sio kesi lakini ni mtizamo wangu tu kuwa salamu zetu huwa zipo kinafki sana.unakuta yes mnafahamiana kabisa na kila mtu anajua jinsi maisha yanavotukimbiza resi,ubize ila kwenye salamu tu mmekutana naye labda mtaani au njian mtu atataka musalimiane dakika kumi,maneno mengi afu ni yale yale
Mfano wa story tumekutana
Mtu:habari ndege
Mimi:safi sana
Mtu:upo?
Mimi:yeah nipo
Mtu:huonekani
Sasa huwa najiuliza huwa tumekaririshwa hadi salamu mtu anakuambia huonekani as if kwamba imeandikwa mtakuwa pamoja saa zote.na wakati anajua kabisa maisha tupo mazingira tofauti
Mfano wa story nyingine
Mtu:shwari
Mimi:ni shwari
Mtu:kama kawaida?
Sasa najiuliza hio kawaida si ndo maana tunaendelea kuishi
Mtu:nambie
Sasa nikwambie kitu gani wakati tunayoyaona ndo haya haya
NINGEWEZA KUTOA MIFANO MINGINE YA SALAMU AMBAZO ZINABOA ILA POINT YANGU YA MUHIMU JAPO SIO YA MSINGI NI KUWA SALAMU ZA KISWAHILI NI KAMA VILE TUNAKARIRISHWA MANENO YA KUSEMA.MPANGILIO WA MAZUNGUMZO HASA TUKIANZA NA SALAMU TUPO SLOW SANA..ME MTU AKIANZA KUZINGUA KWENYE SALAMU TU NASHINDWA KUVUMILIA KUJIAMIN KUONGEA NAYE NAMUONA KAMA AMEKAA KINAFKI NAFKI.namkubali mtu ambaye tukisaliamana tuna flow naturally SASA UNAKUTA MTU HANA CHS KUKWAMBIA LAKINI ILI MUONGEE ATATAKA MSALIMIANE MUDA MREFU
NB:maisha ni zaid ya salamu,hivyo hali kama hizo haziNikwazi sana lakini ndo hivyo huwez kumkataza mtu kufikiri.ndo nimefikiri hivyo kwamba kama huna habari mpya kumwambia mtu msalimie kifupi tu
Mambo vip
Poa
Basi afu pita hivi..sio uanze kumchora mtu akujibu misalamu yako