Mmiliki wa kampuni ya IPTL,Harbinder Seth, ametoweka na vyombo vya usalama vimejiandaa kumkamata ndapo atarejea nchini, Raia mwema limeelezwa.Singh ambayekampuni yake ya Pan african Power solution (PAP) inadaiwa kununua umiliki wa kampuni ya kufua umeme ya IPTL katika mazingira yaliyozua utata, anadaiwa kuwa yupo nchini Kenya au Africa ya Kusini.
Gazeti hili limeelezwa kwamba Singh aliondoka nchini siku chache kabla ya bunge la Tanzania ya wahusika wote wa makosa ya kijinai katika suala hilo wakamatwe na hatua za kisheria dhidi yao zichukuliwe.
Azimio namba moja la Bunge lilisema;....Takukuru, Jeshi la polisi na vyombo vingine husika vya Ulinzi na usalama viwachukule hatua stahiki za kisheria, kwa mujibu wa sheria za nchi yetu,watu wote waliotajwa na Taarifa maalumu ya kamati kuhusika na vitendo vyote vya kijinai kuhusiana na miamala ya akaunti ya Escrow, kuhusika katika vitendo hivyo vya jinai kufuatia uchunguzi mbalmbali unavyoendelea.
Raiamwema limeelezwa kwamba, singh ambaye katka siku za nyuma alikua akipenda kufika katika hotel mbalimbali ikiwemo Sea cliff ya Jijini dar es salaam, Sasa hayupo Dar es salaam lakini anafuatilia kea karibu yanayo endelea.
Naweza kukuthibitishia kwamba sethi hayupo nchini hivi sasa. Kwenye hili swala sitaki kuwa mzungumzaji wake lakini nafahamu kwamba aliondoka kabla ya Bunge kuazimia kwamba wahusika wakamatwe.
"Sasa kama alifanya akijua kwamba hayo hayo yanaweza kutokea mimi sijui. Siwezi pia kujibu swali lako la atakuja lini sabau sijaambiwa. Hata hili la kukuambia kwamba hayupo nimekwambia kwa sababu tunafahamiana na sitaki kukudanganya, Alisema mmoja wa watu wafanyakazi wa Sethi ambaye hata hivyo gazeti hili haliwezi kumtaja jina
Inadaiwa kutoroka kwake kumefanikishwa na kidogo mmoja bila kupepesa masikio huyo ni Pinda aka Mzee wa nyukiImeripotiwa kuwa Singasinga wa IPTL ametoweka kwa kuogopa mkono wa dola(Raia Mwema,leo 10.09.2014).
Je,unafikiri kuna uhusiano wowote kati ya kusuasua kutekelezwa kwa maazimio ya bunge na kutoweka kwa bwana Seth Singh?
Na baada ya kutoweka anaweza kurudi tena nchini au atafuata nyayo za homeboy wake Daudi Balali?
Mimi nakubaliana kabisa na wewe mkuu. Walikuwa wanamtafutia mazingira ya kuishi kabla ya kuanza kutajataja mambo yake ili asiwepo akitakiwa kukamatwa.Ndo maana walikuwa wanapinga asikamatwe ili atoroke kwanza
Ndio maana Mkulu anasema eti tusomewe kwanza report ya CAG.....hivi sijui washauri wake ni akina anani huko, haya leteni na mikataba ya Gesi nayo tusome
Vipi Katiba Mpya imeishia wapi?
Wajua Mkulu anatafuta moto zaidi.Akumbuke huku TANZANIA hatupo wajinga kiasi hiki,ningewaomba WAKAGUZI wawe wazalendo waieleze jamii ya watanzania kwa uelewa wa LAYMAN maana ya ripoti yenyewe bila kumung'nya maneno,maana mwisho wa siku tutajigawa mara nyingine tena baada ya ile Katiba ya Mafisadi kupitishwa kwa kutoshelezwa KURA leo RAIS wetu mpendwa anarudia tena kutugonganisha wananchi wake.
Tunachotakiwa kuwa ni WAMOJA zaidi na ziadi.Wahasibu na Wakaguzi tuwepamoja kuielimisha jamii ili tusitenganishwe tena,Huu ni wakati wetu kulitendea haki TAIFA letu.
Thubutttuuuuuuuuuuu hakuna aisee tena hapo Magogoni Chenge ndio kwanza atapokewa kwa nderemo na vifijoNasubiri wa kumwadabisha Chenge kama yupo Hapa Tanzania!
JK alikuwa anamfanyia mbinu za kusepa ndiyo maana hajatoa maamuzi yoyote.
Singasinga hatabalaliwa ila atabadilisha jina tu
Ni kweli kabisa Mpwa wangu, anajua kuwa kitakachosomwa na wachache wetu kitaishia kutuchonganisha zaidi, na kama kweli ana nia ya dhati juu ya hili basi augawe na urais wake tumsaidie kufanya maamuzi. Kweli JK anatuvuruga tu hakuna lolote la maana.
Thubutttuuuuuuuuuuu hakuna aisee tena hapo Magogoni Chenge ndio kwanza atapokewa kwa nderemo na vifijo