Sitasahau: Ubabe wa wanajeshi uliwatokea puani

Sitasahau: Ubabe wa wanajeshi uliwatokea puani

usawa wa kulia

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2014
Posts
454
Reaction score
154
Ilikua 2011, mtoto wa mjeda aliniibia nguruwe wangu Lugalo mabandani, wakati upelelezi na taratibu za kumshika zikiendelea nlienda Lugalo, yule mtoto aliniona wakajikusanya watoto wa wajeda wakanipiga sana na kumpeleka MP jirani na Mwenge napo nlipigwa sana nkapewa ma MP 2 niende nao polisi Kawe nkafute kesi kinguvu.

Nlimweleza mpelelezi wangu nlipofika kituoni aliwabana wale ma MP kwa maswali wakafyata matako na kua bubu japo wanajifanyaga wababe,
mpelelezi alimwambia mjeda ambaye mwanae kanibia kua anapeleka kesi COURT na anafungua kesi nyingine kuwa wamenipiga.. Yule mjeda alinywea kama mtoto ili asamehewe mwishowe alinipa laki ya kunipoza, akampa mpelelezi hamsini na ishrini ya kufuta kesi.
 
rai yangu TUSIWAOGOPE WAPUUZI WACHACHE wanaojifanyaga wababe hata kama wao ndio wana makosa bz kuna sheria za nchi ambazo hata wao lazima wazifuate
 
Hakuna alie juu ya sheria.

Hawa jamaa wanapenda utemi wa kulazimisha
 
vipi kitimoto wako alirudi sasa!?.. au ndio fidia ilicover the costs...
 
Hiyo sawa, ila ungepanda kwa wakubwa wao hata hiyo ajira zao zingekuwa mashakani usiombe ukimpata mkubwa wake halafu akakuelewa waweza kujuta kwanini ulimsemea waweza kumuombea poo.
 
umeniuzi wewe na hakimu wako kwa kukubali kupokea rushwa na kufungwa mdomo. Cpati picha ningekua mimi wangenitibia hadi magonjwa niliyozaliwa nayo na kunipa fidia kubwa sana. Yani wamenipiga dah
 
Wee kweli kichwa cha kuku...

unapigwa na watoto, na MP...tena unasema sana, kisha unapewa Laki.....

Wee kichwa kuku
 
Mkuu,

Nilidhani uliwatoa nduki!

Kumbe ulitandikwa kama kawaida.

Kuna mmoja ni mstaafu aliwalazimisha majirani zake hapo mtaani kwamba waboreshe nyumba zao wanamtia aibu anapotembelewa na wageni wake.
 
Umeniudhi kwa sababu ulikubali kupokea rushwa ili kesi isiendelee
Pumbavu zako
 
Mkuu,

Nilidhani uliwatoa nduki!

Kumbe ulitandikwa kama kawaida.

Kuna mmoja ni mstaafu aliwalazimisha majirani zake hapo mtaani kwamba waboreshe nyumba zao wanamtia aibu anapotembelewa na wageni wake.

Duh!!!,sasa siangewapa mkwanja wa kukarabatia hizo nyumba???!!!!!.
 
Back
Top Bottom