Tanesco., Shirika pekee linalogawa umeme, limeweka luku, watanzania wanalipa, linapataje hasara? kama kuna watu wana daiwa kwanini lisiwakatie? Hasara ya bilioni 90 jamani hebu wana JF kila mmoja arudi aangalie bajeti ya Serikali kuna Wizara ngapi zinapewa Fesha kidogo sana kuliko Ruzuku ya Bilioni 231 zinzotumiwa na Tanesco kutengeneza Dairy na Kalenda, kutolea matangazo ya kukanusha mgawo hata kama tunaona nchi ipo gizani, Hongera gazeti la Tanzania Daima, kwa kueleza kwa ufasaha mambo ambayo magazeti mengine yanaogopa. Watanzania wanatoka nyumbani hawajanyoosha nguo, nyimbani giza, lakini magazeti yanaletewa tangazo kuwa hakuna mgawo yanaleta kwa wananchi