mutu ya watu
JF-Expert Member
- Dec 19, 2010
- 213
- 41
Hii ni kali ya mwaka! ni kisa cha dada mmoja sister duu!. kilichotokea jijini Dar, dada huyu akiwa amevalia vilivo kimtoka wakidaslam(vimodos), walitoka na Bf wake weekend moja wakaamua kwenda kupumzika kwenye guest moja, usiku Bf wake akamwambia kuwa kesho itabidi atoke mapema kwa kuwa alikuwa safari, ilipofika saa kumi na moja kweli akamuaga na kuondoka. ikabidi na yeye aanze kujiandaa mdogomdogo kufika 12 asbh na yeye akawatayari kuondoka. ili kufika kwake ilibidi apande magari mawili aliposhuka tu kituo cha kwanza ili upande gari nyingine inabidi utembee kwanza sababu kuna kamwendo fulani cha ajabu kila mtu aliyemwangalia alikuwa akishangaa na wengine wakimcheka akapotezea, baadaye akaamua kujicheck, dah kujiangaalia miguun kaona ndala ya mguu mmoja ni tofauti na ndala ya mguu na tena zimekatwa kwa mbele, ikabidi ajishangae kumbe sandals zake ameziacha guest na kubadilisha na ndala za guest, mbaya zaid maduka yalikuwa bado hayajafunguliwa ikabidi amwendee muokota makopo mmoja na kubadilisha naye na kumwoongezea hela sh500 nia yake apate viatu vya kufanana japovimekwisha! duuh! mambo haya.....!!!