Simulizi: Utajiri Wa Damu

Simulizi: Utajiri Wa Damu

Shunie

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2016
Posts
157,054
Reaction score
463,869
Mtunzi Nyemo Chilongani

Sehemu ya 01

"Catherine upo wapi?” ilisikika sauti ya msichana kwenye simu.
“Nyumbani! Kuna nini?”
“Unalala?”
“Ndiyo!”

“Mapema yote hii? Yaani na hili baridi la Arusha bado unalala mapema hii?” aliuliza msichana huyo huku kwa sauti yake jinsi ilivyokuwa ikitoka tu ilionyesha ni kwa jinsi gani alishtushwa kwa kile kilichokuwa kinatokea.

“Nimechoka! Halafu nipo period Amanda!”
“Oh! Kwa hiyo ukiwa period hata kwenda klabu hutaki? Utakula nini kesho?” aliuliza Amanda.

“Nina vijisenti!”
“Kwa hiyo ukiwanavyo hutakiwi kutafuta vingine?”
“Amandaaaaa....”

“Nakupitia hapo! Ngoja niite uber!” alisema Amanda na kukata simu.

Kwa jina aliitwa Catherine Ngolisho. Alikuwa msichana mrembo, mweusi kidogo, mwembamba mwenye sura ya mviringo na lipsi nene ambazo kwa kila mwanaume aliyekuwa akiziangalia alitamani kuzinyonya.
Kifuani alikuwa saa sita, hakuwa mnene lakini kwa nyuma alikuwa na kiwowowofulani cha kiuchokozi ambacho kila mwanaume aliyekuwa akikiona, udenda ulimtoka.

Pamoja na kuwa na uzuri wake, Catherine alikuwa msichana aliyekuwa akiyaendeleza maisha yake huku akijiuza mitaani. Kila siku usiku alikuwa akitoka na wasichana wenzake na kwenda katika Klabu ya Laspinho iliyokuwa katikati ya Jiji la Arusha na kujiuza huko.

Alipata pesa, alipendwa kwa kuwa alikuwa na uzuri wa ajabu ambao uliwachanganya hata watu wengine. Uzuri huo haukuishia machoni tu bali hata kitandani alijua kucheza na mwanaume.

Alicheza michezo yote mibaya, alijua kumdatisha mwanaume, alikuwa na kiuno cha nyigu, alijua kwenda huku na kule, alijua kwenda juu na kurudi chini. Aliutumia mdomo wake vizuri kiasi kwamba kwa kila mwanaume ambaye alimnunua leo, alimuhitaji tena kesho.

Gumzo kubwa likawa kwa Catherine, alikuwa msichana simpo sana ambaye aliyatoa maisha yake kwa kuifanya kazi hiyo kwa kujitoa kwa sababu aliamini ndiyo kitu pekee kilichomfanya kula na kunywa kila siku huku akilipia kodi ya vyumba vyake viwili alivyokuwa akiishi peke yake.
 
Sehemu ya 02.

Kwa sababu aliipenda kazi yake, kila siku Catherine alikuwa akiangalia video za ngono, huko ndipo alipokuwa akijifunzia kila kitu, alichukua utundu wote huko, uchafu wote uliokuwa ukifanyika aliwafanyia wateja wake ambao walikuwa na pesa na kumfanya msichana huyo kuingiza kiasi cha shilingi laki tatu kila alipokuwa akitoka.

Kwa sababu alikuwa mtu hatari faragha, kila mmoja aliyefanyiwa michezo ya hatari alikwenda kumuhadithia mwenzake na hatimaye kila mwanaume kutamani sana kuwa na msichana huyo mrembo ambaye pamoja na fujo zake zote ndiyo kwanza alikuwa na miaka kumi na tisa tu.

Baada ya kupokea simu ya rafiki yake huyo, Catherine akainuka kutoka kitandani, alikuwa amechoka mno, siku hiyo hakutaka kutoka, alihitaji kubaki chumbani kwake, apumzike kwa ajili ya siku nyingine.

Hakutaka kwenda huko kwa kuwa alikuwa kwenye kipindi cha period. Alijiangalia alivyokuwa, hakuzoea kutoka katika hali kama hiyo lakini kwa kuwa aliambiwa na rafiki yake huyo watoke, hakuwa na jinsi, akajiandaa na kisha kumsubiria Amanda.

Baada ya dakika kumi na tano, honi zikaanza kusikika kutoka nje ya nyumba aliyokuwa akiishi, hakutaka kujiuliza mara mbilimbili, akajua kabisa kwamba alikuwa Amanda hiyo kutoka chumbani na kumfuata huku akiwa amevaa suruali yake ya jinzi ya bluu na fulana ya nyekundu ambayo aliikunja mikononi kwa juu.

“Umependeza,” alisema dereva wa Uber, japokuwa hakuwa akimfahamu vizuri msichana huyo lakini alishindwa kuvumilia, alijikuta akimsifia tu pasipo kujali kama Amanda alikuwa humo.

“Nashukuru kaka yangu!” aliitikia kwa sauti nyembambamba kabisa iliyomfanya dereva huyo kuchanganyikiwa.

Catherine alijua kutega, alijua ni kwa jinsi gani mwanaume alitakiwa kudatishwa, sauti yake ilikuwa moja ya mashambulizi makali sana ambayo alipenda kuyapeka kwa adui yake.

Mara ya kwanza tu ambapo ungebahatika kuisikia sauti ya msichana huyo ilikuwa ni lazima kumuomba namba yake ya simu kwa ajili ya mazungumzo ya faragha.
20200601_185201.jpg
 
Sehemu ya 03.

Safari ya kuelekea klabu ikaanza, muda wote dereva wa uber alibaki akiangalia kwenye kioo kile cha ndani, alikuwa akiwaangalia wasichana wale, alichanganyikiwa mno, alimuhitaji Catherine kwani kwa jinsi alivyoonekana, alifaa kabisa kwenda kulala naye usiku wa siku hiyo huku akiwa tayari kutoa pesa zote ambazo alkusanya siku hiyo.
“Ikawaje shosti?” aliuliza Amanda huku safari ikiendelea.

“Basi na kile kitambi chake, alivyokuwa akinilalia, nilikuwa sijisikii kabisa, yaani kwa unene ule na kibamia chake, mmh! Kuna wazee jamani mpaka wanatia hurumaaaa,” alisema Catherine na wote kuanza kucheka.
“Mh! Uliridhika kweli?”

“Walaaaa! Yaani kama ni kula pilau, basi yeye alinionjesha harufu. Ila ana pesa, mzee dakika mbili tu alishindwa kumaliza, akawa hoi, akajilaza tu kama ndama,” alisema Catherine huku akiendelea kucheka.

“Alikulipa?”
“Ndiyo! Yule mbaba ana hela, alinipa laki tano kwa usiku mmoja!”
“Laki tano?”

“Ndiyo! Tena kwa shoo ya dakika tano! Yaani nilimpeleka puta mpaka akaomba poo! Eti akaniambia anataka kunipa gari, nikamwambia sawa, ila nipe na kadi, kasema ataniletea!” alisema Catherine.

Hawakuonekana kujali kama dereva alikuwa akisikia mazungumzo yao, waliendelea kupiga stori huku wakati mwingine wakigongesheana mikono.

Dereva alikuwa hoi, akili yake ilichanganyikiwa kwani kwa jinsi stori alizokuwa akizisikia alijua kabisa kwamba watu waliokuwa wakizungumza walikuwa machangudoa hivyo na yeye kuwa na uhakika wa kupata kama tu angetumia pesa.

Hawakuchukua muda mrefu wakafika katika klabu hiyo na kuteremka. Dereva akashindwa kuvumilia, hapohapo akamuita Catherine ambaye akamsogelea na kusimama mbele yake.

“Niambie!”
“Umependeza sana!” alisema dereva.
“Mara ya pili hiyo unaniambia!”
“Najua! Ila daah!”
“Nini tena jamani!”

“Umeumbika sana! Hebu nikuone kwa nyuma bebi!”alisema dereva, kwa kuwa alionekana kuwa dalili za kuwa mteja, Catherine akageuka na kumtingishia jamaa wowowo.
“Mmh! Maji ya shingo haya!”

“Lakini si unajua kuogelea! Ukishindwa vaa boya,” alisema Catherine na kumuachia mwanaume huyo namba yake.
 
Sehemu ya 04.

Dereva hakutaka kuondoka, alibaki huku akimwangalia msichana huyo alivyokuwa akitembea, aliringa mno, alijua kujitingisha, alimuacha hoi huku muda wote tamaa ikiwa imewaka moyoni mwake.

“Huyu mtoto simuachi! Hata akisema anataka hela ya bosi, bora nitoe zote lakini si kumuacha! Hivi kwa nini Mungu aliumba umasikini? Daah!” alijisemea dereva huyo, akaingia ndani ya gari na kuondoka mahali hapo huku kichwa chake kikimfikiria Catherine tu.

Dereva huyo aliyeitwa Hassan akaondoka huku akiwa na mawazo tele kuhusu Catherine aliyemuona usiku huo. Alifanya kazi zake kama kawaida lakini kila wakati alipokuwa akimfikiria Catherine aliona kabisa kwamba alitakiwa kufanya jambo.

Alikuwa kijana machachari, aliyejua michezo yote kitandani, alikuwa masterplan, alijua kucheza na wanawake, alijua kuwapeleka mpaka pembeni ya kitanda na kuwarudisha kati huku akiwabeba kwa juu, alijua mambo mengi na ndiyo maana hakuona kama alitakiwa kumuacha mtu kama Catherine.

Alipofika nyumbani, hakutaka kumpigia simu, alijifanya kama kutotilia maanani namba ile ili hata kama ingetokea siku anampigia basi aonekane kwamba hana presha kabisa.

Siku hiyo ikapita, aliendelea kufanya kazi kama kawaida, siku ya pili ikapita na ya tatu, ilipofika ya nne, akashindwa kuvumilia, akampigia simu Catherine na kuomba kuonana naye.

“Leo ni siku nzuri,” alisema Catherine, alichomaanisha ni kwamba damu zilikuwa zimekauka, sasa alikuwa huru kwa ajili ya mechi.

“Siku nzuri! Kivipi?” aliuliza Hassan huku akionekana kutokujua lolote lile.
“Kwamba ni wikiendi!” alijibu Catherine.
“Ooh! Sawa kabisa. Ninahitaji sana uje kulala kwangu jamani!” alisema Hassani.
“Kwani wewe unakaa wapi?”
“Ngarenaro!”

“Huko kwa wahuni?”
“Eti kwa wahuni! Njoo bwana!”
“Au mnataka mnifanye threesome?” aliuliza akimaanisha kufanya mapenzi kuanzia na wanaume wawili kwa mpigo.

“Hapana! Just me,” alisema Hassani.
Kazi ya Catherine ilikuwa ni ya hatari, hakumfahamu vizuri mwanaume huyo lakini hakuwa na jinsi, akakubaliana naye na kuelekea huko huku akiwa amevalia gauni lake laini lililokuwa likionyesha maungo yake vizuri kabisa na kukifanya kiwowowo chake kuonekana kila kilipokuwa kikitikisika.
 
Sehemu ya 05.

Hassan alimwambia achukue teksi kwani yeye alikuwa akimsubiri nyumbani. Hilo halikuwa tatizo, Catherine akachukua na kuelekea huko. Alipofika, akateremka na kupokelewa na Hassani ambaye alimlipa dereva teksi.

“Kila siku unaonekana mzuri! Yaani leo ni zaidi ya jana,” alisema Hassani huku akimwangalia msichana huyo kwa macho ya nipe nikupe.

“Hahaha! Halafu wewe bwana!”
“Leo nina uhakika wa kulala na mwanamke mzuri kuliko wote duniani,” alisema Hassani huku akiupeleka mkono wake katika kiwowowo cha Catherine, msichana huyo akajifanya kushtuka kimahaba.

“Jomoniiii! Umentekenya...” alisema Catherine huku kwa sauti laini na ya kike huku akiachia tabasamu.

Alikuwa malaya, alijiuza mitaani hivyo alijua kauli zote za kumuahasisha mwanaume kupitia mwili wake. Hawakubaki hapo nje, wakaingia ndani na kwenda chumbani.

Japokuwa alikuwa akifanya kazi ya uber lakini Hassani alionekana kujiweza hasa, alijua kukipangilia chumba chake, kilionekana kuwa kizuri ambacho kilimvutia kila mtu aliyekuwa akikiangalia.
 
Sehemu ya 06.

Alining’iniza televisheni ukutano, aliweka mapazia mazito huku taa za chumba hicho zikiwa zimewekwa ukutani. Pia kulikuwa na picha kubwa nne ziliokuwa zimebandikwa kwenye kila ukuta, ukiachana na hivyo, pia kulikuwa na kitanda cha chuma ambacho kilichongwa kwa staili ya aina yake.

“Unakunywa nini?” aliuliza Hassani.
“Una nini na nini?”
“Maziwa, juisi, maji, soda, nakusikiliza wewe tu mpenzi!” alisema Hassani.

“Naomba maziwa!”
Haraka sana Hassani akalisogelea friji yake na kutoa maziwa na kumpa msichana Catherine. Kwa jinsi alivyokaa pale kwenye kitanda, gauni lake hilo likapanda na kuyafanya mapaja yake kuwa wazi kitu kilichokuwa kikimchanganya mno Hassani.

Siku hiyo akafanikiwa kufanya mapenzi na Catherine. Msichana huyo alimchanganya mno, alijua kucheza naye kila sehemu chumbani humo.

Japokuwa Hassani alionekana kuwa mwanaume balaa lakini kwa Catherine akampigia saluti yeye mwenyewe. Alikuwa akihema kama punda aliyebeba mzigo kwa masafa marefu, alichoka lakini kwa msichana huyo alionekana kama kuanza kuingia dimbani.

Mpaka wanamaliza Hassani alijilaza pembeni, alichoka, hakutaka kuchokozwa tena kwani alihisi mwili wake ukiwa umepoteza nguvu kwa kiasi kikubwa.

Catherine akalala chumbani hapo mpaka asubuhi ambapo akalipwa kiasi cha shilingi elfu hamsini na kuondoka zake huku akimshukuru Mungu kwa kumuumba mwanamke, kwani kama angekuwa mwanaume, hakujua kwa muda kama huo kiasi hicho cha pesa angekipata wapi.

.
.
 
Sehemu ya 07.

Jarida la Forbes la nchini Marekani na mtandao wake liliweka orodha mpya ya matajiri wakubwa duniani.

Kila mmoja alishtuka baada ya kuona jina la mtu aliyekuwa tajiri namba themanini, kijana wa miaka thelathini na tano, Brian Gosling akiwa amepanda kwa kasi mpaka kufikia nafasi ya tano huku akiwa na utajiri wa dola bilioni hamsini na tano ambazo zilikuwa ni zaidi ya shilingi trilioni mia moja na kumi.

Kila mmoja alishangaa, yalikuwa ni mabadiliko makubwa ambayo hapakuwa na mtu aliyeamini kama yangetokea kwa kipindi hicho. Hapo ndipo watu wakaanza kumfuatilia mwanaume huyo ambaye mpaka kipindi hicho alikuwa bachela, hakuwa ameoa kwa sababu alikuwa bize na biashara zake.

Katika kumfuatilia sana ndipo wakagundua biashara zake nyingi alizokuwa akizifanya. Kwanza alikuwa akimiliki Mtandao wa 7net ambao ulikuwa na kazi ya kuuza bidhaa mbalimbali kama ilivyokuwa Amazon ama eBay, alikuwa na vituo vingi vya mafuta ambapo aliingia ubia na kampuni kadhaa za Uarabuni ambazo zilimruhusu kuchimba mafuta yeye mwenyewe.

Alikuwa akiongoza kwa kuwa na hisa kubwa katika kampuni ya usafirishaji wa Uber. Mbali na hiyo pia alikuwa pia na hisa za kutosha katika Kampuni ya Apple huku pia akimiliki kiwanda cha Microvian ambacho kilikuwa kikitengeneza injini za ndege ndogo binafsi.

Ukiachana na hayo, pia alikuwa na kampuni yake binafsi ya magari ya kifahari aliyoyaita BriGo, jina ambalo liliunganisha majina yake mawili.

Alikuwa na utajiri mkubwa mno, alimiliki majumba mengi, hoteli kadhaa za nyota saba, boti binafsi, ndege, yaani kwa kifupi alikuwa na utajiri mkubwa.

Gosling alikuwa bize, muda wote alikuwa mtu wa kufanya kazi. Kitendo cha kutangazwa kushika namba tano katika orodha ya matajiri duniani kote, ofisi nzima ikaanza kumpigia makofi huku akipongezwa na wafanyakazi wake wote.

Waandishi wa habari hawakukaa, walikuwa bize kumtafuta mwanaume huyo, walihitaji kujua mengi kuhusu utajiri wake mkubwa na wakati alikuwa kijana mdogo kabisa.
 
Sehemu ya 08.

Walipofika na kuzungumza naye, maneno aliyowaambia yalikuwa yaleyale ambayo matajiri wengine waliwaambia kwamba kupambana, kujitoa na kuwasaidia wengine huku akiwasisitiza kuwa walitakiwa kufanya kazi kana kwamba wasingefanya tena maishani mwao.

“Unapotaka kufanikiwa, kitu cha kwanza ni lazima uwe na kiu ya kufanikiwa,” alisema Gosling huku akiwaangalia watu waliokuwa mahali hapo wakiwemo waandishi wa habari.
“Ila unaonekana kuruka kwa kasi sana, hiyo sababu inatosha?” aliuliza mwandishi wa habari kutoka katika Gazeti la New York Times.

“Nina miaka mitano sasa sijawahi kukaa sebuleni kuangalia televisheni, nina miaka sita sijawahi kulala zaidi ya saa tano kitandani mwangu, kuna mtu anaweza kufanya hivyo?” aliuliza Gosling huku akiwaangalia waandishi hao ambao nao walianza kuangaliana.

“Najua hakuna. Unapotaka kuwa bilionea ni lazima ufanye mambo mengine ambayo watu wengine hawawezi kufanya, na kila utakapowaambia, washangae, kama nyie mnavyoshangaa,” alisema Gosling.

Yeye ndiye alikuwa habari kubwa duniani, kila mtu hakuamini alichokiona, alikuwa na umri mdogo sana hivyo watu wengi kuhisi ndani ya miaka kumi ijayo angeweza kuwatetemesha watu kwa utajiri mpaka kushika nafasi ya kwanza kabisa.

Japokuwa alikuwa na utajiri mkubwa, maisha yake yalikuwa simpo kabisa, hakuwa mtu wa starehe, majivuno, alikuwa mtu mkimya aliyependa kuzungumza na watu wengi.

Alikuwa mzuri wa sura na wanawake wengi walimpenda lakini Gosling hakuwa na muda nao, alikuwa bize akiyahangaikia maisha yake kwani moja ya ndoto ambazo alikuwa nazo, kuwa bilionea wa kwanza duniani ilikuwa mbele kabisa.

“Boss! The package is here,” (Bosi! Mzigo umefika) alisikika msichana mmoja aliyekuwa akizungumza naye kwenye simu, msichana huyo aliitwa Gina Valentina.

“Where does it come from?” (Umetoka wapi?)
“Uber!”
“Ooh! Bring it to me,” (Niletee) alisema na kukata simu.

Ndani ya sekunde kumi, msichana mmoja, mrefu, mweupe aliyezifunga nywele zake kwa nyuma huku akiwa amevalia sketi iliyoishia magotini akaanza kuingia ndani ya ofisi hiyo huku akitembea kwa mwendo wa maringo.
 
Sehemu ya 09.

Alipofika katika meza ya Gosling, akamuwekea boksi ambalo akalichukua na kufungua ndani. Humo akakutana na makaratasi kadhaa aliyokuwa akiyahitaji, akayachukua na kuanza kuyaangalia.

Ilikuwa ni mikataba kadhaa ambayo alihitajika kuingia na kampuni ya Sky Broadcast ambayo ilimuomba kuwa mmoja wa watu wanaomiliki hisa katika kampuni hiyo iliyokuwa ikimiliki televisheni kadhaa nchini Uingereza ikiwemo Sky News.

Hakupenda kuwa na hisa humo lakini baada ya kuipitia na kuridhika nayo, akachukua simu yake na kupiga sehemu fulani na kuanza kuzungumza na mtu wa upande wa pili.
“Agreed!” (Imekubaliwa) alisema mara baada ya simu kupokelewa, hapohapo akakata.

Hayo ndiyo yalikuwa maisha yake, alifanya kila liwezekanalo kutafuta pesa, katika maisha yake hakutaka kuona akifeli, alijua kulikuwa na watu wengi waliokuwa wakimtegemea na kutamani kumuona akiendelea kusonga mbele, kuanguka kwake ingemfanya kuonekana mtu asiye na maana ambaye kila mmoja alitaka kuwa kama yeye.

Ilikuwa ni lazima apambane na ndiyo maana aliamua kuyaweka mapenzi pembeni kabisa na hivyo kutengeneza pesa kama alivyokuwa akifanya.

Hilo liliwapa maswali mengi marafiki zake, hawakuwahi kumuona na mwanamke yeyote, wala kusikia akizungumzia mahusiano ya kimapenzi, katika maisha hayo, kitu alichokijali kilikuwa ni kutengeneza pesa huku akiwaambia mara baada ya kuridhika na kiasi atakachokuwanacho, basi angeoa kama walivyokuwa wakimuomba kila siku.
 
Sehemu ya 10.

“When will you get married?” (Utaoa lini?) aliuliza mmoja wa wafanyakazi wake walipokuwa wakipiga stori!
“Why should I get married?” (Kwa nini nioe?)
Kila alipokuwa akiuliza swali hilo, hakukuwa na mtu aliyekuwa na majibu kwani waliamini kila kitu alichokuwa akikihitaji angeweza kukipata hata kama asingeingia kwenye ndoa.

Kama watoto angeweza kuzaa na mwanamke yeyote yule, alikuwa na uwezo wa kumuajiri mtu yeyote na kumfanyia kitu chochote alichohitaji na ndiyo maana katika kipindi hicho hakuona umuhimu wa kuoa, alichokifikiria ni kutengeneza pesa tu.

“I am telling you this! One day I will be the first person in the universe to reach 200b dollars. Just save the date,” (Nawaambieni hili! Kuna siku nitakuwa mtu wa kwanza duniani kufikisha dola bilioni 200.

Ikumbukeni hii tarehe) alisema Gosling, alikuwa akiwaambia wafanyakazi wake ambao kila siku walionekana kuwa kama ndugu zake.
“Ameeeeeennn,” waliitikia wote na kumpigia makofi.

* *
*

Catherine aliendelea kuishi maisha yake ya kujiuza, kila siku alikuwa barabarani akipigiwa simu na wanaume mbalimbali na kuambiwa alikuwa akihitajika mahali.

Aliyatoa kafara maisha yake, alikuwa tayari kupata tatizo lolote lile lakini si kuona akikosa pesa. Kila siku yeye ndiye alikuwa mtu wa kuwasiliza wateja walihitaji nini, kama walitaka kutembea naye bila mpira au watumie mpira.

Maisha yake yalikuwa hivyo, ni ya hatari lakini hakuwa na jinsi. Alifanikiwa kusimamisha mjengo ambao kipindi hicho ulikuwa kwenye hatua za mwisho kabisa.

Kila alipoiangalia nyumba yake kubwa, alimshukuru Mungu kwa kumuumba mwanamke na kumpa kitu ambacho wanaume walikitafuta kwa nguvu zote.

Siku ziliendelea kukatika kama kawaida, kila siku alikuwa mtu wa kutoka usiku na kurudi asubuhi, wakati mwingine alifanya na wanaume hata watatu pasipo kupata mimba kwa kuwa alikuwa akijichoma sindano kwa ajili ya kuzuia mimba zilizokuwa zikidumu kwa miezi mitatu ama zaidi.
 
Sehemu ya 11.

Wanaume kutoka mikoa mbalimbali walipokuwa wakifika Arusha na kuhitaji mwanamke, mtu wa kwanza kabisa kuambiwa alikuwa Catherine kwa sababu alikuwa kila kitu kitandani.

Kila mtu alimpenda kwa kuwa alijituma. Alipokea simu za wanaume wengi, waliokuwa wakilipa vizuri kiasi kwamba maisha yake yalionekana kuwa ya kitajiri na wakati hayakuwa kama watu walivyofikiria.
“Upo wapi?” lilikuwa swali la mwanaume aliyesikika kwenye simu, alikuwa akiongea na Catherine.

“Nyumbani! Wewe nani?” aliuliza msichana huyo kwa sauti nyembamba, kwa jinsi mwanaume huyo alivyosikika, hakuwa na swali alikuwa mmoja wa wanaume waliotamani sana kulala naye.

“Mimi nimekuja Arusha na nimepewa namba yako,” alisikika mwanaume huyo.
“Nikusaidie nini baba yangu?”
“Mimi ni kijana tu, si mbaba kama unavyofikiria! Nataka nikuone! Uje katika Hoteli ya Green Leaf,” alisema mwanaume huyo.

“Kufanya nini?”
“Kufanya nini tena? Si kufanya mapenzi! Au nimepewa namba ya mke wa mchungaji?” aliuliza mwanaume huyo.

“Hapana! Upo sahihi kabisa. Niambie kabisa una kiasi gani, siyo nakuja huko unaniambia una elfu hamsini, hizo kawape watoto wa sekondari wakanunue ice cream,” alisema Catherine maneno yaliyomfanya mwanaume huyo kucheka sana.

“Hahaha!”
“Unacheka tena!”
“Umenifurahisha! Sema wewe unataka kiasi gani?”

“Laki tatu!”
“Mbona gharama ndogo sana na huduma niliyoambiwa unatoa?”
“Huduma huwa na madaraja, hilo daraja la chini linaloitwa A, kuna B na lile la VIP,” alisema Catherine.

“La VIP lipoje?”
“Lipo vizuri sana, unapewa huduma zote unazozitaka, ila bei yake laki tano!” alisema Catherine, kwa mtu mzima kama yeye alipoambiwa angepewa huduma zote, alijua kabisa mwanamke huyo alimaanisha nini.
 
Sehemu ya 12.

“Basi njoo, hata milioni moja nitakulipa kama tu utanidhihirishia zile sifa nilizozisikia ni kweli,” alisema mwanaume huyo na kukata simu.

Catherine hakutaka kupoteza muda, alijiandaa vilivyo, akaenda bafuni kuoga, akajipulizia unyunyu na kuondoka kuelekea huko.

Kiasi alichotajiwa kilikuwa kikubwa mno, kwa mwanamke mtafutaji kama yeye hakutakiwa kukiacha hata kidogo. Alijiandaa haraka na baada ya kumaliza akachukua Bajaj iliyompeleka mpaka katika Hoteli ya Green Leaf iliyokuwa katikati ya Jiji la Arusha.

Alipofika huko, akampigia simu mwanaume huyo na kumwambia aende mapokezi ambapo huko amuulizie na kupelekwa katika chumba chake.

Hilo halikuwa tatizo, akaelekea na kuuliza ambapo moja kwa moja akapelekwa katika chumba cha mwanaume huyo. Alipofika na kumuona, alikuwa mwanaume wa haja, alijazia na kwa jinsi alivyoonekana, alikuwa tishio kitandani.

Akaingia, mwanaume huyo akajitambulisha kwa jina la Jericho. Alikuwa na sura ya kipole japokuwa alionekana kuwa mwiba wa kuotea mbali kitandani.

“Leo kazi ninayo,” alijisemea huku akiingia ndani ya chumba hicho.

Mwili wa Jericho ulikuwa kwenye matamanio makubwa, alipomuona msichana huyo tu, kwa jinsi alivyokuwa mzuri akashindwa kuamini kama kweli alikutana naye na kugundua alikuwa mrembo hata zaidi ya vile alivyokuwa akifikiria.

Akampeleka kitandani, kijasho chembamba kikaanza kumtoka, alichanganyikiwa. Aliwahi kulala na wanawake wengi warembo lakini kwa jinsi Catherine alivyoonekana, alikuwa balaa.
Pale kitandani, hakutaka kuchelewa, alionekana kuwa na pupa, mtu wa haraka sana, ghafla akaanza kumvua nguo Catherine, msichana huyo akamzuia.

“Subiri kwanza! Mapenzi hayatakiwi haraka! Upo kwa mtaalamu,” alisema Catherine na kumlaza kitandani, yeye akakaa juu, Jericho akaona kweli kazi ipo.

Kama alivyowafanyia wanaume wengine ndivyo alivyomfanyia hata Jericho. Mwanaume huyo alichanganyikiwa mno, hakuamini kama angekutana na mwanamke aliyekuwa akijua kama alivyokuwa huyo.

Walifanya kwa dakika kadhaa, Jericho akawa hoi, kila alipomwangalia Catherine aliona kabisa msichana huyo hakuridhika hata kidogo.
“Hivi kwa nini usiende Dar?” aliuliza Jericho huku akimwangalia Catherine.
 
Sehemu ya 13.

“Kufanya nini?”
“Kutafuta wateja wenye pesa zaidi, yaani kwa uwezo wako huu, huku Arusha unapoteza muda tu,” alisema Jericho huku akimwangalia msichana huyo.

“Hapana! Hapahapa kunatosha!”
“Mimi nataka nikufanyie mpango upige pesa zaidi, hata kama si Dar basi sehemu yoyote ile, yaani nataka nikufanyie hivi kwa sababu umenipa huduma ambayo sijawahi kuipata tangu nitoke tumboni mwa mama yangu,” alisema Jericho.

“Mpango gani?”
“Nikuunganishe na hoteli fulani ipo mbugani, huko uende kufanya biashara kwa Wazungu, ulipwe kwa dola, upo tayari?” aliuliza Jericho huku akimwangalia msichana huyo.

Kabla ya Catherine kujibu swali hilo akamwangalia mwanaume huyo, alitaka kupata uhakika kama alikuwa akimaanisha alichokizungumza au alimtania.

Alipomwangalia, alionekana kumaanisha hivyo Jericho kuchukua simu yake na kupiga kwa meneja wa hoteli ya Hakuna Matata iliyokuwa katika Mbuga ya Ngorongoro.

Alizungumza naye kwa dakika kadhaa na kukubaliana kufanya biashara na msichana huyo ambaye naye alitakiwa kulipia kiasi cha shilingi elfu hamsini kila alipokuwa akifanya mapenzi na mwanaume katika hoteli hiyo.

Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa maisha yake mengine, akahama Arusha Mjini na kuelekea katika hoteli hiyo kwenye Mbuga ya Wanyama ya Ngorongoro ambapo ndipo alitakiwa kufanya biashara.

Huko hakuwa peke yake, kulikuwa na wasichana wengine kama sita waliokuwa wakifanya kazi hiyo kama kawaida. Walikuwa wakitengeneza kiasi kikubwa cha pesa lakini ujio wa Catherine ukawa tatizo kwao kwa sababu alikuwa mrembo zaidi yao, alivutia kiasi kwamba mpaka wakati mwingine walitamani kumfukuza.

Alizoeana nao na kuanza kazi ya kutembea na watalii waliokuwa wakitembelea mbuga hiyo. Kutokana na uzuri wake, akatokea kupendwa na watu wengi, wakamfuata na kumlipa kwa dola, kwake, alimshukuru sana Jericho ambaye mara kwa mara alikuwa akimpiga simu na kuzungumza naye.

“Catherine! Nimekusaidia kwa kuwa umenifanya niingie kwenye ulimwengu mwingine wa mapenzi, yaani sikuwahi kukutana na mwanamke kama wewe,” “Usijali! Siku tukionana ndiyo utanitambua, yaani itakuwa balaa, halafu itakuwa bure kabisa,” alisema Catherine.
“Kweli?”
“Ndiyo! Utaona tu!” alisema Catherine.

|
|
 
Sehemu ya 14

Miongoni mwa wanawake waliokuwa wakimpenda Gosling alikuwa msichana Maggie Andrew ambaye alikuwa sekretari wa Gosling ofisini hapo.

Kila siku alikuwa mtu wa kutamani sana kuwa na mwanaume huyo, hakupenda kuwa naye kwa sababu alikuwa tajiri bali moyo wake ulichanganyikiwa, kufa na kuoza kwa ajili yake.

Aliwahi ofisini hapo kila siku, alifanya kazi kwa juhudi kubwa kwa kuwa alijua kabisa mtu kama Gosling, ili akupende, jambo la kwanza ulitakiwa kufanya kazi kwa nguvu zote na hivyo ndivyo alivyotaka.

Alimjua mwanaume huyo, alijua fika hakuwa na msichana yeyote, aliyafuatilia maisha yake, walikuwa wakizungumza sana na kila siku alimwambia Maggie kwamba hakufikiria kutafuta mwanamke kwa kuwa hakujisikia kuoa kipindi hicho.

Hilo lilikuwa likimfurahisha mno Maggie, alijipa uhakika kuna siku angekuwa mke wa mwanaume huyo na kuyafurahia maisha yake pamoja naye milele.

Hakuwa na presha ya kumwambia, alisubiri lakini kitu cha kwanza alitakiwa kuanza kucheza na hisia zake kwa kuamini piga ua kuna siku angekuwa naye.

Hapo ndipo alipoanza mambo yake, kila siku akawa anampelekea zawadi ndogondogo, kila alipomuona akiingia ofisini kitu cha kwanza kilikuwa ni kumsifia alipendeza, alinukia kuliko mtu yeyote ndani ya ofisi hiyo.

Maneno yote matamu ambayo binadamu wa kawaida alitakiwa kuyasikia aliambiwa Gosling, moyo wake ulifurahia pasipo kujua lengo kubwa la msichana huyo lilikuwa ni kumtia katika mikono yake.

Siku zilikatika, Gosling alikuwa bize kiasi kwamba mpaka siku yake ya kuzaliwa inafika hakuwa akikumbuka chochote kile.

Maggie alijua hilo, siku hiyo aliandaa keki nzuri na zawadi ya saa na tai nyekundu kwa ajili ya bosi wake huyo. Alimsubiri mpaka afike ofisini, alipoingia tu, akamfuata ofisini kwake na kuanza kuzungumza naye mazungumzo ya kawaida kama siku nyingine.

“Bosi! Heri ya siku ya kuzaliwa!” alisema Maggie huku akimwangalia bosi wake huyo aliyeonekana kushtuka.

“Heri ya siku ya kuzaliwa! Kwani leo lini?”
“Tarehe 5/9.”
“Oh! Ahsante sana, mambo mengi mno!”
 
Sehemu ya 15

Hapohapo Maggie akasimama na kwenda ofisini kwake, akachukua keki na zawadi zake na kurudi ofisini mule. Akamgawia zawadi zake. Palepale Gosling akavua saa yake na kuvaa ile ya Maggie, akavua tai yake na kuivaa ile aliyoletewa na msichana huyo.

“Nashukuru sana,” alisema Gosling huku akiwa na tabasamu pana.
“Karibu!” alisema Maggie na kumkumbatia mwanaume huyo.

Mambo yalianza kama utani lakini kadiri siku zilivyozidi kwenda mbele ndivyo Gosling na Maggie walivyozidi kuwa karibu. Walikuwa wakipata muda mwingi wa kuzungumza huku wakipeana zawadi za kila aina.

Kwa Gosling, alishajiahidi kamwe asingeweza kuwa kwenye uhusiano na msichana yeyote kwa sababu kichwa chake kilifikiria pesa tu lakini kwa Maggie akahisi kabisa siku si nyingi angekwenda kutekwa na penzi la msichana huyo.

Alijitahidi kumkwepa, wakati mwingine aliahidi kuwa kimya ofisini mwake lakini alishindwa kabisa kwani kila ilipofika majira ya mchana, ilikuwa ni lazima kumpigia simu na kumsalimia.

Maggie akaanza kupata nafasi ndani ya moyo wa mwanaume huyo huku naye akianza kumuweka moyoni mwake. Penzi dogo likaanza kuchipua mioyoni mwao kiasi kwamba kila mmoja akawa anamkumbuka mwenzake kila walipokuwa nyumbani kwao.

Wakawa wanawasiliana kwa simu, kila wakati walikuwa watu wa kuzungumza na wakati mwingine kwenye muda wa ziada waliongea na kutakiana usiku mwema.

Ndani ya mwezi mmoja tu, kila mmoja akatekwa na mwenzake na hatimaye kuanza kubusiana. Penzi likawateka na hakukuwa na siri tena, wawili hao wakaingia kwenye dimbwi la mapenzi, kila mfanyakazi akafahamu kilichokuwa kikiendelea.

Walitakiwa kunyamaza, Gosling hakutaka waandishi wa habari wafahamu kile kilichoendelea, ilikuwa ni lazima wanyamaze kwani kama wangefahamu kilichoendelea ilikuwa ni lazima kutangaza sana suala hilo kitu ambacho hakukitaka kabisa.

Kwa Maggie lilikuwa ni jambo lisilowezekana, kwake, kila mtu kufahamu kama alikuwa kwenye uhusiano na Gosling lilikuwa la muhimu kwake, alitaka aringe kwa wenzake, atembee barabarani huku kila mmoja akijua alikuwa mpenzi wa bilionea mkubwa duniani.
 
Sehemu ya 16

Alichokifanya ni kuwaambia marafiki zake kuhusu Gosling, wao wenyewe hawakuamini, alitamani kuwashika na kuwapeleka kwa mwanaume huyo na kuwaambia alikuwa mpenzi wake.

Ili watu wajue, akamwambia Gosling alitaka kutoka naye chakula cha usiku katika mgahawa mmoja wa watu maarufu na matajiri, hilo kwa Gosling halikuwa tatizo, akakubaliana naye na usiku wa siku husika wakaondoka na kuelekea huko.

Maggie aliwaandaa waandishi wa habari, alitaka washuhudie alikuwa mpenzi halali wa Gosling na walitakiwa kuwa hapo kwa lengo la kupiga picha na kuweka kwenye vyombo vya habari ili kila mtu ajue.

Hicho ndicho kilichofanyika, haraka sana waandishi wakafika mahali hapo hata katika kipindi ambacho Maggie na Gosling walikuwa wakiwasili mahali hapo, tayari walitegesha kamera zao na kuanza kuwapiga picha.

Hiyo ndiyo ilikuwa habari ya siku iliyofuata, kila kona kwenye magazeti, mitandao ilikuwa ni kuhusu wawili hao kutoka kimapenzi. Kwa Gosling ilikuwa ni maumivu makali, alilishika Gazeti la New York Times huku akitetemeka, hakuamini alichokuwa akikiona kwamba kila mtu alijua kilichotokea.

Hakufikiria kabisa Maggie angeweza kufanya kitu kama hicho, alichojua ni kwamba waandishi wa udaku ndiyo waliowapitishia mpaka kufahamu kilichotokea.

Penzi likawa wazi, akapigiwa simu na waandishi wa habari na kuulizwa zaidi kuhusu suala hilo, hakugoma, aliwaambia ukweli alitoka kimapenzi na msichana huyo na muda wowote ule angemuoa.

Siku zikakatika, wawili hao wakapigwa picha na kuonekana kwenye majarida mbalimbali nchini Marekani, kila mtu aliwapenda, uhusiano wao wa kimapenzi ukawafunika hata mastaa, kila kona ilikuwa ni kuwazungumzia watu hao wawili tu.

Wasichana wengi walimuonea wivu Maggie, alionekana kuwa mwenye bahati kuliko wote waliowahi kuwaona, akiwa mdogo kabisa, akapata bahati ya kuwa kwenye uhusiano na bilionea mkubwa, Gosling.

Wakati uhusiano huo ukipambana moto, Maggie akaanza kupokea simu kutoka kwa mtu aliyekuwa akimfahamu vilivyo, huyo aliitwa Andrea Milosevic, alikuwa Mserbia aliyekuwa kwenye uhusiano wake miaka miwili iliyopita.
 
Sehemu ya 17

Maggie alipoanza kupokea simu ya Andrea akaanza kuogopa, alihisi kabisa mwanaume huyo angeharibu kila kitu kama angethubutu kuweka wazi kile kilichotokea kipindi ambacho aliamua kuachana naye na kumfuata msichana mwingine.

Aliogopa na hicho ndicho kitu pekee ambacho kilimnyima raha kupita kawaida. Akawa na kazi ya kumpigia simu Andrea na kumuomba sana kwamba alitakiwa kunyamaza, hakutakiwa kuzungumza chochote kile kwani alichokiangalia ni kuolewa na mwanaume huyo na mwisho wa siku kuwa na utajiri mkubwa.
“What will you give me?” (Utanipa nini?) aliuliza Andrea kwenye simu.

“What do you want to keep you shut up,” (Unahitaji nini kunyamaza?)
“One million dollars,” (Dola milioni moja) alisema mwanaume huyo.

Kiasi alichotajiwa kilikuwa kikubwa mno, ni zaidi ya bilioni mbili za Kitanzania. Hakuwa na pesa hizo kwani hata kuolewa hakuwa ameolewa na ilikuwa vigumu kumwambia Gosling ampe kiasi hicho cha pesa.

Alimwambia Andrea kwamba alitakiwa kunyamaza na kama ingetokea akaolewa basi angmpa kiasi hicho cha pesa kwa sababu naye angekuwa sehemu ya utajiri huo.

Hilo lilikuwa gumu kukubalika kwa Andrea, alimwambia piga ua ilikuwa ni lazima apewe kiasi hicho ili aufumbe mdomo wake usizungumze kile kilichotokea.

Kwa kuwa alitamani sana ndoa na Gosling, Maggie aliomba sana kiasi kwamba Andrea akamuonea huruma na hivyo kukubaliana naye siri itunzwe mpaka siku ambayo angeolewa.

Walikubaliana kunyamaza lakini hakuwa Maggie hakuwa na furaha kabisa kwani alijua vilivyo kuwa kuna siku mwanaume huyo angezungumza kile kilichotokea na hivyo kuwa aibu kubwa kwake.

Aliendelea kuwasiliana na mwanaume huyo, alichokuwa akifanya ni kumpa pesa kidogokidogo kama kuendelea kumnyamazisha huku uhusiano wake na Gosling ukiendelea kupamba moto.

“Ila kuna siku nitamuua, bila kufanya hivyo sitokuwa na amani maisha yangu yote,” alisema Maggie huku akionekana kumaanisha alichokizungumza.

Siku zikaendelea kukatika, ili Gosling kuonyesha alimaanisha kuwa na uhusiano wa kimapenzi na msichana huyo, akaamua kuweka mikakati ya kumvisha pete ya uchumba.
 
Sehemu ya 18

Hakutaka kumwambia, aliwaambia marafiki zake tu kwamba alitaka kufanya jambo hilo muhimu sana kwao. Akawapanga, wakaandaa sehemu na kumuomba Maggie aungane nao huko.

Alipofika, alikaa naye na kuzungumza mambo mengi kama siku nyingine. Ghafla, watu waliokuwa na vyombo vya muziki wakatokea na kuanza kupiga mfululizo.

Maggie alishangaa, hakujua alichokiangalia. Watoto wawili walioshika karatasi fulani wakasimama nyuma ya Gosling, kwa mbali kabisa kiasi kwamba alikuwa akiwaona vizuri kabisa.

Hapohapo watoto hao wakafungua karatasi kubwa ambayo ilisomeka ‘Will You Marry Me?’.

Hakuamini alichokiona, alipoyarudisha macho yake kwa Gosling, mwanaume huyo akapiga magoti na kumuonyeshea pete iliyokuwa kwenye kichombo fulani kidogo.
“Gosling...is this real?” (Gosling...kinachoendelea ndicho ninachokiona?) aliuliza msichana huyo huku akishindwa kuamini.

“It is real! I love Maggie, will you marry me?” (Ndicho unachokiona! Ninakupenda Maggie, utakubali kuolewa nami?) aliuliza mwanaume huyo.

“Why not! I will,” (Kwa nini isiwezekane, nimekubali) alisema msichana huyo.
Hapohapo Gosling akamvisha pete msichana huyo kisha kusimama, akamkumbatia na ghafla vitu fulani vya kung’ang’aa vikaanza kurushwa mahali hapo kana kwamba walikuwa kwenye harusi.

Vyote hivyo viliandaliwa kwa ajili yake, Maggie alishangaa, alibaki akilia muda wote kwani kile kilichoendelea kilimshangaza na kumshtua kupita kawaida.

“I will make you happy for the rest of your life,” (Nitakufanya kuwa na furaha katika maisha yako yote) alisema Gosling na kuanza kubadilishana mate na msichana huyo ambaye mara baada ya kumkumbuka Andrea, moyo wake ukanyong’onyea na furaha kuondoka moyoni mwake.

“Kuna nini?” aliuliza Gosling huku akimwangalia Maggie.
“Hakuna kitu!”alidanganya.
“Umebadilika, ghafla tu!”

“Siamini kwa hiki unachokifanya, siamini kama mwisho wa siku nakwenda kuwa mke wako wa ndoa, ni jambo la kushangaza sana, limeanza ghafla, tumependana na hatimaye kutarajia kuingia kwenye maisha mengine.

Gosling, nitakupenda katika maisha yangu yote,” alisema Maggie na kumkumbatia tena mpenzi wake huyo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom