokuwa wanaishi Marekani na Ulaya walioendesha kampeni za kumchafua Ghadaff na Serikali ya Libya kwamba ni ya kidikteta na kuwahamasisha wananchi wa Libya waungane kuitoa madarakani.
Mashirika ya kimataifa yaliitisha mikutano ya vyombo vya habari ndani na nje ya Libya kuushambulia utawala wa Ghadaff na kuhamasisha watu wafanye vurugu dhidi ya Serikali.
Mataifa ya nje yaliwaita wanasiasa na kwenda nchini kwao kuwafundisha mbinu za kumng’oa Ghadaff kama wanavyofanyiwa akina Zitto Kabwe, Julius Mtatiro, John Mrema, John Mnyika, Godbless Lema, Joshua Nassari na wengine wengi.
Walitumika Walibya waliopo nje ya Libya hasa Ulaya na Marekani kama ilivyo kwa Mange Kimambi.
Walihamasishwa vijana wasirudi nyuma hadi wammalize Ghadaff.
Najua historia hii wengi wanaijua na vijana wengi hawaijui.
Kampeni hii ilifanyika ikabezwa na matokeo yake Muammar Ghadaff walimuua. Lakini kwa kuwa walifanya kwa mihemko bila kujua baada ya hapo kitafuata nini, Libya iliingia kwenye machafuko mpaka leo.
Hii leo Walibya wanaishi kama wapo jehanamu. Wapo radhi wajitose bahari wafe kujiepusha na machafuko yaliyopo nchini kwao. Matumaini waliyoyapata hakuna tena. Waliowahamasisha wafanye waliyoyafanya hawawaoni tena. Hata wale vinara walioipindua Serikali ya Ghadaff wameingia katika mapambano ya wenyewe kwa wenyewe. Hakukaliki hakufai.
Wakati ule wapo waandishi wa habari walioandika na kutahadharisha kama alivyofanya Cyprian Musiba. Kama kawaida walibezwa wakapuuzwa, wananchi waliwazomea na kuwaona wanajipendekeza kwa Ghadaff.
Waandishi wa habari hao waliwataja mpaka vinara wanaotaka kuleta mgogoro Libya lakini wapi. Na badala yake wakawa wanatishiwa maisha.
Hii leo kilichowapata Libya wamefikia mahali wanaota kumpa Urais mtoto wa Muammar Ghaddafi aitwaye Bw. Saif Al-Islam Ghaddafi.
Saif Al-Islam Ghaddafi wakati wa sekeseke lilisababisha kifo cha Baba yake naye alipatwa na msukosuko mkubwa almanusura wamuue lakini wakaamua kumchukulia hatua za kisheria, yamekwenda yamepoa na kwa kilichowakuta kimewafanya hivi sasa Walibya wanaombea apate Urais lakini Libya ikiwa imebomoka kabisa. Wanata aijenge Libya upya kama alivyoijenga Baba yake.
Wanaombea Saif Al-Islam awarudishie Libya iliyokuwa jangwa ikageuzwa kuwa kijani kibichi, iliyokuwa na njaa ikawa na chakula bwelele, iliyokuwa inatoa elimu bure, maji na umeme bure, iliyokuwa inatoa ruzuku kwa wanandoa iliyojengwa na ikawa kinara wa Afrika. Wanaota kuirudisha pepo ya Libya ambayo watu wake hawakupenda kwenda nje ya nchi. Waarabu matajiri wa Afrika.
Namuunga mkono Cyprian Musiba kwa sababu huu upuuzi unaofanywa na Mbowe na genge lake wanasiasa wa CHADEMA, ambao sasa wamejipambanua kuwatumia akina Mange Kimambi, Evarist Chahali na vijana waliowaajiri kufanya uchochezi kwenye mitandao akina Yericko Nyerere na Julius Mtatiro, ukipuuzwa Tanzania hii ambayo ndio kwanza inataka kuinuka itapotea kabisa.
Labda tukumbushane pakichafuka hapa hii reli ya kati (standard gauge) tutaisahau, umeme wa stieglers’ gorge hatutaupata, bandari zinazojengwa hatutaziona, elimu bure tunayoipata tutaisikia bombani, askari na wanajeshi tunawachezea sharubu hawatakuwa na sisi tena, mahakama hazitafanya kazi yao, hospitali hakutakuwa na huduma, wafanyabiashara watafunga biashara zao kuhofia hasara, usafiri wa kutoka sehemu moja kwenda nyingi hautawezekana, huduma katika ofisi za serikali hazitakuwepo.
Kazi itakayokuwepo ni ya Vyombo vya serikali kupambana na wanaoipinga Serikali. Tutawaona wanajeshi, polisi na askari wengine wakiwa na bunduki, vifaru, magari ya washawasha, mabomu na kila aina ya silaha wakiwa mitaani kupambana na wapinzani.
Wakati huo hakutakuwa na msiba, itakuwa mwenzako akiuawa unakimbia kuokoa roho yako, hakutakuwa na familia, kila mmoja atakuwa anahangaika na usalama wake, njia za mawasiliano hazitakuwa zinafanya kazi, watakaokuwa wanawasiliana ni askari waliopo katika mapambano na waasi wanaotengenezwa na akina Mbowe, Mtatiro, Tundu Lissu na Mange Kimambi ambao watakuwa tayari wapo nje ya nchi wamepata hifadhi ya kisiasa kwa hao wanaowatuma.
Ni lazima tujue hatari hii, wakati huo kumuona Mama yako mzazi anabakwa haitakuwa ajabu, kuona mdogo wako anapigwa risasi haitakuwa ajabu, kuona nyumba yenu inachomwa moto na mnabaki hamna pa kulala wala chakula haitakuwa ajabu, hiki chakula kingi tunachokula na kupata nguvu ya kuhamasishana kufanya fujo hakitakuwepo. Koo zitavurugika na maisha yatasimama.
Nataka kukumbusha kuwa haya wanatoyasema akina Mbowe kuwa ni lazima watu wafe kama 100 au 200 haitakuwa hivyo itakuwa ni maelfu kwa maelfu.
Libya aliondolewa Ghaddafi kwa sababu ya utajiri wa mafuta. Hatuna tofauti nao sisi sasa tuna utajiri wa gesi, madini, ardhi na maji ya kutosha. Ukiwa na kiongozi kama Rais Magufuli ambaye amejitoa muhanga kupigania rasilimali za nchi hii mataifa ya magharibi ambao ndio wahusika wakuu wa kunyonya mali hizi lazima watakifanya hiki kinachotokea sasa.
Vibaraka wa kuwaunga mkono ndio hawa wanasiasa na wanaharakati na waandishi wa habari na mashirika ya kimataifa. Sasa kazi ni kwetu Watanzania tunasimama pamoja kukataa ama tunakubali kuingia kwenye mtego huu?
Ndio maana nampongeza Cyprian Musiba kwa kuvunja ukimwa. Maana nashangaa nchi hii ina wasomi lakini wamekaa kimya, sasa sijui wanaujua upuuzi huu ama hawaujui ama ndio wameungana na vibaraka hao?
Nawapongeza wabunge kwa namna wanavyokabiliana na wapuuzi waliotaka kulitumia bunge kutimiza dhamira hii ovu.
Naamini vyombo vya dola vitachukua hatua. Sikatai kukosolewa lakini kukosoa kunakolenga kulibomoa Taifa hakukubaliki.
Na mimi nataka niwaambie Watanzania msitegemee kuwa vyombo vya dola vitakuja kufanya tofauti na anavyotaka Mkuu wa nchi. Tutahamasishwa kuandamana sawa lakini lazima tujue tukiandamana tutapigwa na tena kwa mwendo huu tutapigwa za moto. Tutakuwa tunalia kila siku lakini bila sababu ya msingi.
Hao akina Mbowe hata kama watapewa nchi leo watafanya nini? Wataanzisha jeshi lao? Watakuwa na wafanyakazi wao wa Serikali? Kwa akili gani waliyonayo?
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete aliwahi kusema za kuambiwa changanya na zako.