Malata Junior
JF-Expert Member
- Nov 29, 2011
- 3,108
- 2,553
Kumekuwa na uvumi kwamba CHADEMA imekuwa haijitangazi vijijini na badala yake imejikita maeneo ya mijini tu jambo ambalo si la kweli.Dhana hii ingeweza kukubalika kwa CHADEMA ya miaka mitano iliyopita lakini si CHADEMA ya sasa hasa baada ya kumalizika uchaguzi wa ndani wa chama hivi karibuni.
Miaka ya nyuma CHADEMA haikuwa na viongzi wa ngazi za chini kuanzia misingi,matawi,kata na hata baadhi ya majimbo,wilaya na mikoa uongozi ulikuwa dhaifu sana.Wakati ule chama kilionekana kipo vijijini pale wanapofanya ziara viongozi wa kitaifa hususani mwenyekiti Mbowe,katibu mkuu Slaa na viongozi wengine maarufu kama Lissu,Mnnyika,Mdee,Heche n.k na kwa kiasi fulani MSALITI Zitto (huyu alikuwa anafanya ziara kwa maslahi yake na si ya chama).
Hivi sasa chama hakitegemei ziara za viongozi wa kitaifa kujitangaza na badala yake kila kiongozi anafanya kazi kubwa ya kukieneza na kikitumikia chama katika ngazi yake aliyochaguliwa.
Mfano mimi mwenyewe ni mwenyekiti wa chama wa kata fulani huku Moshi na mjumbe wa kamati ya utendaji ya jimbo lakini mimi na viongozi wenzangu wa kata,matawi na misingi hatutegemei kiongozi yeyote wa kitaifa aje akitangaze chama kwenye kata yetu bali tunawajibika wenyewe tena kwa bidii kubwa.
Hivyo vijana wa Lumumba msikariri kwamba CHADEMA ni Mbowe na Slaa tu kama mnavyofikiri CCM ni Kinana na Nape tu mpaka kupelekea viongozi wengine kukalia benchi hapo Lumumba huku Kinana na Nape wakipuyanga mikoani kila kukicha, au vijana wa Mwandiga mnavyodhani ACT ni Zitto kiasi hata mnashindwa kufanya uchaguzi mpaka Zitto ajiunge rasmi.
CHADEMA ni taasisi yenye viongozi kila ngazi kwa mujibu wa katiba yake na viongozi wake hasa vijijini wako kwenye harakati kubwa hivi sasa za kusimika wagombea ngazi ya mitaa,vijiji na vitongoji.
Baada ya uchaguzi wa serikali za mitaa tutaheshimiana tu.
Miaka ya nyuma CHADEMA haikuwa na viongzi wa ngazi za chini kuanzia misingi,matawi,kata na hata baadhi ya majimbo,wilaya na mikoa uongozi ulikuwa dhaifu sana.Wakati ule chama kilionekana kipo vijijini pale wanapofanya ziara viongozi wa kitaifa hususani mwenyekiti Mbowe,katibu mkuu Slaa na viongozi wengine maarufu kama Lissu,Mnnyika,Mdee,Heche n.k na kwa kiasi fulani MSALITI Zitto (huyu alikuwa anafanya ziara kwa maslahi yake na si ya chama).
Hivi sasa chama hakitegemei ziara za viongozi wa kitaifa kujitangaza na badala yake kila kiongozi anafanya kazi kubwa ya kukieneza na kikitumikia chama katika ngazi yake aliyochaguliwa.
Mfano mimi mwenyewe ni mwenyekiti wa chama wa kata fulani huku Moshi na mjumbe wa kamati ya utendaji ya jimbo lakini mimi na viongozi wenzangu wa kata,matawi na misingi hatutegemei kiongozi yeyote wa kitaifa aje akitangaze chama kwenye kata yetu bali tunawajibika wenyewe tena kwa bidii kubwa.
Hivyo vijana wa Lumumba msikariri kwamba CHADEMA ni Mbowe na Slaa tu kama mnavyofikiri CCM ni Kinana na Nape tu mpaka kupelekea viongozi wengine kukalia benchi hapo Lumumba huku Kinana na Nape wakipuyanga mikoani kila kukicha, au vijana wa Mwandiga mnavyodhani ACT ni Zitto kiasi hata mnashindwa kufanya uchaguzi mpaka Zitto ajiunge rasmi.
CHADEMA ni taasisi yenye viongozi kila ngazi kwa mujibu wa katiba yake na viongozi wake hasa vijijini wako kwenye harakati kubwa hivi sasa za kusimika wagombea ngazi ya mitaa,vijiji na vitongoji.
Baada ya uchaguzi wa serikali za mitaa tutaheshimiana tu.