MziziMkavu, Bible inasema 'Nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukizao'
Lakini Mungu alivyo mwema, hakosi kuwa na suluhisho, anaendelea 'Nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu', hii inavunja ile laana ya mwanzo. Ni kweli malezi na njia anazokuzwa mtoto zinamfanya awe atakavyokuwa. Lakini kama akipata mwanga kutoka kwa jamii inayomzunguka, huenda ikamsaidia kurekebisha walipokosea wazazi na kuanza mwanzo mpya kwa ajili ya wanae!